< 1 Samweli 14 >
1 Siku moja Yonathani mwana wa Sauli akamwambia kijana mbeba silaha wake, akasema, “Njoo, tuwavukie Wafilisti kwenye doria upande ule mwingine.” Lakini hakumwambia baba yake.
Now it happened one day, that Jonathan the son of Saul said unto the young man that bore his armor, Come, and let us go over to the Philistines' outpost, that is on the other side yonder. But unto his father he told nothing.
2 Sauli alikuwa akikaa kwenye viunga vya Gibea chini ya mkomamanga huko Migroni. Alikuwa pamoja na watu kama 600,
And Saul tarried in the lower part of Gib'ah under the pomegranate tree which is by Migron: and the people that were with him were about six hundred men.
3 miongoni mwao alikuwepo Ahiya, ambaye alikuwa amevaa kisibau. Alikuwa mwana wa Ikabodi, nduguye Ahitubu mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo. Hakuna yeyote aliyekuwa na habari kwamba Yonathani alikuwa ameondoka.
And Achiyah, the son of Achitub, the brother of I-chabod, the son of Phinehas, the son of 'Eli, the priest of the Lord in Shiloh, wore the ephod. And the people knew not that Jonathan was gone.
4 Kila upande wa njia ambayo Yonathani alikusudia kupita ili kuvuka kufikia doria ya Wafilisti kulikuwepo na jabali; moja lilikuwa linaitwa Bosesi, na jingine Sene.
And between the passes, by which Jonathan sought to go over unto the outpost of the Philistines, there was a sharp point of rock on the one side, and a sharp point of rock on the other side: and the name of the one was Bozez, and the name of the other Seneh.
5 Jabali moja lilisimama kaskazini kuelekea Mikmashi na jingine upande wa kusini kuelekea Geba.
The one point rose up abruptly northward opposite Michmash, and the other southward opposite Geba'.
6 Yonathani akamwambia kijana wake mbeba silaha, “Njoo, tuvukie doria ya wale jamaa wasiotahiriwa. Huenda Bwana atatenda kwa ajili yetu. Hakuna chochote kitakachoweza kumzuia Bwana kuokoa, kwamba ni kwa wingi au kwa uchache.”
And Jonathan said to the young man that bore his armor, Come, and let us go over unto the outpost of these uncircumcised: it may be that the Lord will work for us; for there is no restraint to the Lord to save by means of many or by means of few.
7 Mbeba silaha wake akamwambia, “Fanya yale yote uliyo nayo katika moyo wako. Songa mbele; moyo wangu na roho yangu viko pamoja nawe.”
And his armor-bearer said unto him, Do all that is in thy heart: turn thee; behold, I am with thee according to thy heart.
8 Yonathani akasema, “Basi njoo; tutavuka kuwaelekea hao watu na kuacha watuone.
Then said Jonathan, Behold, we will pass over unto these men, and we will show ourselves unto them.
9 Kama wakituambia, ‘Subirini hapo mpaka tuje kwenu,’ tutakaa pale tulipo na hatutakwea kwao.
If they say thus unto us, Stand still until we come to you: then will we remain standing in our places, and will not go up unto them.
10 Lakini kama watasema, ‘Pandeni mje kwetu,’ tutakwea, kwa sababu hiyo itakuwa ishara yetu kwamba Bwana amewatia mikononi mwetu.”
But if they say thus, Come up unto us: then will we go up; for the Lord hath delivered them into our hand; and this shall be unto us the sign.
11 Basi wote wawili wakajionyesha kwa doria ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Tazama! Waebrania wanatambaa toka mashimoni walimokuwa wamejificha.”
And when both of them showed themselves unto the outpost of the Philistines, the Philistines said, Behold, Hebrews are coming forth out of the holes wherein they have hidden themselves.
12 Watu wa kwenye doria wakawapigia kelele Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njooni, pandeni kwetu nasi tutawakomesha.” Basi Yonathani akamwambia mbeba silaha wake, “Panda nyuma yangu; Bwana amewatia mikononi mwa Israeli.”
And the men of the outpost addressed Jonathan and his armor-bearer, and said, Come up to us, and we will let you know something. Then said Jonathan unto his armor-bearer, Come up after me; for the Lord hath given them up into the hand of Israel.
13 Yonathani akapanda juu, akitumia mikono yake na miguu, pamoja na mbeba silaha wake papo hapo nyuma yake. Wafilisti wakaanguka mbele ya Yonathani, naye mbeba silaha wake akamfuata akiwaua nyuma yake.
And Jonathan then ascended upon his hands and upon his feet, and his armor-bearer after him: and they fell before Jonathan, and his armor-bearer was killing after him.
14 Katika hilo shambulio la kwanza, Yonathani na mbeba silaha wake waliua kama watu ishirini kwenye eneo kama la nusu eka.
And that first defeat, which Jonathan and his armor-bearer caused, was about twenty men, within about the half of a field, which a yoke of oxen might plough.
15 Kisha fadhaa ikawapata jeshi lote, wale waliokuwa kambini na shambani, wale waliokuwa katika doria na makundi ya washambuliaji, nayo nchi ilitetemeka. Ilikuwa ni hofu ya ghafula iliyotumwa na Mungu.
And there arose a terror in the camp, in the field, and among all the people; the outposts, and the free-booters, they also were terrified, and the earth quaked; and it became a very great terror.
16 Wapelelezi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona jeshi likitokomea pande zote.
And the watchers of Saul in Gib'ah of Benjamin looked; and, behold, the multitude became scattered, and ran hither and thither.
17 Ndipo Sauli akawaambia watu wale waliokuwa pamoja naye, “Kagueni jeshi mkaone ni nani ameondoka katikati yetu.” Walipokagua, akawa ni Yonathani na mbeba silaha wake ambao hawakuwepo.
Then said Saul unto the people that were with him, Muster now, and see who is gone away from us. And they mustered, and, behold, there was neither Jonathan nor his armor-bearer.
18 Sauli akamwambia Ahiya, “Leta Sanduku la Mungu.” (Wakati huo lilikuwa kwa Waisraeli.)
And Saul said unto Achiyah, Bring hither the ark of God; for the ark of God was on that day with the children of Israel.
19 Wakati Sauli alipokuwa akisema na kuhani, makelele katika kambi ya Wafilisti yakaongezeka zaidi na zaidi. Hivyo Sauli akamwambia kuhani, “Rudisha mkono wako.”
And it happened, while Saul was speaking unto the priest, that the confusion which was in the camp of the Philistines went on and increased more and more: And Saul said unto the priest, Withdraw thy hand.
20 Kisha Sauli na watu wake wote wakakusanyika na kwenda vitani. Wakawakuta Wafilisti wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, wakitiana panga kila mmoja na wenzake.
And Saul and all the people that were with him were called together, and they came to the battle; and, behold, the sword of every man was against his fellow, the disorder being very great.
21 Wale Waebrania ambao walishakuwa pamoja na Wafilisti, na waliokuwa wamepanda pamoja nao katika kambi zao, wakaenda upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
And the Hebrews that were with the Philistines as before that time, those namely who had gone up with them, were in the camp round about; but these also resolved to be with the Israelites that were with Saul and Jonathan.
22 Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima ya Efraimu waliposikia kuwa Wafilisti wamekimbia, wakajiunga vitani na kuwafuata kwa bidii.
And all the men of Israel who had hidden themselves on the mountain of Ephraim, heard that the Philistines had fled; and they also followed hard after them in the battle.
23 Hivyo Bwana akawaokoa Waisraeli siku ile, navyo vita vilienea hadi kupita Beth-Aveni.
So the Lord saved Israel that day: and the battle passed over unto Beth-aven.
24 Basi watu wa Israeli walikuwa katika dhiki siku ile, kwa sababu Sauli alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, akisema, “Alaaniwe mtu yeyote ambaye atakula chakula kabla ya jioni, kabla sijalipiza kisasi juu ya adui zangu!” Kwa hiyo hakuna mtu yeyote katika jeshi aliyeonja chakula.
And the men of Israel were hard urged that day; and Saul adjured the people, saying, Cursed be the man that will eat food until the evening, until I have been avenged on my enemies. And the whole people tasted thus no food.
25 Jeshi lote liliingia mwituni, na huko kulikuwepo na asali ardhini.
And [the men of] all the land came to a forest; and there was honey upon the surface of the field.
26 Walipoingia mwituni, wakaona asali ikitiririka, hata hivyo hakuna mtu yeyote aliyetia mkono wake kinywani, kwa sababu waliogopa kiapo.
And when the people were come into the forest, behold, there was a stream of honey; but no one put his hand to his mouth; for the people feared the oath.
27 Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kuwa baba yake alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, hivyo akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya katika sega la asali. Akainua mkono wake na kuutia kinywani mwake, nayo macho yake yakawa maangavu.
But Jonathan had not heard his father charging the people with the oath; he therefore put forth the end of the staff that was in his hand, and dipped it in a honey-comb, and carried his hand again to his mouth; and his eyes became clear.
28 Kisha mmoja wa askari wake akamwambia, “Baba yako alilifunga jeshi kwa kiapo kikali, akisema, ‘Alaaniwe mtu yeyote alaye chakula leo!’ Ndiyo sababu watu wanalegea.”
Then commenced one of the people, and said, Thy father strictly charged the people with an oath, saying, Cursed be the man that will eat food this day; though the people were faint.
29 Yonathani akasema, “Baba yangu ameitaabisha nchi. Ona jinsi nilivyopata nguvu mpya nilipoonja asali hii kidogo.
Then said Jonathan, My father hath troubled the land: see, I pray you, how my eyes become clear, because I have tasted a little of this honey.
30 Ingekuwa bora zaidi mara ngapi kama watu wangalikula leo baadhi ya nyara walizoteka kutoka kwa adui zao. Je, mauaji ya Wafilisti yasingekuwa makubwa zaidi?”
How much more, if haply the people had eaten freely this day of the spoil of their enemies which they found? for would there not have been now a greater defeat among the Philistines?
31 Siku ile baada ya Waisraeli kuwaua Wafilisti kutoka Mikmashi mpaka Aiyaloni, walikuwa wamechoka.
And they smote on that day among the Philistines from Michmash to Ayalon; and the people were very faint.
32 Watu wakarukia zile nyara, wakichukua kondoo, ngʼombe na ndama, wakawachinja hapo juu ya nchi na kuwala, pamoja na damu.
And the people flew upon the spoil, and took sheep, and oxen, and young steers, and slew them on the ground: and the people did eat upon the blood.
33 Kisha mtu mmoja akamwambia Sauli, “Tazama, watu wanatenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama yenye damu.” Akasema, “Mmevunja uaminifu. Livingirisheni jiwe kubwa hapa mara moja.”
And they told Saul, saying, Behold, the people are sinning against the Lord, in eating upon the blood. And he [then] said, Ye have acted treacherously: roll [hither] unto me this day a great stone.
34 Kisha Sauli akasema, “Nendeni miongoni mwa watu, mwaambie, ‘Kila mmoja wenu aniletee ngʼombe wake na kondoo, mwachinjie hapa na mle. Msitende dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama ikiwa na damu ndani yake.’” Hivyo kila mmoja akaleta ngʼombe wake jioni ile na kumchinja hapo.
And Saul said, Disperse yourselves among the people, and say unto them, Bring near unto me every man his ox, and every man his lamb, and slaughter here, and eat; and sin not against the Lord in eating by the blood. And all the people brought near every man his ox by his hand that night, and slaughtered [them] there.
35 Ndipo Sauli akamjengea Bwana madhabahu, na ndiyo ilivyokuwa mara yake ya kwanza kujenga madhabahu.
And Saul built an altar unto the Lord: the same was the first altar that he built unto the Lord.
36 Sauli akasema, “Tuteremke tufuatie Wafilisti usiku na kuwateka nyara mpaka mapambazuko, nasi tusiache hata mmoja wao hai.” Wakajibu, “Fanya lolote lile uonalo jema zaidi kwako.” Lakini kuhani akasema, “Tuulize kwa Mungu mahali hapa.”
And Saul said, Let us go down after the Philistines by night, and spoil them until the morning-light, and let us not leave a man of them. And they said, Do whatsoever seemeth good in thy eyes. Then said the priest, Let us draw near hither unto God.
37 Basi Sauli akamuuliza Mungu, akisema, “Je, niteremke kuwafuatia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwa Israeli?” Lakini Mungu hakumjibu siku ile.
And Saul asked counsel of God, Shall I go down after the Philistines? wilt thou deliver them into the hand of Israel? But he answered him not on that day.
38 Kwa hiyo Sauli akasema, “Njooni hapa, ninyi nyote ambao ni viongozi wa jeshi, na tutafute ni dhambi gani imefanywa leo.
And Saul said, Draw ye near hither all the chief of the people: and know and see through what this sin hath happened this day.
39 Kwa hakika kama Bwana aiokoaye Israeli aishivyo, hata kama itakuwa juu ya mwana wangu Yonathani, ni lazima afe.” Lakini hakuna mtu yeyote aliyesema neno.
For, as the Lord liveth, who saveth Israel, that if it be in Jonathan my son, he shall surely die. But no one answered him among all the people.
40 Kisha Sauli akawaambia Waisraeli wote, “Ninyi simameni huko; mimi na mwanangu Yonathani tutasimama hapa.” Watu wakajibu, “Fanya lile unaloona jema zaidi kwako.”
Then said he unto all Israel, Ye shall be on one side, and I and Jonathan my son will be on the other side. And the people said unto Saul, Do what seemeth good in thy eyes.
41 Kisha Sauli akamwomba Bwana, Mungu wa Israeli, akisema, “Nipe jibu lililo sawa.” Yonathani na Sauli wakatolewa kwa kura, nao watu wakawa salama.
And Saul said unto the Lord, God of Israel, O, show forth the perfect truth. And Jonathan and Saul were seized; but the people came forth [free].
42 Sauli akasema, “Pigeni kura kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kura ikamwangukia Yonathani.
And Saul said, Cast the lot between me and Jonathan my son. And Jonathan was seized.
43 Basi Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie ni nini ulichokifanya.” Hivyo Yonathani akamwambia, “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo yangu. Je, sasa ni lazima nife?”
Then said Saul to Jonathan, Do tell me what thou hast done. And Jonathan told him, and said, I did but taste with the end of the staff that was in my hand a little honey: lo, I am willing to die.
44 Sauli akasema, “Mungu na anishughulikie kwa ukali zaidi kama wewe Yonathani hutakufa.”
And Saul said, May God do thus now, and in future also; for thou shalt surely die, Jonathan.
45 Lakini watu wakamwambia Sauli, “Je, Yonathani atakufa, yeye ambaye ameleta wokovu huu mkubwa Israeli? Hasha! Hakika kama Bwana aishivyo, hakuna hata unywele wa kichwa chake utakaoanguka juu ya ardhi, kwa kuwa alifanya jambo hili leo kwa msaada wa Mungu.” Basi watu wakamwokoa Yonathani, wala hakuuawa.
And the people said unto Saul, Shall Jonathan die, who hath wrought this great salvation in Israel? This shall not be: as the Lord liveth, there shall not fall one hair of his head to the ground; for with God hath he wrought this day. So the people rescued Jonathan, and he died not.
46 Kisha Sauli akaacha kuwafuata Wafilisti, nao wakajiondoa na kurudi katika nchi yao.
Then went Saul up from following the Philistines; and the Philistines went to their own place.
47 Baada ya Sauli kujitwalia utawala katika Israeli, alipigana dhidi ya adui zake kila upande: Moabu, Waamoni, Edomu, wafalme wa Soba, na Wafilisti. Popote alipogeukia, aliwashinda.
So Saul strengthened himself in the government over Israel; and he fought on every side against all his enemies, against Moab, and against the children of 'Ammon, and against Edom, and against the kings of Zobah, and against the Philistines: and whithersoever he turned himself, he caused terror.
48 Akapigana kishujaa na kuwashinda Waamaleki, akiikomboa Israeli kutoka mikono ya wale waliokuwa wamewateka nyara.
And he gathered an army, and he smote the 'Amalekites, and delivered Israel out of the hands of those that spoiled them.
49 Wana wa Sauli walikuwa Yonathani, Ishvi na Malki-Shua. Jina la binti yake mkubwa lilikuwa Merabu, naye mdogo aliitwa Mikali.
Now the sons of Saul were Jonathan, and Yishvi, and Malkishua': and the names of his two daughters—the name of the first-born was Merab, and the name of the younger Michal.
50 Jina la mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu binti wa Ahimaasi. Jina la jemadari wa jeshi la Sauli aliitwa Abneri mwana wa Neri, naye Neri alikuwa babaye mdogo Sauli.
And the name of Saul's wife was Achino'am, the daughter of Achima'az: and the name of the captain of his army was Abner, the son of Ner, Saul's uncle.
51 Babaye Sauli yaani, Kishi na Neri baba yake Abneri walikuwa wana wa Abieli.
And Kish the father of Saul, and Ner the father of Abner, were each the son of Abiel.
52 Siku zote za utawala wa Sauli zilikuwa za vita vikali dhidi ya Wafilisti, na wakati wowote Sauli alimwona mtu mwenye nguvu au shujaa, alimchukua kwa utumishi wake.
And the war against the Philistines was violent all the days of Saul: and when Saul saw any strong man, or any valiant man, he took him unto himself.