< 1 Samweli 19 >
1 Sauli akamwambia mwanawe Yonathani na watumishi wake wote wamuue Daudi. Lakini Yonathani mwana wa Sauli alimpenda sana Daudi.
Şaulee cune duxayk'le Yonatanık'leyiy cune hiqiy-allanbışik'le Davud gik'eva eyhe. Yonatanısmee, Davud geer ıkkan ıxha.
2 Yonathani akamwonya Daudi, akisema, “Baba yangu Sauli anatafuta nafasi ya kukuua. Ujilinde kesho asubuhi, nenda mahali pa siri na ukae huko.
Yonatanee Davudulqa xabar g'uxoole: – Yizde dekkıs Şaulus ğu gik'asır ıkkan. Həşdiyle, hucoon ixhes, ğucar ğu g'iyqa miç'eer havace. Sa ciga t'abal hı'ı, çolee dyugulyxhe.
3 Nitatoka na kukaa na baba yangu shambani mahali uliko. Nitazungumza naye juu yako, nami nitakueleza nitakachogundua.”
Zınar dekkıkasana çoleeqa, ğu dyugulyxhayne cigaysqa, ayres. Mang'uka yiğne hək'ee yuşan ha'as, mang'vee hucooyiy uvhu zı valqa hixhar ha'asın.
4 Yonathani akanena mema juu ya Daudi kwa Sauli baba yake na kumwambia, “Mfalme asitende mabaya kwa mtumishi wake Daudi; hajakukosea, aliyoyafanya yamekuwa ya faida sana kwako.
Yonatanee dekkıs Şaulus, Davudne hək'ee yugun karbı yuşan hı'ı, eyhen: – Paççahee, cune nukarıs Davudus pisvalla hımaa'acen. Mang'vee vas mısacab pisvalla hav'u deş. Mang'vee hı'iyn gırgın işbıd, yiğne yugvalinemee ıxha.
5 Alihatarisha maisha yake alipomuua yule Mfilisti. Bwana akajipatia ushindi mkubwa kwa ajili ya Israeli wote, nawe uliuona na ukafurahi. Kwa nini basi utende mabaya kwa mtu asiye na hatia kama Daudi kwa kumuua bila sababu?”
Mang'vee, qik'uyle qı'dərq'ı'n Filiştinğançena Golyat gik'u, Rəbbeeyib İzrail g'attivxhan hav'u. Ğunar man g'acu, şadxhana. Nya'a ğu nişilycar-alla taxsir deşda Davud gik'u, q'ərane cigeeqa eb k'yaavak'an hav'u, vasda bınah haa'as?
6 Sauli akamsikiliza Yonathani na kuapa hivi: “Hakika kama Bwana aishivyo, Daudi hatauawa.”
Şaulee Yonatanne cuvabıl k'ırı alixhxhı, «Zı mana gik'as deşva» uvhu, Vorne Rəbbine hək'ee k'ın g'iysar.
7 Basi Yonathani akamwita Daudi na kumweleza mazungumzo yote. Akamleta kwa Sauli, naye Daudi akawa pamoja na Sauli kama kwanza.
Yonatanee Davud qort'ul, co yuşan hı'iyn gırgın mang'us yuşan ha'a. Qiyğar, Davud Şaulusqa ıkkekka. Davudur şenkiyn xhinne, Şaulusnee axva.
8 Vita vilitokea tena, naye Daudi akatoka na kupigana na Wafilisti. Akawapiga kwa nguvu nyingi hata wakakimbia mbele yake.
Meeb dəv'ə giviyğal. Davudur oza qıxha ayk'anna Filiştinaaşika saç'ikkvas. Davud manbı ootal-ooxhal hav'u, ğamexhena, manbı Davudne ögiyle heebaxanbı.
9 Lakini roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Bwana ikaja juu ya Sauli alipokuwa ameketi katika nyumba yake akiwa na mkuki mkononi mwake. Daudi alipokuwa anampigia kinubi,
Yiğbışde sa yiğıl Şaul xaa'ar xıle nizeyka gyu'uringa, mang'ulqa Rəbbee g'axuvuyn pisın rı'hı'd qadı gexa. Davudee mane gahıl lira ı'lyviyxə vooxhe.
10 Sauli akajaribu kumchomea Daudi ukutani kwa huo mkuki wake, lakini Daudi akauhepa huo mkuki wa Sauli ukakita ukutani. Usiku ule ule Daudi akakimbia na kuokoka.
Şaulus Davud nizeyka barugus at'iq'an ha'as ıkkiykan. Davud mang'une ögiyle hexvana, mang'vee avhuyn nized qadı barugeeqa k'exa. Mane xəmde Davud hixu g'ittiyxhanna.
11 Sauli akatuma watu nyumbani mwa Daudi wailinde hiyo nyumba na kumuua asubuhi. Lakini Mikali, mkewe Daudi, akamwonya akisema, “Kama hukukimbia kuokoa maisha yako usiku huu, kesho yake utauawa.”
Şaulee Davudne xaaqa insanar g'ıxoole, mana nyaariyva ats'axhxha, miç'eer g'ik'ecenva. Davudne xhunaşşee Mikalee, mang'us xabar huvu eyhen: – G'iyna xəmde vasse, hixu dyugulyxhes dəxeene, g'iyqa miç'eer ğu g'ik'asda.
12 Basi Mikali akamteremsha Daudi kupitia dirishani, naye akakimbia na kuokoka.
Qiyğa Mikalee Davud g'uleençe gyaqqa, manar hixu g'ittiyxhanna.
13 Kisha Mikali akachukua kinyago, akakilaza kitandani, akakifunika kwa vazi na kukiwekea singa za mbuzi kichwani.
Mikalee xaana byuty alyapt'ı tyuleeqa giviyxhe, vuk'lelqad ç'ərnan ts'e'ın g'ekva qali'ı, ooqad tanalinbı adaççe.
14 Sauli alipotuma watu kumkamata Daudi, Mikali akasema, “Yeye ni mgonjwa.”
Şaulee, Davud aqqasva g'axuvuyn insanar abımee, Mikalee «Mana ık'ar vorva» eyhe.
15 Kisha Sauli akatuma watu tena kumwona Daudi naye akawaambia, “Mleteni kwangu juu ya kitanda chake ili nipate kumuua.”
Şaulee mebın insanar g'axuvu, eyhen: – Mana tyulyunukacar zasqa ayre, zı mana gik'as.
16 Lakini wale watu walipoingia, kumbe ni kinyago tu kilichokuwa kitandani na kwenye kichwa kulikuwepo na singa za mbuzi.
Man insanar aqa ikkeepç'ımee g'ecen, tyuleeqa, vuk'lelqa ts'e'ın g'ekva qali'ıyn byutud hotku.
17 Sauli akamwambia Mikali, “Kwa nini umenidanganya mimi hivi na kumwacha adui yangu aende zake ili apate kuokoka?” Mikali akamwambia, “Yeye aliniambia, ‘Niache niende zangu. Kwa nini nikuue?’”
Şaulee Mikalık'le eyhen: – Nya'a zas horbı hı'ı? Yizda duşman g'aykkı, manar hixu g'attirxhınna. Mikalee Şaulus alidghıniy qele: – Davudee zak'le uvhuyn, g'aykke zı əlyhəəs! Deşxheene, zı ğu giyk'as!
18 Daudi alipokuwa amekimbia na kuokoka, alimwendea Samweli huko Rama na kumwambia yale yote Sauli alimfanyia. Ndipo Daudi na Samweli wakaenda Nayothi kukaa huko.
Davud hixu g'attirxhınmee, Ramayeeqa Şamuelyne k'anyaqa qarı, Şaulee cuk hı'iyn gırgın mang'us yuşan ha'an. Mançile qiyğa mana Şamuelika sacigee Nayot eyhene şahareeqa ark'ın, maa aaxva.
19 Habari zikamfikia Sauli kusema: “Daudi yuko Nayothi huko Rama.”
Şaulus «Davud Ramayeene Nayoturva» xabar qabayle.
20 Basi Sauli akatuma watu kumkamata Daudi, lakini walipoona kundi la manabii wakitoa unabii, wakiwa pamoja na Samweli akiwa amesimama hapo kama kiongozi wao, Roho wa Mungu akaja juu ya watu wa Sauli, nao pia wakatoa unabii.
Şaulee mana aqqasva, maqa insanar g'ıxoole. İnsanaaşik'le, Şamuel q'oma ulyorzulyne peyğambaraaşine desteyn peyğambariyvalla haa'a g'ooce. Man g'acumee, Şaulee g'axuvuyne insanaaşilqad Allahın Rı'h geç'e. Manbışeb peyğambariyvalla haa'a giviyğal.
21 Sauli akaelezwa juu ya hilo, naye akapeleka watu wengine zaidi, nao wakatoa unabii pia. Sauli akatuma watu mara ya tatu, nao pia wakatoa unabii.
Man ıxhaynbı Şaululqa hixhar hı'ımee, mang'vee mebın insanar g'ıxoole. Manbışeb peyğambariyvalla haa'a. Şaulee, xhebe'es insanar g'uxoole, manbışeb peyğambariyvalla haa'a.
22 Mwishowe, yeye mwenyewe akaondoka kwenda Rama na kwenda hadi kwenye kile kisima kikubwa kilichoko huko Seku. Naye akauliza, “Wako wapi Samweli na Daudi?” Wakasema, “Wako Nayothi huko Rama.”
Nekke qiyğa vuccar Ramayeeqa arı, Seku eyhene cigayne k'anene, xənne kahrızısqa qarı, maane insanaaşike qiyghanan: – Şamueliy Davud nyaane vob? Maane neng'veemee, «İnyaa'ab, Ramayeene Nayotee vobva» eyhe.
23 Hivyo Sauli akaenda Nayothi huko Rama. Lakini Roho wa Mungu akaja juu yake hata yeye, akawa anatembea huku anatoa unabii hadi akafika Nayothi.
Şaul Ramayeene Nayotqa əlyhəəmee, mana Allahne Rı'hı'n aqqaqqa. Qıyğar insanaaşe Şaul Ramayeene Nayotulqa qıkkeka. Mang'veeyib peyğambariyvalla haa'a vuxha.
24 Akavua majoho yake na pia akatoa unabii mbele ya Samweli. Akalala hali hiyo ule mchana kutwa na usiku kucha. Hii ndiyo sababu watu husema, “Je, Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?”
Qiyğa mang'vee tanalinbı qakki'ı, Şamuelyne ögil peyğambariyvalla haa'a. Mana bıkırne yiğnayiy xəmna ts'eler qukyork'ul axva. Mançil-alla insanaaşe eyhe: «Şaulıkerne peyğambar ıxha?»