< 1 Samweli 18 >
1 Baada ya Daudi kumaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ikaambatana na roho ya Daudi, naye akampenda kama nafsi yake mwenyewe.
And it came to pass, when he had made an end of speaking unto Saul, that, the soul of Jonathan, was knit with, the soul of David, so that Jonathan loved him, as his own soul.
2 Kuanzia siku ile Sauli akamchukua Daudi naye hakumruhusu kurudi nyumbani kwa baba yake.
And Saul took him, that day, —and suffered him not to return unto the house of his father.
3 Yonathani akafanya agano na Daudi kwa sababu alimpenda kama nafsi yake mwenyewe.
And Jonathan and David solemnised a covenant, —because he loved him as his own soul.
4 Yonathani akavua joho alilokuwa amevaa na kumpa Daudi, pamoja na koti lake, silaha zake, hata pamoja na upanga wake, upinde wake na mshipi wake.
And Jonathan stripped himself of the robe which was upon him, and gave it to David, —and his equipments, even to his sword, and to his bow, and to his girdle.
5 Lolote Sauli alilomtuma Daudi kufanya, alitenda kwa hekima, hata Sauli akampa cheo cha juu katika jeshi. Jambo hili likawapendeza watu wote, hata maafisa wa Sauli pia.
And David went forth—whithersoever Saul sent him, he behaved himself prudently, so Saul set him over the men of war, —and he became a favourite in the eyes of all the people, yea even in the eyes of the servants of Saul.
6 Watu walipokuwa wanarudi nyumbani baada ya Daudi kumuua yule Mfilisti, wanawake wakaja kutoka pande zote za miji ya Israeli kumlaki Mfalme Sauli kwa kuimba na kucheza, kwa nyimbo za furaha na kwa matari na zeze.
But so it was, when they came in on the return of David from the smiting of the Philistine, that the women went forth out of all the cities of Israel, singing and dancing, to meet Saul the king, —with timbrels, with rejoicing, and with instruments of three strings.
7 Walipokuwa wanacheza, wakaimba: “Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake.”
And the women that made merry responded to each other in song, and said, —Saul, hath smitten, his thousands, but, David, his, tens of thousands.
8 Sauli akakasirika sana; sehemu hii ya kurudia rudia ya wimbo huu ilimkasirisha sana. Akafikiri kuwa, “Wamempa Daudi makumi elfu, lakini mimi wamenipa elfu tu. Apate nini zaidi isipokuwa ufalme?”
Then was Saul exceeding angry, and this saying was offensive in his eyes, and he said, —They have ascribed, to David, ten thousands, but, to me, have they ascribed thousands, —What, more, then, can he have but, the kingdom?
9 Kuanzia wakati ule na kuendelea Sauli akawa na jicho la wivu juu ya Daudi.
And Saul was eyeing David from that day forward.
10 Kesho yake roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Mungu ikaja kwa nguvu juu ya Sauli. Alikuwa akitabiri nyumbani mwake, wakati Daudi alikuwa akipiga kinubi, kama alivyozoea. Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake;
And, when it came to pass, on the morrow, that a superhuman spirit of sadness came suddenly upon Saul, and he was moved to raving in the midst of the house, —and, David, began playing with his hand, as he had done day by day, that a spear being in Saul’s hand,
11 akautupa kwa nguvu, akijiambia mwenyewe, “Nitamchoma kwa mkuki abaki hapo ukutani.” Lakini Daudi akamkwepa mara mbili.
Saul hurled the spear, and said to himself—I will smite David, even to the wall! But David moved round from before him, twice.
12 Sauli akamwogopa Daudi, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Daudi, lakini alikuwa amemwacha yeye.
And Saul feared because of David, —for Yahweh was with him, whereas, from Saul, he had departed.
13 Kwa hiyo Sauli akamwondoa Daudi mbele yake na kumpa kuwa kiongozi wa watu elfu moja, naye Daudi akatoka na kuingia akiongoza vikosi katika vita.
So Saul removed him from him, and appointed him to be for him the captain of a thousand, —and he went out and came in before the people.
14 Katika kila kitu alichofanya, Daudi alipata mafanikio makubwa, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja naye.
And it came to pass that David, in all his ways, acted prudently, —and, Yahweh, was with him.
15 Sauli alipoona jinsi alivyokuwa akifanikiwa, akamwogopa.
And, when Saul saw that, he, was acting very prudently, he was afraid of him.
16 Lakini Israeli wote na Yuda walimpenda Daudi, kwa sababu ndiye alikuwa akiwaongoza katika vita vyao.
But, all Israel and Judah, were in love with David, —for he was going out and coming in before them.
17 Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupa umwoe, endapo tu utanitumikia kwa ushujaa na kupigana vita vya Bwana.” Kwa maana Sauli alisema moyoni mwake, “Sitainua mkono wangu dhidi yake. Acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
So then Saul said unto David—Lo! my elder daughter Merab, her, will I give thee to wife, only, approve thyself unto me as a son of valour and fight the battles of Yahweh. Saul, however, had said to himself—Let not, my own hand, be upon him, but let, the hand of the Philistines, be upon him.
18 Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, nayo jamaa yangu ni nini au ukoo wa baba yangu katika Israeli, kwamba mimi niwe mkwewe mfalme?”
And David said unto Saul—Who am, I, or who are my kinsfolk, the family of my father, in Israel, —that I should become son-in-law, to the king?
19 Basi ulipofika wakati wa Daudi kupewa Merabu, binti Sauli, huyo binti aliozwa kwa Adrieli, Mmeholathi.
But it came to pass, within the time for giving Merab daughter of Saul to David, that, she, was given to Adriel the Meholathite, to wife.
20 Basi Mikali binti Sauli alimpenda Daudi, nao walipomwambia Sauli juu ya jambo hili, likampendeza.
Then did Michal, Saul’s daughter, love David, —and it was told Saul, and the thing was right in his eyes.
21 Sauli akawaza, “Nitampa Daudi binti yangu, ili apate kuwa mtego kwake, ili kwamba mkono wa Wafilisti upate kuwa juu yake.” Hivyo Sauli akamwambia Daudi, “Sasa unayo nafasi ya pili ya kuwa mkwe wangu.”
And Saul said to himself—I will give her unto him, that she may prove to him a snare, and that, the hand of the Philistines, may be upon him. So then Saul said unto David, A second time, mayest thou become my son-in-law to-day.
22 Ndipo Sauli akawaagiza watumishi wake, akisema, “Zungumzeni na Daudi kwa siri na kumwambia, ‘Tazama, mfalme amependezwa nawe, nao watumishi wake wote wanakupenda. Basi na uwe mkwewe mfalme.’”
And Saul commanded his servants—Speak ye unto David quietly saying, Lo! the king delighteth in thee, and, all his servants, love thee, —now, therefore, become thou son-in-law to the king.
23 Watumishi wa Sauli wakarudia hayo maneno kwa Daudi. Lakini Daudi akasema, “Je, mnafikiri ni jambo dogo kuwa mkwewe mfalme? Mimi ni mtu maskini tu, na nisiyejulikana sana.”
And the servants of Saul spake, in the ears of David, these words. And David said—Seemeth it a light thing, in your eyes, to become son-in-law to the king, seeing that, I, am a poor man and lightly esteemed?
24 Watumishi wa Sauli walipomweleza yale Daudi aliyoyasema,
So the servants of Saul told him, saying, —According to these words, spake David,
25 Sauli akajibu, “Mwambieni Daudi, ‘Mfalme hataki zawadi nyingine kuwa mahari isipokuwa magovi 100 ya Wafilisti, ili kulipiza kisasi juu ya adui zake.’” Mawazo ya Sauli yalikuwa Daudi akaanguke mikononi mwa Wafilisti.
Then said Saul—Thus, shall ye say unto David—The king hath no delight in purchase-price, but rather in a hundred foreskins of Philistines, by avenging himself on the enemies of the king. But, Saul, thought to let David fall by the hand of the Philistines.
26 Watumishi walipomwambia Daudi mambo haya, ikampendeza kuwa mkwewe mfalme. Basi kabla siku iliyopangwa haijafika,
So, when his servants told David these words, the thing was right in the eyes of David, to become son-in-law unto the king, —and the days had not expired.
27 Daudi na watu wake walitoka na kuwaua Wafilisti mia mbili. Akayaleta magovi yao na kupeleka hesabu kamilifu kwa mfalme, ili kwamba apate kuwa mkwewe mfalme. Ndipo Sauli akamwoza Daudi Mikali binti yake.
Wherefore David arose, and went—he and his men, and smote among the Philistines two hundred men, and David brought in their foreskins, and gave them in full tale unto the king, that he might become son-in-law unto the king, and Saul gave him Michal his daughter, to wife.
28 Sauli alipotambua kuwa Bwana alikuwa pamoja na Daudi na kwamba Mikali binti yake anampenda Daudi,
And Saul saw and knew that, Yahweh, was with David, and that, all Israel, loved him.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi, naye Sauli akabaki kuwa adui yake siku zote za maisha yake.
So then Saul went on to fear because of David, yet more, —and it came to pass that Saul was hostile to David, all the days.
30 Majemadari wa jeshi la Wafilisti waliendelea kupigana vita na kadiri walivyoendelea kupigana, Daudi akazidi kutenda kwa hekima kuliko maafisa wengine wa Sauli, nalo jina lake likajulikana sana.
And, when the princes of the Philistines came forth, so it was, that, as often as they came forth, David was more circumspect than any of the servants of Saul, so that his name was, precious exceedingly.