< 1 Samweli 18 >
1 Baada ya Daudi kumaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ikaambatana na roho ya Daudi, naye akampenda kama nafsi yake mwenyewe.
И кад сврши разговор са Саулом, душа Јонатанова приону за душу Давидову, и Јонатан га запази као своју душу.
2 Kuanzia siku ile Sauli akamchukua Daudi naye hakumruhusu kurudi nyumbani kwa baba yake.
И узе га Саул тај дан, и не даде му да се врати кући оца свог.
3 Yonathani akafanya agano na Daudi kwa sababu alimpenda kama nafsi yake mwenyewe.
И Јонатан учини веру с Давидом, јер га љубљаше као своју душу.
4 Yonathani akavua joho alilokuwa amevaa na kumpa Daudi, pamoja na koti lake, silaha zake, hata pamoja na upanga wake, upinde wake na mshipi wake.
И скиде Јонатан са себе плашт, који ношаше, и даде га Давиду, и одело своје и мач свој и лук свој и појас свој.
5 Lolote Sauli alilomtuma Daudi kufanya, alitenda kwa hekima, hata Sauli akampa cheo cha juu katika jeshi. Jambo hili likawapendeza watu wote, hata maafisa wa Sauli pia.
И иђаше Давид на шта га год Саул пошиљаше, и беше срећан, и постави га Саул над војницима, и омиле свему народу, па и слугама Сауловим.
6 Watu walipokuwa wanarudi nyumbani baada ya Daudi kumuua yule Mfilisti, wanawake wakaja kutoka pande zote za miji ya Israeli kumlaki Mfalme Sauli kwa kuimba na kucheza, kwa nyimbo za furaha na kwa matari na zeze.
А кад се враћаху, и кад се Давид враћаше убивши Филистејина, излазише жене из сваког града Израиљевог певајући и играјући на сусрет цару Саулу, с бубњевима и с весељем и гуслама.
7 Walipokuwa wanacheza, wakaimba: “Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake.”
И отпевајући жене једне другима уза свирке говораху: Саул згуби своју хиљаду, али Давид својих десет хиљада.
8 Sauli akakasirika sana; sehemu hii ya kurudia rudia ya wimbo huu ilimkasirisha sana. Akafikiri kuwa, “Wamempa Daudi makumi elfu, lakini mimi wamenipa elfu tu. Apate nini zaidi isipokuwa ufalme?”
И разгневи се Саул врло, и не бише му по вољи те речи, и рече: Давиду дадоше десет хиљада, а мени дадоше хиљаду; још му само царство треба.
9 Kuanzia wakati ule na kuendelea Sauli akawa na jicho la wivu juu ya Daudi.
И од тог дана Саул гледаше попреко Давида.
10 Kesho yake roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Mungu ikaja kwa nguvu juu ya Sauli. Alikuwa akitabiri nyumbani mwake, wakati Daudi alikuwa akipiga kinubi, kama alivyozoea. Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake;
А сутрадан нападе Саула зли дух Божји, те пророковаше у кући, а Давид му удараше руком својом у гусле као пре: а Саулу у руци беше копље.
11 akautupa kwa nguvu, akijiambia mwenyewe, “Nitamchoma kwa mkuki abaki hapo ukutani.” Lakini Daudi akamkwepa mara mbili.
И Саул баци копље говорећи: Да прикујем Давида за зид. Али му се Давид измаче два пута.
12 Sauli akamwogopa Daudi, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Daudi, lakini alikuwa amemwacha yeye.
И Саула беше страх од Давида, јер Господ беше с њим, а од Саула беше одступио.
13 Kwa hiyo Sauli akamwondoa Daudi mbele yake na kumpa kuwa kiongozi wa watu elfu moja, naye Daudi akatoka na kuingia akiongoza vikosi katika vita.
Зато га уклони Саул од себе, и постави га хиљадником; и он одлажаше и долажаше пред народом.
14 Katika kila kitu alichofanya, Daudi alipata mafanikio makubwa, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja naye.
И Давид беше срећан у свему што чињаше, јер Господ беше с њим.
15 Sauli alipoona jinsi alivyokuwa akifanikiwa, akamwogopa.
А Саул видећи да је веома срећан, бојаше га се.
16 Lakini Israeli wote na Yuda walimpenda Daudi, kwa sababu ndiye alikuwa akiwaongoza katika vita vyao.
А сав Израиљ и Јуда љубљаше Давида, јер он одлажаше и долажаше пред њима.
17 Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupa umwoe, endapo tu utanitumikia kwa ushujaa na kupigana vita vya Bwana.” Kwa maana Sauli alisema moyoni mwake, “Sitainua mkono wangu dhidi yake. Acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
И рече Саул Давиду: Ево, кћер своју старију Мераву даћу ти за жену, само ми буди храбар и води ратове Господње. Јер Саул говораше: Нећу да се дигне моја рука на њ, него филистејска рука нека се дигне на њ.
18 Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, nayo jamaa yangu ni nini au ukoo wa baba yangu katika Israeli, kwamba mimi niwe mkwewe mfalme?”
А Давид рече Саулу: Ко сам ја и какав је живот мој или дом оца мог у Израиљу, да будем зет царев?
19 Basi ulipofika wakati wa Daudi kupewa Merabu, binti Sauli, huyo binti aliozwa kwa Adrieli, Mmeholathi.
А кад дође време да Мераву, кћер Саулову, даду Давиду, дадоше је Адрилу Меолаћанину за жену.
20 Basi Mikali binti Sauli alimpenda Daudi, nao walipomwambia Sauli juu ya jambo hili, likampendeza.
Али Давида љубљаше Михала, кћи Саулова; а кад то јавише Саулу, би му по вољи.
21 Sauli akawaza, “Nitampa Daudi binti yangu, ili apate kuwa mtego kwake, ili kwamba mkono wa Wafilisti upate kuwa juu yake.” Hivyo Sauli akamwambia Daudi, “Sasa unayo nafasi ya pili ya kuwa mkwe wangu.”
И рече Саул: Даћу му је да му буде замка и да се диже на њ рука филистејска. А Давиду рече Саул: Бићеш ми данас зет с другом.
22 Ndipo Sauli akawaagiza watumishi wake, akisema, “Zungumzeni na Daudi kwa siri na kumwambia, ‘Tazama, mfalme amependezwa nawe, nao watumishi wake wote wanakupenda. Basi na uwe mkwewe mfalme.’”
И заповеди Саул слугама својим: Реците Давиду тајно и говорите: Гле, омилео си цару, и све слуге његове љубе те; буди сада зет царев.
23 Watumishi wa Sauli wakarudia hayo maneno kwa Daudi. Lakini Daudi akasema, “Je, mnafikiri ni jambo dogo kuwa mkwewe mfalme? Mimi ni mtu maskini tu, na nisiyejulikana sana.”
И слуге Саулове рекоше те речи Давиду, а Давид рече: Мислите ли да је лако бити зет царев? Та ја сам сиромах и мали човек.
24 Watumishi wa Sauli walipomweleza yale Daudi aliyoyasema,
И Саулу јавише ово слуге његове говорећи: Овако рече Давид.
25 Sauli akajibu, “Mwambieni Daudi, ‘Mfalme hataki zawadi nyingine kuwa mahari isipokuwa magovi 100 ya Wafilisti, ili kulipiza kisasi juu ya adui zake.’” Mawazo ya Sauli yalikuwa Daudi akaanguke mikononi mwa Wafilisti.
А Саул рече: Овако реците Давиду: Не тражи цар уздарја, него сто окрајака филистејских, да се цар освети својим непријатељима. А Саул мишљаше како би Давид пао у руке Филистејима.
26 Watumishi walipomwambia Daudi mambo haya, ikampendeza kuwa mkwewe mfalme. Basi kabla siku iliyopangwa haijafika,
И слуге његове казаше Давиду те речи, и Давиду би по вољи да постане царев зет. И време се још не наврши.
27 Daudi na watu wake walitoka na kuwaua Wafilisti mia mbili. Akayaleta magovi yao na kupeleka hesabu kamilifu kwa mfalme, ili kwamba apate kuwa mkwewe mfalme. Ndipo Sauli akamwoza Daudi Mikali binti yake.
А Давид уста и отиде са својим људима, и поби двеста Филистеја. И донесе Давид окрајке њихове, и дадоше их на број цару да би постао царев зет. И Саул му даде за жену Михалу кћер своју.
28 Sauli alipotambua kuwa Bwana alikuwa pamoja na Daudi na kwamba Mikali binti yake anampenda Daudi,
И Саул виде и позна да је Господ са Давидом; и Михала кћи Саулова љубљаше га.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi, naye Sauli akabaki kuwa adui yake siku zote za maisha yake.
А Саул се још већма побоја Давида; и беше Саул једнако непријатељ Давиду.
30 Majemadari wa jeshi la Wafilisti waliendelea kupigana vita na kadiri walivyoendelea kupigana, Daudi akazidi kutenda kwa hekima kuliko maafisa wengine wa Sauli, nalo jina lake likajulikana sana.
А кнезови филистејски удараху; и кад год удараху, Давид беше срећнији од свих слуга Саулових, и име се његово врло прослави.