< 1 Samweli 17 >

1 Wakati huu Wafilisti wakakusanya majeshi yao kwa ajili ya vita, nao wakakusanyika huko Soko katika Yuda. Wakapiga kambi huko Efes-Damimu, kati ya Soko na Azeka.
Les Philistins, ayant rassemblé leurs armées pour faire la guerre, se réunirent à Socho, qui appartient à Juda; ils campèrent entre Socho et Azéca, à Ephès-Dommim.
2 Sauli na Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi katika Bonde la Ela na kupanga jeshi ili kupigana vita na Wafilisti.
Saül et les hommes d'Israël se rassemblèrent aussi et campèrent dans la vallée de Térébinthe; ils se rangèrent en bataille en face des Philistins.
3 Wafilisti wakawa katika kilima kimoja na Waisraeli katika kilima kingine, hilo bonde likiwa kati yao.
Les Philistins étaient postés sur la montagne d'un côté, et Israël était posté sur la montagne de l'autre côté: la vallée était entre eux.
4 Shujaa aliyeitwa Goliathi, aliyetoka Gathi, akajitokeza kutoka kambi ya Wafilisti. Alikuwa na urefu dhiraa sita na shibiri moja.
Alors sortit des camps des Philistins un champion; il se nommait Goliath, il était de Geth, et sa taille était de six coudées et un palme.
5 Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya shaba kifuani mwake yenye uzito wa shekeli elfu tano.
Un casque d'airain couvrait sa tête, et il portait une cuirasse à écailles; et le poids de la cuirasse était de cinq mille sicles d'airain.
6 Miguuni mwake alivaa mabamba ya shaba, na alikuwa na mkuki wa shaba mgongoni mwake.
Il avait aux pieds une chaussure d'airain et un javelot d'airain entre ses épaules.
7 Mpini wa huo mkuki ulikuwa kama mti wa mfumaji, na ncha ya chuma yake ilikuwa na uzito wa shekeli mia sita. Mbeba ngao wake alitangulia mbele yake.
Le bois de sa lance était comme une ensouple de tisserand, et la pointe de sa lance pesait six cents sicles de fer; celui qui portait son bouclier marchait devant lui.
8 Goliathi alisimama na kuwapigia kelele majeshi ya Israeli, akisema, “Kwa nini mmetoka kupanga vita? Je, mimi si Mfilisti, na ninyi ni watumishi wa Sauli? Chagueni mtu na anishukie mimi.
Goliath s'arrêta et, s'adressant aux bataillons d'Israël, il leur cria: « Pourquoi êtes-vous sortis pour vous ranger en bataille? Ne suis-je pas le Philistin, et n'êtes-vous pas les esclaves de Saül? Choisissez un homme qui descende contre moi.
9 Kama anaweza kupigana nami na kuniua, tutakuwa chini yenu; lakini kama nikimshinda na kumuua, ninyi mtakuwa chini yetu na mtatutumikia.”
S'il l'emporte en se battant avec moi et qu'il me tue, nous vous serons assujettis; mais si je l'emporte sur lui et que je le tue, vous nous serez assujettis et vous nous servirez. »
10 Kisha yule Mfilisti akasema, “Siku hii ya leo nayatukana majeshi ya Israeli! Nipeni mtu tupigane.”
le Philistin ajouta: « Je jette aujourd'hui ce défi à l'armée d'Israël: Donnez-moi un homme, et nous nous battrons ensemble. »
11 Kwa kusikia maneno ya Wafilisti, Sauli na Waisraeli wote wakafadhaika na kuogopa.
En entendant ces paroles du Philistin, Saül et tout Israël furent effrayés et saisis d'une grande crainte.
12 Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefrathi jina lake Yese aliyekuwa ametoka Bethlehemu ya Yuda. Yese alikuwa na wana wanane, naye wakati wa Sauli alikuwa mzee tena wa umri mkubwa.
Or David était fils de cet Ephratéen de Bethléem de Juda nommé Isaï, qui avait huit fils; cet homme, au temps de Saül, était vieux, avancé en âge.
13 Wana wakubwa watatu wa Yese walikuwa wamefuatana na Sauli vitani: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Eliabu, wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama.
Les trois fils aînés d'Isaï étaient allés suivre Saül à la guerre; et les noms de ces trois fils qui étaient allés à la guerre étaient Eliab l'aîné, Abinadab le second, et Samma le troisième.
14 Daudi ndiye alikuwa mdogo wa wote. Hao wakubwa watatu wakamfuata Sauli,
David était le plus jeune. Les trois aînés suivaient Saül,
15 lakini Daudi alikuwa akienda kwa Sauli na kurudi ili kuchunga kondoo wa baba yake huko Bethlehemu.
et David allait et venait d'auprès de Saül, pour paître les brebis de son père à Bethléem.
16 Kwa siku arobaini huyo Mfilisti alikuwa akija mbele kila siku asubuhi na jioni na kujionyesha.
Le Philistin s'avançait matin et soir, et il se présenta pendant quarante jours.
17 Wakati huo Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Chukua hii efa ya bisi na hii mikate kumi kwa ajili ya ndugu zako uwapelekee upesi kambini mwao.
Isaï dit à David, son fils: « Prends pour tes frères cet épha de grain rôti et ces dix pains, et cours au camp vers tes frères.
18 Chukua pamoja na hizi jibini kumi kwa jemadari wa kikosi chao. Ujue hali ya ndugu zako na uniletee taarifa za uhakika kutoka kwao.
Et ces dix fromages, porte-les au chef de leur millier. Tu visiteras tes frères pour voir s'ils se portent bien, et tu prendras d'eux un gage.
19 Wao wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli huko kwenye Bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti.”
Saül et eux, et tous les hommes d'Israël, sont dans la vallée de Térébinthe, faisant la guerre aux Philistins. »
20 Asubuhi na mapema Daudi akaondoka, akaliacha kundi la kondoo pamoja na mchungaji, akapakia vitu vile na kuondoka, kama vile Yese alivyokuwa amemwagiza. Akafika kambini wakati jeshi lilikuwa likitoka kwenda kwenye sehemu yake ya kupigania, huku wakipiga kelele za vita.
David se leva de bon matin et, laissant les brebis à un gardien, il prit les provisions et partit, comme Isaï le lui avait commandé. Quand il arriva au campement, l'armée sortait du camp pour se ranger en bataille et on poussait des cris de guerre.
21 Israeli na Wafilisti walikuwa wakipanga safu zao wakitazamana.
Israélites et Philistins se rangèrent en ligne, troupe contre troupe.
22 Daudi akaacha vile vitu vyake kwa mtunza vifaa, akakimbilia katika safu za vita na kuwasalimu ndugu zake.
David déposa ses bagages entre les mains du gardien des bagages, et courut vers la troupe. Aussitôt arrivé, il demanda à ses frères comment ils se portaient.
23 Alipokuwa akisema nao, Goliathi, yule Mfilisti shujaa kutoka Gathi, akajitokeza mbele ya safu zake na kupiga ile kelele yake ya kawaida ya matukano, naye Daudi akayasikia.
Pendant qu'il s'entretenait avec eux, voici que le champion, — il se nommait Goliath, le Philistin de Geth, — s'avança hors des rangs des Philistins, tenant les mêmes discours et David l'entendit.
24 Waisraeli walipomwona yule mtu, wote wakamkimbia kwa woga mkuu.
En voyant cet homme, tous ceux d'Israël se retirèrent devant lui, saisis d'une grande crainte.
25 Basi Waisraeli walikuwa wakisema, “Je, mnaona jinsi mtu huyu anavyoendelea kujitokeza. Hujitokeza ili kutukana Israeli. Mfalme atatoa utajiri mwingi kwa yule mtu atakayemuua. Pia atamwoza binti yake na atasamehe jamaa ya baba yake kulipa kodi katika Israeli.”
Un Israélite dit: « Voyez-vous cet homme qui s'avance? C'est pour défier Israël qu'il s'avance. Celui qui le tuera, le roi le comblera de grandes richesses, il lui donnera sa fille et il affranchira de toute charge la maison de son père en Israël. »
26 Daudi akauliza watu waliokuwa wamesimama karibu naye, “Je, atafanyiwa nini mtu atakayemuua huyu Mfilisti na kuondoa aibu hii katika Israeli? Ni nani huyu Mfilisti asiyetahiriwa hata atukane majeshi ya Mungu aliye hai?”
David dit aux hommes qui se tenaient près de lui: « Que fera-t-on à celui qui tuera ce Philistin et qui ôtera l'opprobre de dessus Israël? Qui est donc ce Philistin, cet incirconcis, pour insulter les troupes du Dieu vivant? »
27 Wakarudia yale yaliyokuwa yamesemwa na kumwambia kuwa, “Hili ndilo atakalotendewa mtu yule atakayemuua.”
Le peuple lui répéta les mêmes paroles, en disant: « Voilà ce qu'on fera à celui qui le tuera. »
28 Eliabu nduguye mkubwa Daudi alipomsikia akizungumza na watu hasira ikawaka juu yake akamuuliza, “Kwa nini umeteremka kuja hapa? Nao wale kondoo wachache kule nyikani umewaacha na nani? Ninajua jinsi ulivyo na kiburi na jinsi moyo wako ulivyo mwovu; umekuja hapa kutazama vita tu.”
Eliab, son frère aîné, l'entendit parler aux hommes, et la colère d'Eliab s'enflamma contre David, et il dit: « Pourquoi es-tu descendu, et à qui as-tu laissé ce petit nombre de brebis dans le désert? Je connais ton orgueil et la malice de ton cœur; c'est pour voir la bataille que tu es descendu. »
29 Daudi akasema, “Sasa nimefanya nini? Je, siwezi hata kuongea.”
David répondit: « Qu'ai-je fait maintenant? N'est-ce pas une simple parole? »
30 Daudi akamgeukia mtu mwingine na kumuuliza jambo lilo hilo, nao watu wakamjibu vilevile kama mwanzo.
Et, se détournant de lui pour s'adresser à un autre, il tint le même langage; et le peuple lui répondit comme la première fois.
31 Lile Daudi alilosema likasikiwa na kuelezwa kwa Sauli, naye Sauli akatuma aitwe.
Lorsqu'on eut entendu les paroles prononcées par David, on les rapporta à Saül, qui le fit venir.
32 Daudi akamwambia Sauli, “Mtu yeyote asife moyo kwa habari ya huyu Mfilisti; mtumishi wako atakwenda kupigana naye.”
David dit à Saül: « Que le cœur ne défaille à personne! Ton serviteur ira combattre contre ce Philistin. »
33 Sauli akamjibu Daudi, “Wewe hutaweza kwenda kupigana dhidi ya huyu Mfilisti; wewe ni kijana tu, naye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
Saül dit à David: « Tu ne peux aller contre ce Philistin pour combattre avec lui, car tu es un enfant, et il est un homme de guerre depuis sa jeunesse. »
34 Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako amekuwa akichunga kondoo wa baba yake. Wakati simba au dubu alikuja na kuchukua kondoo kutoka kundi,
David dit à Saül: « Lorsque ton serviteur faisait paître les brebis de son père, et qu'un lion ou un ours venait et enlevait une brebis du troupeau,
35 nilifuatia, nikampiga na nikampokonya kondoo kwenye kinywa chake. Aliponigeukia, nilimkamata nywele zake, nikampiga na kumuua.
je me mettais à sa poursuite, je le frappais et j'arrachais la brebis de sa gueule; s'il se dressait contre moi, je le saisissais à la mâchoire, je le frappais et je le tuais.
36 Mtumishi wako ameshaua simba na dubu pia; huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa sababu ameyatukana majeshi ya Mungu aliye hai.
Ton serviteur a tué le lion comme l'ours, et il en sera du Philistin, de cet incirconcis, comme de l'un d'eux, car il a insulté les troupes du Dieu vivant. »
37 Bwana ambaye aliniokoa toka katika makucha ya simba na makucha ya dubu ataniokoa kutoka mikono ya huyu Mfilisti.” Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, naye Bwana na awe pamoja nawe.”
David ajouta: « Yahweh qui m'a délivré du lion et de l'ours, me délivrera aussi de la main de ce Philistin. » Et Saül dit à David: « Va, et que Yahweh soit avec toi! »
38 Ndipo Sauli akamvika Daudi silaha zake mwenyewe za vita. Akamvika dirii na chapeo ya shaba kichwani mwake.
Saül fit revêtir David de ses habits, mit sur sa tête un casque d'airain et l'endossa d'une cuirasse;
39 Daudi akajifunga upanga juu ya hayo mavazi na kujaribu kutembea kwa sababu alikuwa hana uzoefu navyo. Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda nikiwa nimevaa hivi, kwa sababu sina uzoefu navyo.” Hivyo akavivua.
puis David ceignit l'épée de Saül par-dessus son armure, et il essaya de marcher, car il n'avait jamais essayé d'armure. David dit à Saül: « Je ne puis marcher avec ces armes, je n'y suis point accoutumé. » Et, s'en étant débarrassé,
40 Kisha akachukua fimbo yake mkononi, akachagua mawe laini matano kutoka kwenye kijito, akayaweka kwenye kifuko ndani ya mfuko wake wa kichungaji, akiwa na kombeo yake mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.
David prit en main son bâton, choisit dans le torrent cinq cailloux polis et les mit dans son sac de berger, dans sa gibecière. Puis, sa fronde à la main, il s'avança vers le Philistin.
41 Wakati ule ule, yule Mfilisti, akiwa na mbeba ngao wake mbele yake, akaendelea kujongea karibu na Daudi.
Le Philistin s'approcha peu à peu de David, précédé de l'homme qui portait le bouclier.
42 Mfilisti akamwangalia Daudi kote na kumwona kuwa ni kijana tu, mwekundu na mzuri wa kupendeza, naye akamdharau.
Le Philistin regarda, vit David et le méprisa, car il était très jeune, blond et beau de visage.
43 Akamwambia Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata unanijia na fimbo?” Yule Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
Le Philistin dit à David: « Suis-je un chien, que tu viennes à moi avec un bâton? » Et le Philistin maudit David par ses dieux.
44 Tena Mfilisti akamwambia, “Njoo hapa, nami nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni nyama yako.”
Et le Philistin dit à David: « Viens à moi, que je donne ta chair aux oiseaux du ciel et aux bêtes des champs. »
45 Daudi akamwambia yule Mfilisti. “Wewe unanijia na upanga, mkuki na fumo, lakini mimi ninakujia kwa jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa majeshi ya Israeli, ambaye wewe umemtukana.
David répondit au Philistin: « Tu viens à moi avec l'épée, la lance et le javelot; et moi je viens à toi au nom de Yahweh des armées, du Dieu des bataillons d'Israël, que tu as insulté.
46 Siku hii leo Bwana atakutia mkononi mwangu, nami nitakupiga na kukukata kichwa chako. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya jeshi la Wafilisti, nayo dunia yote itajua kuwa yuko Mungu katika Israeli.
Aujourd'hui Yahweh te livrera entre mes mains, je te frapperai et j'enlèverai ta tête de dessus toi; aujourd'hui je donnerai les cadavres de l'armée des Philistins aux oiseaux du ciel et aux animaux de la terre; et toute la terre saura qu'Israël a un Dieu;
47 Wale wote waliokusanyika hapa watajua kuwa Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; kwa kuwa vita ni vya Bwana, naye atawatia wote mikononi mwetu.”
et toute cette multitude saura que ce n'est ni par l'épée ou par la lance que Yahweh sauve, car à Yahweh appartient la guerre, et il vous a livrés entre nos mains. »
48 Yule Mfilisti aliposogea karibu ili kumshambulia, Daudi akaenda mbio kuelekea safu ya vita kukutana naye.
Le Philistin, s'étant levé, se mit en marche et s'avança au-devant de David, et David se hâta de courir, vers le front de la troupe, à la rencontre du Philistin.
49 Daudi akatia mkono wake mfukoni na kuchukua jiwe, akalirusha kwa kombeo, nalo likampiga yule Mfilisti kwenye paji la uso. Lile jiwe likaingia kipajini mwa uso, akaanguka chini kifudifudi.
David mit la main dans sa gibecière, en retira une pierre et la lança avec sa fronde; il frappa le Philistin au front, et la pierre s'enfonça dans son front, et il tomba le visage contre terre.
50 Basi Daudi akamshinda huyo Mfilisti kwa kombeo na jiwe; bila kuwa na upanga mikononi mwake akampiga huyo Mfilisti na kumuua.
Ainsi David, avec une fronde et une pierre, fut plus fort que le Philistin, il frappa à mort le Philistin. Et il n'y avait pas d'épée dans la main de David.
51 Daudi akakimbia na kusimama juu yake. Akaushika upanga wa huyo Mfilisti na kuuvuta toka kwenye ala yake. Baada ya kumuua, akakata kichwa chake kwa ule upanga. Wafilisti walipoona kuwa shujaa wao amekufa, wakageuka na kukimbia.
David courut, s'arrêta près du Philistin et, s'étant saisi de son épée qu'il tira du fourreau, il le tua et lui coupa la tête avec elle.
52 Ndipo watu wa Israeli na Yuda wakainuka kwenda mbele wakipiga kelele na kufuatia Wafilisti mpaka kwenye ingilio la Gathi kwenye malango ya Ekroni. Maiti zao zilitawanyika kando ya barabara ya Shaaraimu hadi Gathi na Ekroni.
Voyant leur héros mort, les Philistins prirent la fuite. Et les hommes d'Israël et de Juda se levèrent, en poussant des cris, et poursuivirent les Philistins jusqu'à l'entrée de Geth et jusqu'aux portes d'Accaron. Les cadavres des Philistins jonchèrent le chemin de Saraïm jusqu'à Geth et jusqu'à Accaron.
53 Waisraeli waliporudi kutoka kuwafukuza Wafilisti, waliteka nyara kutoka kambi yao.
A leur retour de la poursuite des Philistins, les enfants d'Israël pillèrent leur camp.
54 Daudi akachukua kichwa cha yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu, naye akaweka silaha za huyo Mfilisti katika hema lake mwenyewe.
David prit la tête du Philistin et la fit porter à Jérusalem, et il mit dans sa tente les armes du Philistin.
55 Sauli alipomwona Daudi anakwenda kukabiliana na huyo Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, “Abneri, yule kijana ni mwana wa nani?” Abneri akajibu, “Hakika kama uishivyo, ee mfalme, mimi sifahamu.”
Lorsque Saül eut vu David s'avancer à la rencontre du Philistin, il dit à Abner, chef de l'armée: « De qui ce jeune homme est-il fils, Abner? » Abner répondit: « Aussi vrai que ton âme est vivante, ô roi, je l'ignore. »
56 Mfalme akasema, “Uliza huyu kijana ni mwana wa nani.”
Le roi lui dit: « Informe-toi donc de qui est fils ce jeune homme. »
57 Mara Daudi aliporudi kutoka kumuua huyo Mfilisti, Abneri akamchukua na kumleta mbele ya Sauli. Daudi alikuwa bado anakishikilia kichwa cha yule Mfilisti.
Quand David fut de retour après avoir tué le Philistin, Abner le prit et le mena devant Saül; David avait à la main la tête du Philistin.
58 Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mwana wa nani?” Daudi akasema, “Mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese wa Bethlehemu.”
Saül lui dit: « De qui es-tu fils, jeune homme. » Et David répondit: « Je suis fils de ton serviteur, Isaï de Bethléem. »

< 1 Samweli 17 >