< 1 Samweli 2 >

1 Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
And Hannah prayed, and said: my heart exulteth in the LORD, my horn is exalted in the LORD; my mouth is enlarged over mine enemies; because I rejoice in Thy salvation.
2 “Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
There is none holy as the LORD, for there is none beside Thee; neither is there any rock like our God.
3 “Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
Multiply not exceeding proud talk; let not arrogancy come out of your mouth; for the LORD is a God of knowledge, and by Him actions are weighed.
4 “Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
The bows of the mighty men are broken, and they that stumbled are girded with strength.
5 Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
They that were full have hired out themselves for bread; and they that were hungry have ceased; while the barren hath borne seven, she that had many children hath languished.
6 “Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
The LORD killeth, and maketh alive; He bringeth down to the grave, and bringeth up. (Sheol h7585)
7 Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
The LORD maketh poor, and maketh rich; He bringeth low, He also lifteth up.
8 Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
He raiseth up the poor out of the dust, He lifteth up the needy from the dung-hill, to make them sit with princes, and inherit the throne of glory; for the pillars of the earth are the LORD'S, and He hath set the world upon them.
9 Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
He will keep the feet of His holy ones, but the wicked shall be put to silence in darkness; for not by strength shall man prevail.
10 wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
They that strive with the LORD shall be broken to pieces; against them will He thunder in heaven; the LORD will judge the ends of the earth; and He will give strength unto His king, and exalt the horn of His anointed.
11 Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
And Elkanah went to Ramah to his house. And the child did minister unto the LORD before Eli the priest.
12 Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
Now the sons of Eli were base men; they knew not the LORD.
13 Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
And the custom of the priests with the people was, that, when any man offered sacrifice, the priest's servant came, while the flesh was in seething, with a flesh-hook of three teeth in his band;
14 Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
and he struck it into the pan, or kettle, or caldron, or pot; all that the flesh-hook brought up the priest took therewith. So they did unto all the Israelites that came thither in Shiloh.
15 Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
Yea, before the fat was made to smoke, the priest's servant came, and said to the man that sacrificed: 'Give flesh to roast for the priest; for he will not have sodden flesh of thee, but raw.'
16 Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
And if the man said unto him: 'Let the fat be made to smoke first of all, and then take as much as thy soul desireth'; then he would say: 'Nay, but thou shalt give it me now; and if not, I will take it by force.'
17 Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
And the sin of the young men was very great before the LORD; for the men dealt contemptuously with the offering of the LORD.
18 Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
But Samuel ministered before the LORD, being a child, girded with a linen ephod.
19 Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
Moreover his mother made him a little robe, and brought it to him from year to year, when she came up with her husband to offer the yearly sacrifice.
20 Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
And Eli would bless Elkanah and his wife, and say: 'The LORD give thee seed of this woman for the loan which was lent to the LORD.' And they would go unto their own home.
21 Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
So the LORD remembered Hannah, and she conceived, and bore three sons and two daughters. And the child Samuel grew before the LORD.
22 Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Now Eli was very old; and he heard all that his sons did unto all Israel, and how that they lay with the women that did service at the door of the tent of meeting.
23 Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
And he said unto them: 'Why do ye such things? for I hear evil reports concerning you from all this people.
24 Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
Nay, my sons; for it is no good report which I hear the LORD'S people do spread abroad.
25 Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
If one man sin against another, God shall judge him; but if a man sin against the LORD, who shall entreat for him?' But they hearkened not unto the voice of their father, because the LORD would slay them.
26 Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
And the child Samuel grew on, and increased in favour both with the LORD, and also with men.
27 Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
And there came a man of God unto Eli, and said unto him: 'Thus saith the LORD: Did I reveal Myself unto the house of thy father, when they were in Egypt in bondage to Pharaoh's house?
28 Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
And did I choose him out of all the tribes of Israel to be My priest, to go up unto Mine altar, to burn incense, to wear an ephod before Me? and did I give unto the house of thy father all the offerings of the children of Israel made by fire?
29 Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
Wherefore kick ye at My sacrifice and at Mine offering, which I have commanded in My habitation; and honourest thy sons above Me, to make yourselves fat with the chiefest of all the offerings of Israel My people?
30 “Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
Therefore the LORD, the God of Israel, saith: I said indeed that thy house, and the house of thy father, should walk before Me for ever; but now the LORD saith: Be it far from Me: for them that honour Me I will honour, and they that despise Me shall be lightly esteemed.
31 Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
Behold, the days come, that I will cut off thine arm, and the arm of thy father's house, that there shall not be an old man in thy house.
32 nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
And thou shalt behold a rival in My habitation, in all the good which shall be done to Israel; and there shall not be an old man in thy house for ever.
33 Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
Yet will I not cut off every man of thine from Mine altar, to make thine eyes to fail, and thy heart to languish; and all the increase of thy house shall die young men.
34 “‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
And this shall be the sign unto thee, that which shall come upon thy two sons, on Hophni and Phinehas: in one day they shall die both of them.
35 Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
And I will raise Me up a faithful priest, that shall do according to that which is in My heart and in My mind; and I will build him a sure house; and he shall walk before Mine anointed for ever.
36 Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”
And it shall come to pass, that every one that is left in thy house shall come and bow down to him for a piece of silver and a loaf of bread, and shall say: Put me, I pray thee, into one of the priests' offices, that I may eat a morsel of bread.'

< 1 Samweli 2 >