< 1 Samweli 19 >
1 Sauli akamwambia mwanawe Yonathani na watumishi wake wote wamuue Daudi. Lakini Yonathani mwana wa Sauli alimpenda sana Daudi.
Solo da egefe Yonada: ne amola ea ouligisu dunu huluane ilima e da Da: ibidi fane legemusa: sia: ilegei. Be Yonada: ne da Da: ibidima bagade dogolegei galu.
2 Yonathani akamwonya Daudi, akisema, “Baba yangu Sauli anatafuta nafasi ya kukuua. Ujilinde kesho asubuhi, nenda mahali pa siri na ukae huko.
Amaiba: le, Yonada: ne da Da: ibidima amane sia: i, “Na ada da di fane legemusa: logo hogolala. Aya hahabe noga: le dawa: ma! Wamoaligisu soge hogole, amogawi esaloma!
3 Nitatoka na kukaa na baba yangu shambani mahali uliko. Nitazungumza naye juu yako, nami nitakueleza nitakachogundua.”
Na da ada ani asili, dia wamoaligi dialebe amo gadenene aligili, dimadi sia: na adama sia: mu. Na da dima hamomu sia: nabasea, amo dima adomu.”
4 Yonathani akanena mema juu ya Daudi kwa Sauli baba yake na kumwambia, “Mfalme asitende mabaya kwa mtumishi wake Daudi; hajakukosea, aliyoyafanya yamekuwa ya faida sana kwako.
Yonada: ne da Soloma Da: ibidi ea hou nodone olelei. E amane sia: i, “Ada! Dia hawa: hamosu dunu Da: ibidima mae giadofale hamoma. E da dima giadofale hamedafa hamoi. Be e da dima giadofale mae hamone, e da dima fidisu hou baligili bagadedafa hamoi.
5 Alihatarisha maisha yake alipomuua yule Mfilisti. Bwana akajipatia ushindi mkubwa kwa ajili ya Israeli wote, nawe uliuona na ukafurahi. Kwa nini basi utende mabaya kwa mtu asiye na hatia kama Daudi kwa kumuua bila sababu?”
E da ea esalusu mae dawa: le, Goulaia: de fane legei. Amalalu, Hina Gode da Isala: ili fi ilia baligili hasalasimusa: hamonesi. Di da amo ba: loba, nodoi. Amaiba: le, di da abuliba: le hame giadofasu dunu amo bai hamedenewane fane legemusa: dawa: bela: ?”
6 Sauli akamsikiliza Yonathani na kuapa hivi: “Hakika kama Bwana aishivyo, Daudi hatauawa.”
Solo da Yonada: ne ea sia: nababeba: le, dafawaneyale dawa: i. E da Hina Gode Ea Dioba: le, Da: ibidi ea hame fane legemu ilegele sia: i.
7 Basi Yonathani akamwita Daudi na kumweleza mazungumzo yote. Akamleta kwa Sauli, naye Daudi akawa pamoja na Sauli kama kwanza.
Amaiba: le, Yonada: ne da Da: ibidi wele guda: le, Solo ea sia: i liligi huluane ema adole i. Amalalu, e da Da: ibidi amo Soloma oule asili, Da: ibidi da ea musa: hamoi defele bu Solo ea hawa: hamosu.
8 Vita vilitokea tena, naye Daudi akatoka na kupigana na Wafilisti. Akawapiga kwa nguvu nyingi hata wakakimbia mbele yake.
Filisidini dunu amola Isala: ili dunu da bu gegei. Da: ibidi da ilima doagala: le, ilima noga: le hasalasibiba: le, Filisidini dunu da hobeale afia: su.
9 Lakini roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Bwana ikaja juu ya Sauli alipokuwa ameketi katika nyumba yake akiwa na mkuki mkononi mwake. Daudi alipokuwa anampigia kinubi,
Ha afaega, wadela: i a: silibu Hina Godemadi misi da Soloma aligila sa: i. E da hi diasua goge agei hi loboa gaguli esalu, amo Da: ibidi da amoga ea sani baidama dusa esalu.
10 Sauli akajaribu kumchomea Daudi ukutani kwa huo mkuki wake, lakini Daudi akauhepa huo mkuki wa Sauli ukakita ukutani. Usiku ule ule Daudi akakimbia na kuokoka.
Solo da ea goge agei amoga Da: ibidi dobeala bobodole danoma: nesimusa: gala: le ba: i. Be Da: ibidi da giadofale, goge agei da dobea damana nudasi. Da: ibidi da hame ludiba: le, hobeale asi.
11 Sauli akatuma watu nyumbani mwa Daudi wailinde hiyo nyumba na kumuua asubuhi. Lakini Mikali, mkewe Daudi, akamwonya akisema, “Kama hukukimbia kuokoa maisha yako usiku huu, kesho yake utauawa.”
Amogala gasiawane, Solo da Da: ibidi ea diasu ba: lesili hahabe fama: ne, hawa: hamosu dunu asunasi. Da: ibidi idua Maiga: le da ema amane sisa: i, “Di da wali gasia hame hobeale dasea, aya medole legei dagoi ba: mu.”
12 Basi Mikali akamteremsha Daudi kupitia dirishani, naye akakimbia na kuokoka.
Maiga: le da Da: ibidi fo misa: ne agenesi gelabodi amoga gudu asunasia guduli, e da hobea: i.
13 Kisha Mikali akachukua kinyago, akakilaza kitandani, akakifunika kwa vazi na kukiwekea singa za mbuzi kichwani.
Amalu, e da dununa hamoi ogogosu ‘gode’ liligi diasua bugisi amo lale, diaheda: su da: iya diasili, goudi hinaboga hamoi dialuma fugululisili, abula sosonesi.
14 Sauli alipotuma watu kumkamata Daudi, Mikali akasema, “Yeye ni mgonjwa.”
Solo ea dunu da Da: ibidi lala manoba, Maiga: le da ilima amane sia: i, “E da oloi diala.”
15 Kisha Sauli akatuma watu tena kumwona Daudi naye akawaambia, “Mleteni kwangu juu ya kitanda chake ili nipate kumuua.”
Be Solo da ea hawa: hamosu dunu ilia siga Da: ibidi oloi dialebe ba: ma: ne bu asunasi. E ilima amane sia: i, “Ea diaheda: su da: iya dialebe, amo goeguda: gaguli misa. Amasea, na da e medole legemu.”
16 Lakini wale watu walipoingia, kumbe ni kinyago tu kilichokuwa kitandani na kwenye kichwa kulikuwepo na singa za mbuzi.
Ilia da ganodini sa: ili ba: loba, dununa hahamoi liligi amo da goudi hinaboga hamoi busafugululi diasi dialebe ba: i.
17 Sauli akamwambia Mikali, “Kwa nini umenidanganya mimi hivi na kumwacha adui yangu aende zake ili apate kuokoka?” Mikali akamwambia, “Yeye aliniambia, ‘Niache niende zangu. Kwa nini nikuue?’”
Solo da Maiga: lema adole ba: i, “Di da abuliba: le na ha lai hobeama: ne nama ogogobela: ?” Maiga: le da bu adole i, “Na da e hobeama: ne hame fidisia, e da na fane legemu sia: i.”
18 Daudi alipokuwa amekimbia na kuokoka, alimwendea Samweli huko Rama na kumwambia yale yote Sauli alimfanyia. Ndipo Daudi na Samweli wakaenda Nayothi kukaa huko.
Da: ibidi da hobeale, La: ima sogega, Sa: miuelema asili, Solo ea ema hamoi liligi huluane ema adole i. Amalu, e amola Sa: miuele ela da Na: iode amoma asili esalu.
19 Habari zikamfikia Sauli kusema: “Daudi yuko Nayothi huko Rama.”
Solo da Da: ibidi amo da Na: iode sogebi, La: ima soge amo ganodini esalebe nabi.
20 Basi Sauli akatuma watu kumkamata Daudi, lakini walipoona kundi la manabii wakitoa unabii, wakiwa pamoja na Samweli akiwa amesimama hapo kama kiongozi wao, Roho wa Mungu akaja juu ya watu wa Sauli, nao pia wakatoa unabii.
Amaiba: le, e da dunu amo Da: ibidi gagula masa: ne asunasi. Ilia da asili ba: loba, Sa: miuele hi ouligili balofede dunu huluane gilisi da hoahoasa gogosa: dalebe ba: i. Amalu, Hina Gode Ea A: silibu Hadigidafa da Solo ea dunu ilima aliligila dabeba: le, ilia amola da momadelale hoahoasa gogosa: dusa: i.
21 Sauli akaelezwa juu ya hilo, naye akapeleka watu wengine zaidi, nao wakatoa unabii pia. Sauli akatuma watu mara ya tatu, nao pia wakatoa unabii.
Solo da amo sia: nababeba: le, e da dunu eno dewane asunasi. Be ilia amola da amanewane momadelale hoahoasa gogosa: dusa: i. E da dunu mogi osoda eno asunasi, be ilia da amanewane hamoi.
22 Mwishowe, yeye mwenyewe akaondoka kwenda Rama na kwenda hadi kwenye kile kisima kikubwa kilichoko huko Seku. Naye akauliza, “Wako wapi Samweli na Daudi?” Wakasema, “Wako Nayothi huko Rama.”
Amalalu, Solo hi bisili La: ima soge amoga masusa: asi. E da hano si bagade Sigu sogebiga dialu amoga doaga: le, Sa: miuele amola Da: ibidi da habia: le nababa: loba, ela da Na: iode sogega esalayabe nabi.
23 Hivyo Sauli akaenda Nayothi huko Rama. Lakini Roho wa Mungu akaja juu yake hata yeye, akawa anatembea huku anatoa unabii hadi akafika Nayothi.
Solo da amoga ahoanoba, Gode Ea A: silibu da ema aligila sa: ili, e da hoahoasa gogosa: ahoana, Na: iode sogebiga doaga: i.
24 Akavua majoho yake na pia akatoa unabii mbele ya Samweli. Akalala hali hiyo ule mchana kutwa na usiku kucha. Hii ndiyo sababu watu husema, “Je, Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?”
Solo da Sa: miuele ea si da: iyawane hoahoasa, abula huluane gigisa: le fasili gogosa: lalu, amo esoha amola gasia e da da: i nabado solegadole gebewane dialu. (Amo hou hamobeba: le, fa: no dunu da amane sia: dasu, “Solo da balofede dunu hamobela: ?”)