< 1 Samweli 14 >

1 Siku moja Yonathani mwana wa Sauli akamwambia kijana mbeba silaha wake, akasema, “Njoo, tuwavukie Wafilisti kwenye doria upande ule mwingine.” Lakini hakumwambia baba yake.
Then on a day Ionathan the sonne of Saul sayde vnto the yong man that bare his armour, Come and let vs goe ouer towarde the Philistims garison, that is yonder on the other side, but he tolde not his father.
2 Sauli alikuwa akikaa kwenye viunga vya Gibea chini ya mkomamanga huko Migroni. Alikuwa pamoja na watu kama 600,
And Saul taried in the border of Gibeah vnder a pomegranate tree, which was in Migron, and the people that were with him, were about sixe hundreth men.
3 miongoni mwao alikuwepo Ahiya, ambaye alikuwa amevaa kisibau. Alikuwa mwana wa Ikabodi, nduguye Ahitubu mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo. Hakuna yeyote aliyekuwa na habari kwamba Yonathani alikuwa ameondoka.
And Ahiah the sonne of Ahitub, Ichabods brother, the sonne of Phinehas, the sonne of Eli, was the Lordes Priest in Shiloh, and ware an Ephod: and the people knewe not that Ionathan was gone.
4 Kila upande wa njia ambayo Yonathani alikusudia kupita ili kuvuka kufikia doria ya Wafilisti kulikuwepo na jabali; moja lilikuwa linaitwa Bosesi, na jingine Sene.
Nowe in the way whereby Ionathan sought to go ouer to the Philistims garison, there was a sharpe rocke on the one side, and a sharpe rocke on the other side: the name of the one was called Bozez, and the name of the other Seneh.
5 Jabali moja lilisimama kaskazini kuelekea Mikmashi na jingine upande wa kusini kuelekea Geba.
The one rocke stretched from the North towarde Michmash, and the other was from the South toward Gibeah.
6 Yonathani akamwambia kijana wake mbeba silaha, “Njoo, tuvukie doria ya wale jamaa wasiotahiriwa. Huenda Bwana atatenda kwa ajili yetu. Hakuna chochote kitakachoweza kumzuia Bwana kuokoa, kwamba ni kwa wingi au kwa uchache.”
And Ionathan saide to the yong man that bare his armour, Come, and let vs goe ouer vnto the garison of these vncircumcised: it may be that the Lord will worke with vs: for it is not hard to the Lord to saue with many, or with fewe.
7 Mbeba silaha wake akamwambia, “Fanya yale yote uliyo nayo katika moyo wako. Songa mbele; moyo wangu na roho yangu viko pamoja nawe.”
And he that bare his armour, saide vnto him, Doe all that is in thine heart: goe where it pleaseth thee: beholde, I am with thee as thine heart desireth.
8 Yonathani akasema, “Basi njoo; tutavuka kuwaelekea hao watu na kuacha watuone.
Then said Ionathan, Beholde, we goe ouer vnto those men, and will shewe our selues vnto them.
9 Kama wakituambia, ‘Subirini hapo mpaka tuje kwenu,’ tutakaa pale tulipo na hatutakwea kwao.
If they say on this wise to vs, Tarie vntill we come to you, then we will stand still in our place, and not goe vp to them.
10 Lakini kama watasema, ‘Pandeni mje kwetu,’ tutakwea, kwa sababu hiyo itakuwa ishara yetu kwamba Bwana amewatia mikononi mwetu.”
But if they say, Come vp vnto vs, then we will goe vp: for the Lord hath deliuered them into our hande: and this shall be a signe vnto vs.
11 Basi wote wawili wakajionyesha kwa doria ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Tazama! Waebrania wanatambaa toka mashimoni walimokuwa wamejificha.”
So they both shewed themselues vnto the garison of the Philistims: and the Philistims said, See, the Ebrewes come out of the holes wherein they had hid themselues.
12 Watu wa kwenye doria wakawapigia kelele Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njooni, pandeni kwetu nasi tutawakomesha.” Basi Yonathani akamwambia mbeba silaha wake, “Panda nyuma yangu; Bwana amewatia mikononi mwa Israeli.”
And the men of the garison answered Ionathan, and his armour bearer, and said, Come vp to vs: for we will shewe you a thing. Then Ionathan said vnto his armour bearer, Come vp after me: for the Lord hath deliuered them into the hand of Israel.
13 Yonathani akapanda juu, akitumia mikono yake na miguu, pamoja na mbeba silaha wake papo hapo nyuma yake. Wafilisti wakaanguka mbele ya Yonathani, naye mbeba silaha wake akamfuata akiwaua nyuma yake.
So Ionathan went vp vpon his hands and vpon his feete, and his armour bearer after him: and some fell before Ionathan, and his armour bearer slewe others after him.
14 Katika hilo shambulio la kwanza, Yonathani na mbeba silaha wake waliua kama watu ishirini kwenye eneo kama la nusu eka.
So the first slaughter which Ionathan and his armour bearer made, was about twentie men, as it were within halfe an acre of land which two oxen plowe.
15 Kisha fadhaa ikawapata jeshi lote, wale waliokuwa kambini na shambani, wale waliokuwa katika doria na makundi ya washambuliaji, nayo nchi ilitetemeka. Ilikuwa ni hofu ya ghafula iliyotumwa na Mungu.
And there was a feare in the hoste, and in the field, and among all the people: the garison also, and they that went out to spoyle, were afraid themselues: and the earth trembled: for it was striken with feare by God.
16 Wapelelezi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona jeshi likitokomea pande zote.
Then the watchmen of Saul in Gibeah of Beniamin sawe: and beholde, the multitude was discomfited, and smitten as they went.
17 Ndipo Sauli akawaambia watu wale waliokuwa pamoja naye, “Kagueni jeshi mkaone ni nani ameondoka katikati yetu.” Walipokagua, akawa ni Yonathani na mbeba silaha wake ambao hawakuwepo.
Therefore saide Saul vnto the people that were with him, Search nowe and see, who is gone from vs. And when they had nombred, beholde, Ionathan and his armour bearer were not there.
18 Sauli akamwambia Ahiya, “Leta Sanduku la Mungu.” (Wakati huo lilikuwa kwa Waisraeli.)
And Saul said vnto Ahiah, Bring hither the Arke of God (for the Arke of God was at that time with the children of Israel)
19 Wakati Sauli alipokuwa akisema na kuhani, makelele katika kambi ya Wafilisti yakaongezeka zaidi na zaidi. Hivyo Sauli akamwambia kuhani, “Rudisha mkono wako.”
And while Saul talked vnto the Priest, the noyse that was in the hoste of the Philistims, spred farther abroade, and encreased: therefore Saul said vnto the Priest, Withdraw thine hand.
20 Kisha Sauli na watu wake wote wakakusanyika na kwenda vitani. Wakawakuta Wafilisti wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, wakitiana panga kila mmoja na wenzake.
And Saul was assembled with all the people that were with him, and they came to the battell: and behold, euery mans sworde was against his fellow, and there was a very great discomfiture.
21 Wale Waebrania ambao walishakuwa pamoja na Wafilisti, na waliokuwa wamepanda pamoja nao katika kambi zao, wakaenda upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
Moreouer, the Ebrewes that were with the Philistims beforetime, and were come with them into all partes of the hoste, euen they also turned to be with the Israelites that were with Saul and Ionathan.
22 Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima ya Efraimu waliposikia kuwa Wafilisti wamekimbia, wakajiunga vitani na kuwafuata kwa bidii.
Also all the men of Israel which had hid themselues in mount Ephraim, when they heard, that the Philistims were fled, they followed after them in the battell.
23 Hivyo Bwana akawaokoa Waisraeli siku ile, navyo vita vilienea hadi kupita Beth-Aveni.
And so the Lord saued Israel that day: and the battell continued vnto Beth-auen.
24 Basi watu wa Israeli walikuwa katika dhiki siku ile, kwa sababu Sauli alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, akisema, “Alaaniwe mtu yeyote ambaye atakula chakula kabla ya jioni, kabla sijalipiza kisasi juu ya adui zangu!” Kwa hiyo hakuna mtu yeyote katika jeshi aliyeonja chakula.
And at that time the men of Israel were pressed with hunger: for Saul charged the people with an othe, saying, Cursed be the man that eateth foode till night, that I may be auenged of mine enemies: so none of the people tasted any sustenance.
25 Jeshi lote liliingia mwituni, na huko kulikuwepo na asali ardhini.
And all they of the land came to a wood, where hony lay vpon the ground.
26 Walipoingia mwituni, wakaona asali ikitiririka, hata hivyo hakuna mtu yeyote aliyetia mkono wake kinywani, kwa sababu waliogopa kiapo.
And the people came into the wood, and beholde, the hony dropped, and no man mooued his hand to his mouth: for the people feared the othe.
27 Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kuwa baba yake alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, hivyo akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya katika sega la asali. Akainua mkono wake na kuutia kinywani mwake, nayo macho yake yakawa maangavu.
But Ionathan heard not when his father charged the people with the othe: wherefore he put foorth the ende of the rod that was in his hand, and dipt it in an hony combe, and put his hand to his mouth, and his eyes receiued sight.
28 Kisha mmoja wa askari wake akamwambia, “Baba yako alilifunga jeshi kwa kiapo kikali, akisema, ‘Alaaniwe mtu yeyote alaye chakula leo!’ Ndiyo sababu watu wanalegea.”
Then answered one of the people, and said, Thy father made the people to sweare, saying, Cursed be the man that eateth sustenance this day: and the people were faint.
29 Yonathani akasema, “Baba yangu ameitaabisha nchi. Ona jinsi nilivyopata nguvu mpya nilipoonja asali hii kidogo.
Then said Ionathan, My father hath troubled the land: see nowe howe mine eyes are made cleare, because I haue tasted a litle of this honie:
30 Ingekuwa bora zaidi mara ngapi kama watu wangalikula leo baadhi ya nyara walizoteka kutoka kwa adui zao. Je, mauaji ya Wafilisti yasingekuwa makubwa zaidi?”
Howe much more, if the people had eaten to day of the spoyle of their enemies which they found? for had there not bene nowe a greater slaughter among the Philistims?
31 Siku ile baada ya Waisraeli kuwaua Wafilisti kutoka Mikmashi mpaka Aiyaloni, walikuwa wamechoka.
And they smote the Philistims that day, from Michmash to Aiialon: and the people were exceeding faint.
32 Watu wakarukia zile nyara, wakichukua kondoo, ngʼombe na ndama, wakawachinja hapo juu ya nchi na kuwala, pamoja na damu.
So the people turned to the spoile, and tooke sheepe, and oxen, and calues, and slewe them on the ground, and the people did eate them with the blood.
33 Kisha mtu mmoja akamwambia Sauli, “Tazama, watu wanatenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama yenye damu.” Akasema, “Mmevunja uaminifu. Livingirisheni jiwe kubwa hapa mara moja.”
Then men tolde Saul, saying, Beholde, the people sinne against the Lord, in that they eate with the blood. And he saide, Ye haue trespassed: roule a great stone vnto me this day.
34 Kisha Sauli akasema, “Nendeni miongoni mwa watu, mwaambie, ‘Kila mmoja wenu aniletee ngʼombe wake na kondoo, mwachinjie hapa na mle. Msitende dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama ikiwa na damu ndani yake.’” Hivyo kila mmoja akaleta ngʼombe wake jioni ile na kumchinja hapo.
Againe Saul said, Goe abroade among the people, and bid them bring me euery man his oxe, and euery man his sheepe, and slay them here, and eate and sinne not against the Lord in eating with the blood. And ye people brought euery man his oxe in his hand that night, and slew them there.
35 Ndipo Sauli akamjengea Bwana madhabahu, na ndiyo ilivyokuwa mara yake ya kwanza kujenga madhabahu.
Then Saul made an altar vnto the Lord, and that was the first altar that he made vnto the Lord.
36 Sauli akasema, “Tuteremke tufuatie Wafilisti usiku na kuwateka nyara mpaka mapambazuko, nasi tusiache hata mmoja wao hai.” Wakajibu, “Fanya lolote lile uonalo jema zaidi kwako.” Lakini kuhani akasema, “Tuulize kwa Mungu mahali hapa.”
And Saul saide, Let vs goe downe after the Philistims by night, and spoyle them vntill the morning shine, and let vs not leaue a man of them. And they saide, Doe whatsoeuer thou thinkest best. Then saide the Priest, Let vs drawe neere hither vnto God.
37 Basi Sauli akamuuliza Mungu, akisema, “Je, niteremke kuwafuatia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwa Israeli?” Lakini Mungu hakumjibu siku ile.
So Saul asked of God, saying, Shall I goe downe after ye Philistims? wilt thou deliuer them into the hands of Israel? But he answered him not at that time.
38 Kwa hiyo Sauli akasema, “Njooni hapa, ninyi nyote ambao ni viongozi wa jeshi, na tutafute ni dhambi gani imefanywa leo.
And Saul said, All ye chiefe of the people, come ye hither, and knowe, and see by whom this sinne is done this day.
39 Kwa hakika kama Bwana aiokoaye Israeli aishivyo, hata kama itakuwa juu ya mwana wangu Yonathani, ni lazima afe.” Lakini hakuna mtu yeyote aliyesema neno.
For as the Lord liueth, which saueth Israel, though it be done by Ionathan my sonne, he shall dye the death. But none of all the people answered him.
40 Kisha Sauli akawaambia Waisraeli wote, “Ninyi simameni huko; mimi na mwanangu Yonathani tutasimama hapa.” Watu wakajibu, “Fanya lile unaloona jema zaidi kwako.”
Then he saide vnto all Israel, Be ye on one side, and I and Ionathan my sonne will be on the other side. And the people saide vnto Saul, Doe what thou thinkest best.
41 Kisha Sauli akamwomba Bwana, Mungu wa Israeli, akisema, “Nipe jibu lililo sawa.” Yonathani na Sauli wakatolewa kwa kura, nao watu wakawa salama.
Then Saul said vnto the Lord God of Israel, Giue a perfite lot. And Ionathan and Saul were taken, but the people escaped.
42 Sauli akasema, “Pigeni kura kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kura ikamwangukia Yonathani.
And Saul saide, Cast lot betweene me and Ionathan my sonne. And Ionathan was taken.
43 Basi Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie ni nini ulichokifanya.” Hivyo Yonathani akamwambia, “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo yangu. Je, sasa ni lazima nife?”
Then Saul said to Ionathan, Tell me what thou hast done. And Ionathan tolde him, and said, I tasted a litle hony with the ende of the rod, that was in mine hand, and loe, I must die.
44 Sauli akasema, “Mungu na anishughulikie kwa ukali zaidi kama wewe Yonathani hutakufa.”
Againe Saul answered, God doe so and more also, vnlesse thou die the death, Ionathan.
45 Lakini watu wakamwambia Sauli, “Je, Yonathani atakufa, yeye ambaye ameleta wokovu huu mkubwa Israeli? Hasha! Hakika kama Bwana aishivyo, hakuna hata unywele wa kichwa chake utakaoanguka juu ya ardhi, kwa kuwa alifanya jambo hili leo kwa msaada wa Mungu.” Basi watu wakamwokoa Yonathani, wala hakuuawa.
And the people said vnto Saul, Shall Ionathan die, who hath so mightily deliuered Israel? God forbid. As the Lord liueth, there shall not one heare of his head fall to the ground: for he hath wrought with God this day. So the people deliuered Ionathan that he dyed not.
46 Kisha Sauli akaacha kuwafuata Wafilisti, nao wakajiondoa na kurudi katika nchi yao.
Then Saul came vp from the Philistims: and the Philistims went to their owne place.
47 Baada ya Sauli kujitwalia utawala katika Israeli, alipigana dhidi ya adui zake kila upande: Moabu, Waamoni, Edomu, wafalme wa Soba, na Wafilisti. Popote alipogeukia, aliwashinda.
So Saul helde the kingdome ouer Israel, and fought against all his enemies on euery side, against Moab, and against the children of Ammon, and against Edom, and against the Kings of Zobah, and against the Philistims: and whithersoeuer he went, he handled them as wicked men.
48 Akapigana kishujaa na kuwashinda Waamaleki, akiikomboa Israeli kutoka mikono ya wale waliokuwa wamewateka nyara.
He gathered also an hoste and smote Amalek, and deliuered Israel out of the handes of them that spoyled them.
49 Wana wa Sauli walikuwa Yonathani, Ishvi na Malki-Shua. Jina la binti yake mkubwa lilikuwa Merabu, naye mdogo aliitwa Mikali.
Nowe the sonnes of Saul were Ionathan, and Ishui, and Malchishua: and the names of his two daughters, the elder was called Merab, and the yonger was named Michal.
50 Jina la mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu binti wa Ahimaasi. Jina la jemadari wa jeshi la Sauli aliitwa Abneri mwana wa Neri, naye Neri alikuwa babaye mdogo Sauli.
And the name of Sauls wife was Ahinoam the daughter of Ahimaaz: and the name of his chiefe captaine was Abner the sonne of Ner, Sauls vncle.
51 Babaye Sauli yaani, Kishi na Neri baba yake Abneri walikuwa wana wa Abieli.
And Kish was Sauls father: and Ner the father of Abner was the sonne of Abiel.
52 Siku zote za utawala wa Sauli zilikuwa za vita vikali dhidi ya Wafilisti, na wakati wowote Sauli alimwona mtu mwenye nguvu au shujaa, alimchukua kwa utumishi wake.
And there was sore warre against the Philistims all the dayes of Saul: and whomsoeuer Saul sawe to be a strong man, and meete for the warre, he tooke him vnto him.

< 1 Samweli 14 >