< 1 Samweli 14 >

1 Siku moja Yonathani mwana wa Sauli akamwambia kijana mbeba silaha wake, akasema, “Njoo, tuwavukie Wafilisti kwenye doria upande ule mwingine.” Lakini hakumwambia baba yake.
Un jour, Jonathas, fils de Saül, dit au jeune homme qui portait ses armes: « Viens, et passons jusqu'au poste des Philistins, qui est là, de l'autre côté. » Et il n'en dit rien à son père.
2 Sauli alikuwa akikaa kwenye viunga vya Gibea chini ya mkomamanga huko Migroni. Alikuwa pamoja na watu kama 600,
— Saül se tenait à l'extrémité de Gabaa, sous le grenadier de Magron, et le peuple qui était avec lui était d'environ six cents hommes.
3 miongoni mwao alikuwepo Ahiya, ambaye alikuwa amevaa kisibau. Alikuwa mwana wa Ikabodi, nduguye Ahitubu mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo. Hakuna yeyote aliyekuwa na habari kwamba Yonathani alikuwa ameondoka.
Achias, fils d'Achitob, frère d'Ichabod, fils de Phinées, fils d'Héli, prêtre de Yahweh à Silo, portait l'éphod. Le peuple ne savait pas non plus que Jonathas s'en fût allé.
4 Kila upande wa njia ambayo Yonathani alikusudia kupita ili kuvuka kufikia doria ya Wafilisti kulikuwepo na jabali; moja lilikuwa linaitwa Bosesi, na jingine Sene.
Entre les passages par lesquels Jonathas cherchait à arriver au poste des Philistins, il y avait une dent de rocher d'un côté et une dent de rocher de l'autre côté, l'une nommée Bosès, et l'autre nommée Séné.
5 Jabali moja lilisimama kaskazini kuelekea Mikmashi na jingine upande wa kusini kuelekea Geba.
L'une de ces dents se dresse au nord, vis-à-vis de Machmas, et l'autre au midi, vis-à-vis de Gabée. —
6 Yonathani akamwambia kijana wake mbeba silaha, “Njoo, tuvukie doria ya wale jamaa wasiotahiriwa. Huenda Bwana atatenda kwa ajili yetu. Hakuna chochote kitakachoweza kumzuia Bwana kuokoa, kwamba ni kwa wingi au kwa uchache.”
Jonathas dit donc au jeune homme qui portait ses armes: « Viens, et passons jusqu'au poste de ces incirconcis. Peut-être Yahweh agira-t-il pour nous; car rien n'empêche Yahweh de sauver, soit par un nombre grand, soit par un petit nombre. »
7 Mbeba silaha wake akamwambia, “Fanya yale yote uliyo nayo katika moyo wako. Songa mbele; moyo wangu na roho yangu viko pamoja nawe.”
Son écuyer lui répondit: « Fais tout ce que tu as dans le cœur; va où tu voudras, me voici avec toi prêt à te suivre. »
8 Yonathani akasema, “Basi njoo; tutavuka kuwaelekea hao watu na kuacha watuone.
Jonathas dit: « Voici, nous passerons vers ces hommes et nous nous montrerons vers eux.
9 Kama wakituambia, ‘Subirini hapo mpaka tuje kwenu,’ tutakaa pale tulipo na hatutakwea kwao.
S'ils nous disent: Arrêtez, jusqu'à ce que nous venions à vous! nous resterons en place et nous ne monterons pas vers eux.
10 Lakini kama watasema, ‘Pandeni mje kwetu,’ tutakwea, kwa sababu hiyo itakuwa ishara yetu kwamba Bwana amewatia mikononi mwetu.”
Mais s'ils disent: Montez vers nous! nous monterons, car Yahweh les a livrés entre nos mains. Cela sera pour nous le signe. »
11 Basi wote wawili wakajionyesha kwa doria ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Tazama! Waebrania wanatambaa toka mashimoni walimokuwa wamejificha.”
Ils se montrèrent tous deux au poste des Philistins, et les Philistins dirent: « Voici les Hébreux qui sortent des trous où ils s'étaient cachés. »
12 Watu wa kwenye doria wakawapigia kelele Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njooni, pandeni kwetu nasi tutawakomesha.” Basi Yonathani akamwambia mbeba silaha wake, “Panda nyuma yangu; Bwana amewatia mikononi mwa Israeli.”
Et les hommes du poste, s'adressant à Jonathas et à son écuyer, dirent: « Montez vers nous, et nous vous ferons savoir quelque chose. » Et Jonathas dit à son écuyer: « Monte après moi, car Yahweh les a livrés entre nos mains. »
13 Yonathani akapanda juu, akitumia mikono yake na miguu, pamoja na mbeba silaha wake papo hapo nyuma yake. Wafilisti wakaanguka mbele ya Yonathani, naye mbeba silaha wake akamfuata akiwaua nyuma yake.
Et Jonathas monta, sur les mains et sur les pieds, suivi de son écuyer. Les Philistins tombaient devant Jonathas, et son écuyer tuait derrière lui.
14 Katika hilo shambulio la kwanza, Yonathani na mbeba silaha wake waliua kama watu ishirini kwenye eneo kama la nusu eka.
Ce premier massacre que firent Jonathas et son écuyer fut d'environ vingt hommes, sur la longueur d'un demi-sillon d'un arpent de terre.
15 Kisha fadhaa ikawapata jeshi lote, wale waliokuwa kambini na shambani, wale waliokuwa katika doria na makundi ya washambuliaji, nayo nchi ilitetemeka. Ilikuwa ni hofu ya ghafula iliyotumwa na Mungu.
L'épouvante se répandit dans le camp des Philistins, dans la campagne et dans tout le peuple; le poste aussi et l'armée de destruction furent saisis de peur; la terre trembla: c'était une terreur de Dieu.
16 Wapelelezi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona jeshi likitokomea pande zote.
Les sentinelles de Saül qui étaient à Gabaa de Benjamin virent comment la multitude des Philistins se dispersait et allait de côté et d'autre.
17 Ndipo Sauli akawaambia watu wale waliokuwa pamoja naye, “Kagueni jeshi mkaone ni nani ameondoka katikati yetu.” Walipokagua, akawa ni Yonathani na mbeba silaha wake ambao hawakuwepo.
Saül dit au peuple qui était avec lui: « Faites la revue et voyez qui s'en est allé d'avec nous. » Ils firent la revue, et voici qu'il n'y avait ni Jonathas ni son écuyer.
18 Sauli akamwambia Ahiya, “Leta Sanduku la Mungu.” (Wakati huo lilikuwa kwa Waisraeli.)
Et Saül dit à Achias: « Fais approcher l'arche de Dieu. » — Car l'arche de Dieu était en ce jour-là avec les enfants d'Israël. —
19 Wakati Sauli alipokuwa akisema na kuhani, makelele katika kambi ya Wafilisti yakaongezeka zaidi na zaidi. Hivyo Sauli akamwambia kuhani, “Rudisha mkono wako.”
Pendant que Saül parlait au prêtre, le tumulte qui se faisait dans le camp des Philistins allait croissant; et Saül dit au prêtre: « Retire ta main. »
20 Kisha Sauli na watu wake wote wakakusanyika na kwenda vitani. Wakawakuta Wafilisti wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, wakitiana panga kila mmoja na wenzake.
Puis Saül et tout le peuple qui était avec lui, s'étant rassemblés, s'avancèrent jusqu'au lieu du combat, et voici que l'épée de l'un était tournée contre l'autre, et la confusion était extrême.
21 Wale Waebrania ambao walishakuwa pamoja na Wafilisti, na waliokuwa wamepanda pamoja nao katika kambi zao, wakaenda upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
Les Hébreux qui étaient auparavant avec les Philistins, étant montés avec eux au camp tout autour, se mirent eux aussi du côté de ceux d'Israël qui étaient avec Saül et Jonathas.
22 Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima ya Efraimu waliposikia kuwa Wafilisti wamekimbia, wakajiunga vitani na kuwafuata kwa bidii.
Tous les hommes d'Israël qui s'étaient cachés dans la montagne d'Ephraïm, apprenant la fuite des Philistins, s'attachèrent également à les poursuivre en combattant.
23 Hivyo Bwana akawaokoa Waisraeli siku ile, navyo vita vilienea hadi kupita Beth-Aveni.
C'est ainsi que Yahweh délivra Israël ce jour-là. Le combat se poursuivit jusqu'à Beth-Aven.
24 Basi watu wa Israeli walikuwa katika dhiki siku ile, kwa sababu Sauli alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, akisema, “Alaaniwe mtu yeyote ambaye atakula chakula kabla ya jioni, kabla sijalipiza kisasi juu ya adui zangu!” Kwa hiyo hakuna mtu yeyote katika jeshi aliyeonja chakula.
Les hommes d'Israël étaient à bout de forces en ce jour-là. Saül fit jurer le peuple, en disant: « Maudit soit l'homme qui prendra de la nourriture jusqu'au soir, jusqu'à ce que je me sois vengé de mes ennemis! » Et personne ne goûta de nourriture.
25 Jeshi lote liliingia mwituni, na huko kulikuwepo na asali ardhini.
Tout le peuple vint dans la forêt, et il y avait du miel à la surface du sol.
26 Walipoingia mwituni, wakaona asali ikitiririka, hata hivyo hakuna mtu yeyote aliyetia mkono wake kinywani, kwa sababu waliogopa kiapo.
Et le peuple entra dans la forêt, il vit du miel qui coulait; mais nul ne porta la main à la bouche, car le peuple avait crainte du serment.
27 Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kuwa baba yake alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, hivyo akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya katika sega la asali. Akainua mkono wake na kuutia kinywani mwake, nayo macho yake yakawa maangavu.
Mais Jonathas n'avait pas entendu lorsque son père avait fait faire le serment au peuple; il avança l'extrémité du bâton qu'il avait à la main et, l'ayant plongé dans un rayon de miel, il ramena sa main à sa bouche, et ses yeux furent éclaircis.
28 Kisha mmoja wa askari wake akamwambia, “Baba yako alilifunga jeshi kwa kiapo kikali, akisema, ‘Alaaniwe mtu yeyote alaye chakula leo!’ Ndiyo sababu watu wanalegea.”
Alors quelqu'un du peuple, prenant la parole, lui dit: « Ton père a fait jurer le peuple, en disant: Maudit soit l'homme qui prendra de la nourriture aujourd'hui! Et le peuple était épuisé. »
29 Yonathani akasema, “Baba yangu ameitaabisha nchi. Ona jinsi nilivyopata nguvu mpya nilipoonja asali hii kidogo.
Jonathas dit: « Mon père a causé le malheur du peuple. Voyez donc comme mes yeux sont clairs, parce que j'ai goûté un peu de ce miel!
30 Ingekuwa bora zaidi mara ngapi kama watu wangalikula leo baadhi ya nyara walizoteka kutoka kwa adui zao. Je, mauaji ya Wafilisti yasingekuwa makubwa zaidi?”
Ah! Si le peuple avait mangé aujourd'hui du butin trouvé chez ses ennemis, combien la défaite des Philistins n'aurait-elle pas été plus grande! »
31 Siku ile baada ya Waisraeli kuwaua Wafilisti kutoka Mikmashi mpaka Aiyaloni, walikuwa wamechoka.
Ils battirent ce jour-là les Philistins depuis Machmas jusqu'à Ajalon, et le peuple était tout défaillant.
32 Watu wakarukia zile nyara, wakichukua kondoo, ngʼombe na ndama, wakawachinja hapo juu ya nchi na kuwala, pamoja na damu.
Le peuple se jeta sur le butin et, ayant pris des brebis, des bœufs et des veaux, il les égorgèrent sur la terre, et le peuple en mangea avec le sang.
33 Kisha mtu mmoja akamwambia Sauli, “Tazama, watu wanatenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama yenye damu.” Akasema, “Mmevunja uaminifu. Livingirisheni jiwe kubwa hapa mara moja.”
On le rapporta à Saül, en disant: « Voici que le peuple pèche contre Yahweh, en mangeant la chair avec le sang. » Saül dit: « Vous avez commis une infidélité, roulez à l'instant vers moi une grande pierre. »
34 Kisha Sauli akasema, “Nendeni miongoni mwa watu, mwaambie, ‘Kila mmoja wenu aniletee ngʼombe wake na kondoo, mwachinjie hapa na mle. Msitende dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama ikiwa na damu ndani yake.’” Hivyo kila mmoja akaleta ngʼombe wake jioni ile na kumchinja hapo.
Et Saül dit: « Dispersez-vous parmi le peuple, et dites-leur: Amenez-moi chacun votre bœuf et chacun votre brebis; égorgez-les ici; vous en mangerez alors et vous ne pécherez pas contre Yahweh en mangeant avec le sang. » Et chacun parmi tout le peuple amena pendant la nuit son bœuf par la main, et l'égorgea là.
35 Ndipo Sauli akamjengea Bwana madhabahu, na ndiyo ilivyokuwa mara yake ya kwanza kujenga madhabahu.
Saül bâtit un autel à Yahweh; ce fut le premier autel qu'il éleva pour Yahweh.
36 Sauli akasema, “Tuteremke tufuatie Wafilisti usiku na kuwateka nyara mpaka mapambazuko, nasi tusiache hata mmoja wao hai.” Wakajibu, “Fanya lolote lile uonalo jema zaidi kwako.” Lakini kuhani akasema, “Tuulize kwa Mungu mahali hapa.”
Saül dit: « Descendons, pendant qu'il fait nuit, à la poursuite des Philistins, pillons les jusqu'à ce que luise le matin, et n'en laissons pas survivre un seul. » Ils dirent: « Fais tout ce qui te semblera bon. » Mais le grand prêtre dit: « Approchons-nous ici de Dieu. »
37 Basi Sauli akamuuliza Mungu, akisema, “Je, niteremke kuwafuatia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwa Israeli?” Lakini Mungu hakumjibu siku ile.
Et Saül consulta Dieu: « Descendrai-je à la poursuite des Philistins? Les livrerez-vous entre les mains d'Israël? » Et Yahweh ne lui donna pas de réponse ce jour-là.
38 Kwa hiyo Sauli akasema, “Njooni hapa, ninyi nyote ambao ni viongozi wa jeshi, na tutafute ni dhambi gani imefanywa leo.
Saül dit: « Approchez ici, vous tous, chefs du peuple; recherchez et voyez quel est le péché qui a été commis aujourd'hui.
39 Kwa hakika kama Bwana aiokoaye Israeli aishivyo, hata kama itakuwa juu ya mwana wangu Yonathani, ni lazima afe.” Lakini hakuna mtu yeyote aliyesema neno.
Car, aussi vrai que Yahweh, le libérateur d'Israël, est vivant, le péché fût-il sur mon fils Jonathas, il mourra. » Et dans tout le peuple personne ne lui répondit.
40 Kisha Sauli akawaambia Waisraeli wote, “Ninyi simameni huko; mimi na mwanangu Yonathani tutasimama hapa.” Watu wakajibu, “Fanya lile unaloona jema zaidi kwako.”
Il dit à tout Israël: « Vous, mettez-vous d'un côté, et moi et mon fils Jonathas nous serons de l'autre côté. » Et le peuple dit à Saül: « Fais ce qui te semblera bon. »
41 Kisha Sauli akamwomba Bwana, Mungu wa Israeli, akisema, “Nipe jibu lililo sawa.” Yonathani na Sauli wakatolewa kwa kura, nao watu wakawa salama.
Saül dit à Yahweh: « Dieu d'Israël, fais connaître la vérité! » Jonathas et Saül furent désignés, et le peuple fut libéré.
42 Sauli akasema, “Pigeni kura kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kura ikamwangukia Yonathani.
Alors Saül dit: « Jetez le sort entre moi et Jonathas, mon fils. » Et Jonathas fut désigné.
43 Basi Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie ni nini ulichokifanya.” Hivyo Yonathani akamwambia, “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo yangu. Je, sasa ni lazima nife?”
Saül dit à Jonathas: « Déclare-moi ce que tu as fait. » Jonathas le lui déclara, en disant: « J'ai goûté un peu de miel, avec l'extrémité du bâton que j'avais à la main; me voici, je mourrai! »
44 Sauli akasema, “Mungu na anishughulikie kwa ukali zaidi kama wewe Yonathani hutakufa.”
Et Saül dit: « Que Dieu me traite dans toute sa rigueur, si tu ne meurs pas, Jonathas! »
45 Lakini watu wakamwambia Sauli, “Je, Yonathani atakufa, yeye ambaye ameleta wokovu huu mkubwa Israeli? Hasha! Hakika kama Bwana aishivyo, hakuna hata unywele wa kichwa chake utakaoanguka juu ya ardhi, kwa kuwa alifanya jambo hili leo kwa msaada wa Mungu.” Basi watu wakamwokoa Yonathani, wala hakuuawa.
Le peuple dit à Saül: « Jonathas mourrait donc, lui qui a opéré cette grande délivrance en Israël? Loin de nous! Yahweh est vivant! il ne tombera pas à terre un cheveu de sa tête car c'est avec Dieu qu'il a agi en ce jour. » C'est ainsi que le peuple sauva Jonathas, et il ne mourut point.
46 Kisha Sauli akaacha kuwafuata Wafilisti, nao wakajiondoa na kurudi katika nchi yao.
Saül monta à Gabaa, sans poursuivre les Philistins et les Philistins regagnèrent leur pays.
47 Baada ya Sauli kujitwalia utawala katika Israeli, alipigana dhidi ya adui zake kila upande: Moabu, Waamoni, Edomu, wafalme wa Soba, na Wafilisti. Popote alipogeukia, aliwashinda.
Lorsque Saül eut pris possession de la royauté sur Israël, il fit la guerre aux alentours à tous ses ennemis, à Moab, aux enfants, d'Ammon, à Edom, aux rois de Soba et aux Philistins, et, partout où il se tournait, il l'emportait.
48 Akapigana kishujaa na kuwashinda Waamaleki, akiikomboa Israeli kutoka mikono ya wale waliokuwa wamewateka nyara.
Il fit des exploits, battit Amalec et délivra Israël de la main de ceux qui le pillaient.
49 Wana wa Sauli walikuwa Yonathani, Ishvi na Malki-Shua. Jina la binti yake mkubwa lilikuwa Merabu, naye mdogo aliitwa Mikali.
Les fils de Saül étaient Jonathas, Jessui et Melchisua; ses deux filles s'appelaient, l'aînée Mérob, et la plus jeune Michol.
50 Jina la mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu binti wa Ahimaasi. Jina la jemadari wa jeshi la Sauli aliitwa Abneri mwana wa Neri, naye Neri alikuwa babaye mdogo Sauli.
Le nom de la femme de Saül était Achinoam, fille d'Achimaas. Le nom du chef de son armée était Abner, fils de Ner, oncle de Saül.
51 Babaye Sauli yaani, Kishi na Neri baba yake Abneri walikuwa wana wa Abieli.
Cis, père de Saül, et Ner, père d'Abner, étaient fils d'Abiel.
52 Siku zote za utawala wa Sauli zilikuwa za vita vikali dhidi ya Wafilisti, na wakati wowote Sauli alimwona mtu mwenye nguvu au shujaa, alimchukua kwa utumishi wake.
La guerre fut acharnée contre les Philistins pendant tous les jours de Saül, et quand Saül apercevait un homme fort et vaillant, il l'attachait à son service.

< 1 Samweli 14 >