< 1 Samweli 2 >

1 Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
Ana je molila in rekla: »Moje srce se razveseljuje v Gospodu, moj rog je povišan v Gospodu. Moja usta so povečana nad mojimi sovražniki, ker se veselim v tvoji rešitvi duše.
2 “Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
Nihče ni svet kakor Gospod, kajti nikogar ni poleg tebe. Niti ni nobene skale, podobne našemu Bogu.
3 “Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
Ne govorite več tako silno ponosno, naj aroganca ne pride iz vaših ust, kajti Gospod je Bog spoznanja in pri njem so tehtana dejanja.
4 “Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
Loki mogočnih mož so zlomljeni in tisti, ki so se spotaknili, so opasani z močjo.
5 Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
Tisti, ki so bili siti, so se dali v najem zaradi kruha; tisti, ki so bili lačni, so oslabeli, tako, da je jalova rodila sedmero in tista, ki ima mnogo otrok, je postala slabotna.
6 “Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
Gospod ubija in oživlja. Privede dol do groba in privede gor. (Sheol h7585)
7 Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
Gospod dela revne in dela bogate, ponižuje in povzdiguje.
8 Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
Revnega vzdiguje iz prahu in berača povzdiguje iz gnojišča, da ju posadi med prince in jima stori, da podedujeta prestol slave, kajti stebri zemlje so Gospodovi in nanje je postavil zemeljski [krog].
9 Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
Varoval bo stopala svojih svetih in zlobni bodo tiho v temi, kajti noben človek ne bo prevladal z močjo.
10 wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
Gospodovi nasprotniki bodo zlomljeni na koščke. Iz nebes bo zagrmel nad njimi. Gospod bo sodil konce zemlje; moč bo dal svojemu kralju in povišal rog svojega maziljenca.«
11 Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
Elkaná je odšel v Ramo, k svoji hiši. Otrok pa je služil Gospodu pred duhovnikom Élijem.
12 Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
Torej Élijeva sinova sta bila Beliálova sinova; onadva nista poznala Gospoda.
13 Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
In običaj duhovnikov z ljudstvom je bil, da ko je katerikoli mož daroval klavno daritev, je prišel duhovnikov služabnik, medtem ko je meso vrelo, s kavljem za meso, s tremi zobmi, v svoji roki;
14 Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
in to zabodel v ponev ali kotliček ali kotel ali lonec; vse, kar so kavlji za meso prinesli gor, je duhovnik vzel zase. Tako sta počela v Šilu vsem Izraelcem, ki so prihajali tja.
15 Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
Tudi preden so sežgali tolščo, je prišel duhovnikov služabnik in rekel možu, ki je daroval: »Izroči meso za pečenje duhovniku, kajti od tebe ne bo imel kuhanega mesa, temveč surovega.«
16 Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
Če pa bi mu katerikoli moški rekel: »Naj ne izpustijo, da sedaj zažgejo tolščo, potem pa vzemi, kolikor si želi tvoja duša; « Potem bi mu odgovoril: » Ne, temveč mi boš to dal sedaj. Če pa ne, bom to vzel s silo.«
17 Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
Zato je bil greh mladeničev zelo velik pred Gospodom, kajti moža sta prezirala Gospodovo daritev.
18 Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
Toda Samuel je služil pred Gospodom, ko je bil še otrok, opasan z lanenim efódom.
19 Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
Poleg tega mu je mati iz leta v leto izdelala majhen plašč in ga prinesla k njemu, ko je prišla gor s svojim soprogom, da daruje letno klavno daritev.
20 Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
Éli je blagoslovil Elkaná in njegovo ženo ter rekel: » Gospod ti daj seme od te ženske, zaradi posojila, ki je posojen Gospodu.« In odšli so na svoj dom.
21 Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
Gospod je obiskal Ano, tako da je spočela in rodila [še] tri sinove in dve hčeri. Otrok Samuel pa je rasel pred Gospodom.
22 Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Torej Éli je bil zelo star in slišal vse, kar sta njegova sinova počela vsemu Izraelu in kako sta ležala z ženskami, ki so se zbirale pri vratih šotorskega svetišča skupnosti.
23 Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
Rekel jima je: »Zakaj počneta takšne stvari? Kajti od vsega ljudstva slišim o vajinih zlih postopanjih.
24 Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
Ne, moja sinova, kajti to ni dober glas, ki ga slišim. Vidva povzročata Gospodovemu ljudstvu, da greši.
25 Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
Če en mož greši zoper drugega, ga bo sodil sodnik, toda če mož greši zoper Gospoda, kdo bo posredoval zanj.« Vendar nista prisluhnila glasu svojega očeta, ker ju je Gospod hotel ubiti.
26 Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
Otrok Samuel pa je rasel in bil je v naklonjenosti tako z Gospodom kakor tudi z ljudmi.
27 Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
K Éliju je prišel Božji mož ter mu rekel: »Tako govori Gospod: ›Ali sem se očitno prikazal hiši tvojega očeta, ko so bili v Egiptu, v faraonovi hiši?
28 Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
In ali sem ga izbral izmed vseh Izraelovih rodov, da bo moj duhovnik, da daruje na mojem oltarju, da zažiga kadilo, da nosi efód pred menoj? In ali sem dal hiši tvojega očeta vse daritve, narejene z ognjem, Izraelovih otrok?
29 Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
Zakaj brcate ob mojo klavno daritev in ob mojo daritev, ki sem jo zapovedal v svojem prebivališču in svoja sinova bolj častiš kakor mene, da ste se odebelili z glavnimi izmed vseh daritev Izraela, mojega ljudstva?‹
30 “Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
Zato govori Gospod, Izraelov Bog: ›Zares sem rekel, da naj bi tvoja hiša in hiša tvojega očeta hodili pred menoj na veke.‹ Toda sedaj govori Gospod: ›To bodi daleč od mene, kajti tiste, ki spoštujejo mene, bom jaz spoštoval in tisti, ki me prezirajo, bodo prezirani.
31 Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
Glej, pridejo dnevi, ko bom odsekal tvoj laket in laket hiše tvojega očeta, da v tvoji hiši ne bo starca.
32 nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
In ti boš videl sovražnika v mojem prebivališču v vsem bogastvu, ki ga bo Bog dal Izraelu, in v tvoji hiši na veke ne bo starca.
33 Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
Moški od tebe, ki ga ne bom odsekal izpred svojega oltarja, bo [preostal], da použije tvoje oči in da žalosti tvoje srce in ves narast tvoje hiše bo umrl v cvetu njihove starosti.
34 “‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
To ti bo znamenje, ki bo prišlo nad tvoja dva sinova, na Hofníja in Pinhása; v enem dnevu bosta oba izmed njiju umrla.
35 Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
Jaz pa si bom dvignil zvestega duhovnika, ki bo delal glede na to, kar je v mojem srcu in v mojem umu in zgradil mu bom zanesljivo hišo; in ta bo hodil pred mojim maziljencem na veke.
36 Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”
Zgodilo se bo, da bo vsak, kdor preostane v tvoji hiši, prišel in klečeplazil k njemu za košček srebra in grižljaj kruha in rekel bo: ›Postavi me, prosim te, v eno izmed duhovniških služb, da bom lahko jedel kos kruha.‹«

< 1 Samweli 2 >