< 1 Samweli 18 >

1 Baada ya Daudi kumaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ikaambatana na roho ya Daudi, naye akampenda kama nafsi yake mwenyewe.
Davud Şauluka yuşan hı'ı ç'əvxhayle qiyğa, Yonatanne yik'esqa Davud yugra qarayle. Mang'us Davud vuc xhinne ıkkiykan giyğal.
2 Kuanzia siku ile Sauli akamchukua Daudi naye hakumruhusu kurudi nyumbani kwa baba yake.
Mane yiğıle Şaulee Davud cune k'ane aqqaqqa, dekkıne xaaqa əlyhəəs haysar deş.
3 Yonathani akafanya agano na Daudi kwa sababu alimpenda kama nafsi yake mwenyewe.
Mana vuc xhinne geer ıkkanva Yonatanee Davuduka hambaziyvalla haa'asva cuvab g'ats'ayk'van.
4 Yonathani akavua joho alilokuwa amevaa na kumpa Daudi, pamoja na koti lake, silaha zake, hata pamoja na upanga wake, upinde wake na mshipi wake.
Yonatanee tanalinbı g'ayşu, g'ılıncıka, vukuka, zirehıka sacigee ts'irab Davudusqa qoole.
5 Lolote Sauli alilomtuma Daudi kufanya, alitenda kwa hekima, hata Sauli akampa cheo cha juu katika jeshi. Jambo hili likawapendeza watu wote, hata maafisa wa Sauli pia.
Şaulee Davud nene işiqar qihna g'axuvee, mang'vee mana iş yugba haa'a vuxha. Mançil-allar Şaulee Davuduke cune g'oşunee ç'ak'ınbışda sa ha'a, man milletned, Şaulne hiqiy-allanbışded ulesqa yugda qadayle.
6 Watu walipokuwa wanarudi nyumbani baada ya Daudi kumuua yule Mfilisti, wanawake wakaja kutoka pande zote za miji ya Israeli kumlaki Mfalme Sauli kwa kuimba na kucheza, kwa nyimbo za furaha na kwa matari na zeze.
Davudee Filiştinğançena gik'u yı'q'əlqa siyk'almee, İzrailyne gırgıne şaharbışeençen yedar dyafbıyiy t'amp'ırbı alyaat'u, şadeebaxhen mə'niybıyiy mık'ar ha'a paççah Şaulne ögeeqa qığeebaç'e.
7 Walipokuwa wanacheza, wakaimba: “Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake.”
Yedaaşe mık'ar ha'a-ha'a, inəxdın mə'niybı qədəqqə ıxha: – Şaulee aazırbışika, Davudemee, yits'ıd aazırbışika gyapt'ı.
8 Sauli akakasirika sana; sehemu hii ya kurudia rudia ya wimbo huu ilimkasirisha sana. Akafikiri kuwa, “Wamempa Daudi makumi elfu, lakini mimi wamenipa elfu tu. Apate nini zaidi isipokuwa ufalme?”
Şaulus mançike geeb qəl vooxhe, manbışe eyhenbı mang'une yik'eençe eyxhe deş. Mang'vee eyhen: – Davudee yits'ıd aazırıka, zımee aazırıkava manbışe eyhe. Sık'ınne gahıle manbışis mang'uke paççahcar ha'as ıkkiykanas.
9 Kuanzia wakati ule na kuendelea Sauli akawa na jicho la wivu juu ya Daudi.
Mane yiğıle Şaul Davuduqa sacurayracar ilyakka giyğal, mang'vee Davudus paxıliyvalla haa'a.
10 Kesho yake roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Mungu ikaja kwa nguvu juu ya Sauli. Alikuwa akitabiri nyumbani mwake, wakati Daudi alikuwa akipiga kinubi, kama alivyozoea. Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake;
Qinne yiğıl Allahee g'axuvuyn pisın rı'h Şaululqa gexa. Mang'vee xaa nen qadiy ha'a giyğal. Davudeeme, vucee ögiyl ha'an xhinne, meeb xılyaqa lira alyapt'ı mana ilyviyxə vuxha. Şaulne xıle nize eyxhe.
11 akautupa kwa nguvu, akijiambia mwenyewe, “Nitamchoma kwa mkuki abaki hapo ukutani.” Lakini Daudi akamkwepa mara mbili.
Şaulee «Hasre Davud ine nizeyka baruguk at'iq'an ha'asva» culed-alqa uvhu, man xıledın nize ayhen. Davudusse q'öne yəqqee mançike hixvas əxəna.
12 Sauli akamwogopa Daudi, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Daudi, lakini alikuwa amemwacha yeye.
Rəbbee Davudun sura aqqıva, vucur g'alerçuva, Şaul Davudule qəyq'ənna.
13 Kwa hiyo Sauli akamwondoa Daudi mbele yake na kumpa kuwa kiongozi wa watu elfu moja, naye Daudi akatoka na kuingia akiongoza vikosi katika vita.
Mançil-allar Şaulee Davud cuke əq'əna qı'ı, mang'uke aazırıng'una xərna hı'ı. Mançile qiyğa Davudee g'oşun dəv'eeqa vukku qadayle ıxha.
14 Katika kila kitu alichofanya, Daudi alipata mafanikio makubwa, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja naye.
Rəbb Davuduka vorva, mang'une xılençe gırgın işbı qöö ıxha.
15 Sauli alipoona jinsi alivyokuwa akifanikiwa, akamwogopa.
Davudne xılençe gırgın qöö g'acu, Şaul qəyq'ənna.
16 Lakini Israeli wote na Yuda walimpenda Daudi, kwa sababu ndiye alikuwa akiwaongoza katika vita vyao.
Gırgıne İzrailybışisiy Yahudabışis Davudee co dəv'eeqa vukku qavayleva, mana geer ıkkan ıxha.
17 Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupa umwoe, endapo tu utanitumikia kwa ushujaa na kupigana vita vya Bwana.” Kwa maana Sauli alisema moyoni mwake, “Sitainua mkono wangu dhidi yake. Acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
Şaulee Davuduk'le eyhen: – İna yizda xərna yiş, Merav vorna, mana zı vas heyles. Saccu ğu yizde yəqqə yik'eka ixhe, Rəbbinab dəv'ə vukkee. Şaulne fıkıreençe «Hasre mana yizde deş, Filiştinaaşde xıle qik'ecenva» ılğeç'e.
18 Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, nayo jamaa yangu ni nini au ukoo wa baba yangu katika Israeli, kwamba mimi niwe mkwewe mfalme?”
Davudee Şauluk'le eyhen: – Nya'a, zı vuşune eyxhe? Yizda xizan hucoo eyhen karne, dekkına xizanıb İzrailee şavunbışdane vob, zake paççahıs yezne ixhes?
19 Basi ulipofika wakati wa Daudi kupewa Merabu, binti Sauli, huyo binti aliozwa kwa Adrieli, Mmeholathi.
Şaulna yiş Merav, Davudus heylesda gah qabımee, mana Mexolğançene Adrielis heele.
20 Basi Mikali binti Sauli alimpenda Daudi, nao walipomwambia Sauli juu ya jambo hili, likampendeza.
Davudmee, Şaulne manisa yişşis Mikalıs ıkkiykan. Mançina gaf Şaululqa hivxhar hav'umee, mana mang'une yik'eençe vooxhe.
21 Sauli akawaza, “Nitampa Daudi binti yangu, ili apate kuwa mtego kwake, ili kwamba mkono wa Wafilisti upate kuwa juu yake.” Hivyo Sauli akamwambia Daudi, “Sasa unayo nafasi ya pili ya kuwa mkwe wangu.”
Şaulne fıkreençe «Davudus Mikal hiyvu, mang'us gugu haa'as, Davud Filiştinaaşde xıleka gik'asva» ılğeç'e. Qiyğa Şaulee Davuduk'le eyhen: – Vasse g'iyna meer yizda yezne ixhes əxə.
22 Ndipo Sauli akawaagiza watumishi wake, akisema, “Zungumzeni na Daudi kwa siri na kumwambia, ‘Tazama, mfalme amependezwa nawe, nao watumishi wake wote wanakupenda. Basi na uwe mkwewe mfalme.’”
Şaulee cone hiqiy-allanbışilqa əmr haa'a, Davuduk'le dyugulenda inəxüd eyheva: – İlekke paççahıs ğu nimeeyiy ıkkan, mang'une hiqiy-allanbışisir ğu ıkkanna. Qora ğu həşde mang'us yezne ixhe.
23 Watumishi wa Sauli wakarudia hayo maneno kwa Daudi. Lakini Daudi akasema, “Je, mnafikiri ni jambo dogo kuwa mkwewe mfalme? Mimi ni mtu maskini tu, na nisiyejulikana sana.”
Şaulne hiqiy-allanbışe, Davudus man g'ayxha'ang'a, Davudee manbışik'le eyhen: – Paççahna yezne ıxhay, vuşdemee nəxdın ıxhay karne vod? Zı kar deşda, şavuk'lecar dyats'ana insan vor.
24 Watumishi wa Sauli walipomweleza yale Daudi aliyoyasema,
Şaulne hiqiy-allanbışe «Davudee inva uvhuva» Şaululqa hixhar ha'a.
25 Sauli akajibu, “Mwambieni Daudi, ‘Mfalme hataki zawadi nyingine kuwa mahari isipokuwa magovi 100 ya Wafilisti, ili kulipiza kisasi juu ya adui zake.’” Mawazo ya Sauli yalikuwa Daudi akaanguke mikononi mwa Wafilisti.
Şaulee eyhen: – Davuduk'le eyhe: «Paççahee vake, yişşel-alla pıl deş heqqa. Mang'vee vake, çine cigee, cuna qəl qığaahasva, cune duşmanaaşin vəşne Filiştinğançeng'un sunnat hı'iyn ç'ürüx heqqa». Manıd Şaulee, Davud Filiştinaaşde xıleka gik'asva ha'a.
26 Watumishi walipomwambia Daudi mambo haya, ikampendeza kuwa mkwewe mfalme. Basi kabla siku iliyopangwa haijafika,
Şaulne hiqiy-allanbışe man eyhenbı Davudulqa hixhar ha'anbı. Davudusur yezne ixhes ıkkiykkanna. Gyuvxhuna gah g'avalessecab,
27 Daudi na watu wake walitoka na kuwaua Wafilisti mia mbili. Akayaleta magovi yao na kupeleka hesabu kamilifu kwa mfalme, ili kwamba apate kuwa mkwewe mfalme. Ndipo Sauli akamwoza Daudi Mikali binti yake.
Davud cune g'oşunıka hark'ın Filiştinaaşda q'öd vəş adamiy gek'a. Paççahna yezne ixhesdemee, Davudee manbı sunnat hav'u ıxhayn ç'ürüxbı paççahısqa adayle. Manke Şauleeyir cuna yiş Mikal Davudus heelena.
28 Sauli alipotambua kuwa Bwana alikuwa pamoja na Daudi na kwamba Mikali binti yake anampenda Daudi,
Şaululqa hitxhırmee, Rəbb Davuduka vorva, yişşes Mikalısır Davud ıkkanırva,
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi, naye Sauli akabaki kuwa adui yake siku zote za maisha yake.
mana mang'ule sık'ırar geer qəyq'ən giyğal. Qik'asmeeyir mana Davudna duşman eyxhe.
30 Majemadari wa jeshi la Wafilisti waliendelea kupigana vita na kadiri walivyoendelea kupigana, Daudi akazidi kutenda kwa hekima kuliko maafisa wengine wa Sauli, nalo jina lake likajulikana sana.
Filiştinaaşde g'oşunbışde ç'ak'ınbışe dəv'ə ç'əvcab haa'a vuxha deş. Manbışe dəv'ə hav'uylette, Davud mane dəv'əbışee, Şaulne gırgıne hiqiy-allane insanaaşile ək'elika ıxha. Mançile qiyğa milletın mang'un do axtıda aqqaqqa.

< 1 Samweli 18 >