< 1 Samweli 15 >

1 Samweli akamwambia Sauli, “Mimi ndiye ambaye Bwana alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Israeli, basi sasa sikiliza ujumbe kutoka kwa Bwana.
Afterward Samuel said vnto Saul, The Lord sent me to anoint thee King ouer his people, ouer Israel: nowe therefore obey the voyce of the wordes of the Lord.
2 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa kile walichowatendea Israeli walipowavizia wakati walipanda kutoka Misri.
Thus saith the Lord of hostes, I remember what Amalek did to Israel, howe they laide waite for the in ye way, as they came vp from Egypt.
3 Basi sasa nenda ukawashambulie Waamaleki na kuwaangamiza kabisa pamoja na kila kitu kilicho mali yao. Usiwahurumie; waue wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, ngʼombe na kondoo, ngamia na punda.’”
Nowe therefore goe, and sinite Amalek, and destroy ye all that perteyneth vnto them, and haue no compassion on them, but slay both man and woman, both infant and suckling, both oxe, and sheepe, both camell, and asse.
4 Ndipo Sauli akawaita watu na kuwapanga huko Telaimu, askari wa miguu 200,000 pamoja na watu 10,000 kutoka Yuda.
And Saul assembled ye people, and nombred them in Telaim, two hundreth thousande footemen, and ten thousand men of Iudah.
5 Sauli akaenda katika mji wa Amaleki na kuwavizia bondeni.
And Saul came to a citie of Amalek, and set watch at the riuer.
6 Kisha akawaambia Wakeni, “Ondokeni, waacheni Waamaleki ili nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao, kwa kuwa ninyi mliwatendea mema Waisraeli wote wakati walipanda kutoka Misri.” Basi Wakeni wakaondoka, wakawaacha Waamaleki.
And Saul said vnto the Kenites, Goe, depart, and get you downe from among the Amalekites, least I destroy you with them: for ye shewed mercie to all the children of Israel, when they came vp from Egypt: and the Kenites departed from among the Amalekites.
7 Ndipo Sauli akawashambulia Waamaleki toka Havila mpaka Shuri, hadi mashariki ya Misri.
So Saul smote the Amalekites from Hauilah as thou commest to Shur, that is before Egypt,
8 Akamchukua Agagi, mfalme wa Waamaleki akiwa hai, nao watu wake wote akawaangamiza kabisa kwa upanga.
And tooke Agag the King of the Amalekites aliue, and destroyed all the people with the edge of the sword.
9 Lakini Sauli na hilo jeshi wakamhifadhi hai Agagi na kondoo na ngʼombe walio wazuri, mafahali na wana-kondoo walionona kila kitu kilichokuwa kizuri. Hivi vitu hawakuwa radhi kuviangamiza kabisa, bali kila kitu kilichodharauliwa na kilicho dhaifu wakakiangamiza kabisa.
But Saul and the people spared Agag, and the better sheepe, and the oxen, and the fat beasts, and the lambes, and all that was good, and they would not destroy them: but euery thing that was vile and nought worth, that they destroyed.
10 Kisha neno la Bwana likamjia Samweli kusema:
Then came the worde of the Lord vnto Samuel, saying,
11 “Ninasikitika kwamba nimemfanya Sauli kuwa mfalme, kwa sababu ameacha kunifuata mimi na hakutimiza maagizo yangu.” Samweli akafadhaika, naye akamlilia Bwana usiku ule wote.
It repenteth me that I haue made Saul King: for he is turned from me, and hath not performed my commandements. And Samuel was mooued, and cryed vnto the Lord all night.
12 Asubuhi na mapema Samweli akaamka kwenda kukutana na Sauli, lakini akaambiwa, “Sauli amekwenda Karmeli. Huko amesimamisha mnara kwa heshima yake mwenyewe naye ameendelea na kuteremkia Gilgali.”
And when Samuel arose early to meete Saul in the morning, one tolde Samuel, saying, Saul is gone to Carmel: and beholde, he hath made him there a place, from whence he returned, and departed, and is gone downe to Gilgal.
13 Samweli alipomfikia, Sauli akamwambia, “Bwana akubariki! Nimetimiza yale Bwana aliniagiza.”
Then Samuel came to Saul, and Saul said vnto him. Blessed be thou of the Lord, I haue fulfilled the commandement of the Lord.
14 Lakini Samweli akasema, “Nini basi huu mlio wa kondoo masikioni mwangu? Huu mlio wa ngʼombe ninaousikia ni kitu gani?”
But Samuel saide, What meaneth then the bleating of the sheepe in mine eares, and the lowing of the oxen which I heare?
15 Sauli akajibu, “Askari wamewaleta kutoka kwa Waamaleki, waliwaacha wale kondoo na ngʼombe wazuri ili kuwatoa dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, lakini tuliwaangamiza kabisa wengine wote.”
And Saul answered, They haue brought them from the Amalekites: for the people spared the best of the sheepe, and of the oxen to sacrifice them vnto the Lord thy God, and the remnant haue we destroyed.
16 Samweli akamwambia Sauli, “Ngoja! Nami nitakuambia lile Bwana aliloniambia usiku huu.” Sauli akajibu, “Niambie.”
Againe Samuel saide to Saul, Let me tell thee what the Lord hath saide to me this night. And he said vnto him, Say on.
17 Samweli akamwambia, “Ingawa zamani ulijiona mdogo machoni pako mwenyewe, Je, hukuwa kiongozi wa kabila za Israeli? Bwana alikutia mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli.
Then Samuel saide, When thou wast litle in thine owne sight, wast thou not made the head of the tribes of Israel? for the Lord anointed thee King ouer Israel.
18 Naye akakutuma kwa kazi maalum, akisema, ‘Nenda ukaangamize kabisa wale watu waovu, wale Waamaleki, upigane nao vita mpaka utakapowaangamiza kabisa.’
And the Lord sent thee on a iourney, and saide, Goe, and destroy those sinners the Amalekites, and fight against them, vntill thou destroy them.
19 Kwa nini hukumtii Bwana? Kwa nini ulivamia nyara na kufanya uovu machoni pa Bwana?”
Nowe wherefore hast thou not obeyed the voyce of the Lord, but hast turned to the pray, and hast done wickedly in the sight of the Lord?
20 Sauli akasema, “Lakini nilimtii Bwana. Nilikamilisha ile kazi ambayo Bwana alinituma. Niliwaangamiza Waamaleki kabisa na kumleta Agagi mfalme wao.
And Saul saide vnto Samuel, Yea, I haue obeyed the voyce of the Lord, and haue gone the way which the Lord sent me, and haue brought Agag the King of Amalek, and haue destroyed the Amalekites.
21 Askari walichukua kondoo na ngʼombe kutoka kwenye nyara, zile ambazo ni nzuri sana zimewekwa wakfu kwa Mungu, ili zitolewe dhabihu kwa Bwana Mungu wako huko Gilgali.”
But the people tooke of the spoyle, sheepe, and oxen, and the chiefest of the things which shoulde haue bene destroyed, to offer vnto the Lord thy God in Gilgal.
22 Lakini Samweli akajibu: “Je, Bwana anafurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama vile kuitii sauti ya Bwana? Kutii ni bora zaidi kuliko dhabihu, nako kusikia ni bora kuliko mafuta ya kondoo dume.
And Samuel saide, Hath the Lord as great pleasure in burnt offerings and sacrifices, as when the voyce of the Lord is obeyed? beholde, to obey is better then sacrifice, and to hearken is better then the fatte of rammes.
23 Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uaguzi, nao ukaidi ni kama uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umelikataa neno la Bwana, naye amekukataa wewe kuendelea kuwa mfalme.”
For rebellion is as the sinne of withcraft, and transgression is wickednesse and idolatrie. Because thou hast cast away the worde of the Lord, therefore hee hath cast away thee from being King.
24 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi. Nimevunja amri ya Bwana na maagizo yako. Niliwaogopa watu na kwa hiyo nikafanya walivyotaka.
Then Saul sayde vnto Samuel, I haue sinned: for I haue transgressed the commandement of the Lord, and thy wordes, because I feared the people, and obeyed their voyce.
25 Sasa ninakusihi usamehe dhambi yangu, nawe urudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana.”
Nowe therefore I pray thee, take away my sinne, and turne againe with mee, that I may worship the Lord.
26 Lakini Samweli akamwambia, “Sitarudi pamoja nawe. Umelikataa neno la Bwana, naye Bwana amekukataa wewe, usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli!”
But Samuel saide vnto Saul, I will not returne with thee: for thou hast cast away the word of the Lord, and the Lord hath cast away thee, that thou shalt not be King ouer Israel.
27 Samweli alipogeuka ili aondoke, Sauli akangʼangʼania pindo la joho lake, nalo likararuka.
And as Samuel turned himselfe to goe away, he caught the lappe of his coate, and it rent.
28 Samweli akamwambia, “Bwana ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye ameutia kwa mmoja wa majirani zako, aliye bora kuliko wewe.
Then Samuel saide vnto him, The Lord hath rent the kingdome of Israel from thee this day, and hath giuen it to thy neighbour, that is better then thou.
29 Yeye aliye Utukufu wa Israeli hasemi uongo wala hana kigeugeu; kwa kuwa yeye si mwanadamu, hata abadili nia yake.”
For in deede the strength of Israel will not lye nor repent: for hee is not a man that hee should repent.
30 Sauli akajibu, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali niheshimu mbele ya wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli; rudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana Mungu wako.”
Then he saide, I haue sinned: but honour mee, I pray thee, before the Elders of my people, and before Israel, and turne againe with mee, that I may worship the Lord thy God.
31 Hivyo Samweli akarudi pamoja na Sauli, naye Sauli akamwabudu Bwana.
So Samuel turned againe, and followed Saul: and Saul worshipped the Lord.
32 Ndipo Samweli akasema, “Niletee Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akaja kwake kwa ujasiri, akifikiri, “Hakika uchungu wa mauti umepita.”
Then saide Samuel, Bring yee hither to me Agag ye King of the Amalekites: and Agag came vnto him pleasantly, and Agag saide, Truely the bitternesse of death is passed.
33 Lakini Samweli akasema, “Kama upanga wako ulivyofanya wanawake kufiwa na watoto wao, ndivyo mama yako atakavyokuwa hana mtoto miongoni mwa wanawake.” Naye Samweli akamuua Agagi mbele za Bwana huko Gilgali.
And Samuel sayde, As thy sworde hath made women childlesse, so shall thy mother bee childelesse among other women. And Samuel hewed Agag in pieces before the Lord in Gilgal.
34 Kisha Samweli akaenda Rama, lakini Sauli akapanda nyumbani kwake huko Gibea ya Sauli.
So Samuel departed to Ramah, and Saul went vp to his house to Gibeah of Saul.
35 Hadi siku Samweli alipofariki hakwenda kumwona Sauli tena, ingawa Samweli alimwombolezea. Naye Bwana alihuzunika kwamba alimfanya Sauli kuwa mfalme juu ya Israeli.
And Samuel came no more to see Saul vntill the day of his death: but Samuel mourned for Saul, and the Lord repented that hee made Saul King ouer Israel.

< 1 Samweli 15 >