< 1 Samweli 13 >
1 Sauli alikuwa na miaka thelathini, alipokuwa mfalme, akatawala Israeli miaka arobaini na miwili.
A son of a year [is] Saul in his reigning, yea, two years he hath reigned over Israel,
2 Sauli alichagua watu 3,000 kutoka Israeli; miongoni mwa hao watu 2,000 walikuwa pamoja naye huko Mikmashi na katika nchi ya vilima ya Betheli, nao watu 1,000 walikuwa pamoja na Yonathani huko Gibea ya Benyamini. Watu waliosalia aliwarudisha nyumbani mwao.
and Saul chooseth for himself three thousand [men] out of Israel; and two thousand are with Saul in Michmash, and in the hill-country of Beth-El; and a thousand have been with Jonathan in Gibeah of Benjamin; and the remnant of the people he hath sent each to his tents.
3 Yonathani akashambulia ngome ya Wafilisti huko Geba, nao Wafilisti wakapata habari hizo. Kisha Sauli akaamuru tarumbeta ipigwe nchi yote na kusema, “Waebrania na wasikie!”
And Jonathan smiteth the garrison of the Philistines which [is] in Geba, and the Philistines hear, and Saul hath blown with a trumpet through all the land, saying, 'Let the Hebrews hear.'
4 Hivyo Israeli wote wakasikia habari kwamba: “Sauli ameshambulia ngome ya Wafilisti, nao sasa Israeli wamekuwa harufu mbaya kwa Wafilisti.” Basi watu waliitwa kuungana na Sauli huko Gilgali.
And all Israel have heard, saying, 'Saul hath smitten the garrison of the Philistines,' and also, 'Israel hath been abhorred by the Philistines;' and the people are called after Saul to Gilgal.
5 Wafilisti wakakusanyika ili kupigana na Israeli, wakiwa na magari ya vita 3,000, waendesha magari ya vita 6,000 na askari wa miguu wengi kama mchanga wa ufuoni mwa bahari. Walipanda na kupiga kambi huko Mikmashi, mashariki ya Beth-Aveni.
And the Philistines have been gathered to fight with Israel; thirty thousand chariots, and six thousand horsemen, and a people as the sand which [is] on the sea-shore for multitude; and they come up and encamp in Michmash, east of Beth-Aven.
6 Watu wa Israeli walipoona kuwa hali yao ni ya hatari na kuwa jeshi lao limesongwa sana, wakajificha katika mapango na katika vichaka, katikati ya miamba, kwenye mashimo na kwenye mahandaki.
And the men of Israel have seen that they are distressed, that the people hath been oppressed, and the people hide themselves in caves, and in thickets, and in rocks, and in high places, and in pits.
7 Hata baadhi ya Waebrania wakavuka Yordani mpaka nchi ya Gadi na Gileadi. Sauli akabaki huko Gilgali, navyo vikosi vyote vilivyokuwa pamoja naye vilikuwa vikitetemeka kwa hofu.
And Hebrews have passed over the Jordan to the land of Gad and Gilead; and Saul [is] yet in Gilgal, and all the people have trembled after him.
8 Akangoja kwa siku saba, muda uliowekwa na Samweli; lakini Samweli hakuja Gilgali, nao watu wa Sauli wakaanza kutawanyika.
And he waiteth seven days, according to the appointment with Samuel, and Samuel hath not come to Gilgal, and the people are scattered from off him.
9 Basi akasema, “Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani.” Naye Sauli akatoa sadaka ya kuteketezwa.
And Saul saith, 'Bring nigh unto me the burnt-offering, and the peace-offerings;' and he causeth the burnt-offering to ascend.
10 Mara alipomaliza kutoa hiyo sadaka, Samweli akatokea, naye Sauli akaondoka kwenda kumlaki.
And it cometh to pass at his completing to cause the burnt-offering to ascend, that lo, Samuel hath come, and Saul goeth out to meet him, to bless him;
11 Samweli akamuuliza, “Umefanya nini?” Sauli akajibu, “Nilipoona kwamba watu wanatawanyika, na kwamba hukuja wakati uliopangwa na kwamba Wafilisti walikuwa wakikusanyika huko Mikmashi,
and Samuel saith, 'What hast thou done?' And Saul saith, 'Because I saw that the people were scattered from off me, and thou hadst not come at the appointment of the days, and the Philistines are gathered to Michmash,
12 nikawaza, ‘Sasa Wafilisti watateremka dhidi yangu huko Gilgali nami sijaomba kibali kwa Bwana.’ Hivyo nikalazimika kutoa sadaka ya kuteketezwa.”
and I say, Now do the Philistines come down unto me to Gilgal, and the face of Jehovah I have not appeased; and I force myself, and cause the burnt-offering to ascend.'
13 Samweli akasema, “Umetenda kwa upumbavu. Hukuyashika maagizo ya Bwana Mungu wako aliyokupa. Kama ungelitii, angeudumisha ufalme wako juu ya Israeli kwa wakati wote.
And Samuel saith unto Saul, 'Thou hast been foolish; thou hast not kept the command of Jehovah thy God, which He commanded thee, for now had Jehovah established thy kingdom over Israel unto the age;
14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amemtafuta mtu aupendezaye moyo wake, na amemchagua awe kiongozi wa watu wake, kwa sababu hukuyatii maagizo ya Bwana.”
and, now, thy kingdom doth not stand, Jehovah hath sought for Himself a man according to His own heart, and Jehovah chargeth him for leader over His people, for thou hast not kept that which Jehovah commanded thee.'
15 Kisha Samweli akaondoka Gilgali, akapanda Gibea ya Benyamini, naye Sauli akawahesabu watu aliokuwa nao. Jumla yao walikuwa watu 600.
And Samuel riseth, and goeth up from Gilgal to Gibeah of Benjamin; and Saul inspecteth the people who are found with him, about six hundred men,
16 Sauli, mwanawe Yonathani na watu waliokuwa pamoja nao walikuwa wakiishi huko Gibea ya Benyamini, wakati Wafilisti wakiwa wamepiga kambi huko Mikmashi.
and Saul, and Jonathan his son, and the people who are found with them, are abiding in Gibeah of Benjamin, and the Philistines have encamped in Michmash.
17 Makundi ya wavamiaji walikuja kutoka kambi ya Wafilisti katika vikosi vitatu. Kikosi kimoja kilielekea Ofra karibu na Shuali,
And the destroyer goeth out from the camp of the Philistines — three detachments; the one detachment turneth unto the way of Ophrah, unto the land of Shual;
18 kikosi kingine kilielekea Beth-Horoni, nacho kikosi cha tatu kilielekea kwenye nchi ya mpakani ielekeayo Bonde la Seboimu linalotazamana na jangwa.
and the one detachment turneth the way of Beth-Horon, and the one detachment turneth the way of the border which is looking on the valley of the Zeboim, toward the wilderness.
19 Hapakuwa na mhunzi ambaye angeweza kupatikana katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walikuwa wamesema, “Waebrania wasije wakatengeneza panga au mikuki!”
And an artificer is not found in all the land of Israel, for the Philistines said, 'Lest the Hebrews make sword or spear;'
20 Hivyo Waisraeli wote huteremka kwa Wafilisti ili kunoa majembe ya plau, majembe ya mkono, mashoka na miundu.
and all Israel go down to the Philistines, to sharpen each his ploughshare, and his coulter, and his axe, and his mattock;
21 Bei ilikuwa fedha theluthi mbili za shekeli kunoa majembe ya plau na majembe ya mkono, na theluthi moja ya shekeli kwa nyuma, mashoka na michokoo.
and there hath been the file for mattocks, and for coulters, and for three-pronged rakes, and for the axes, and to set up the goads.
22 Kwa hiyo siku ya vita hakuna askari yeyote aliyekuwa kambini na Sauli na Yonathani ambaye alikuwa na upanga wala mkuki mkononi mwake; Sauli tu na mwanawe Yonathani ndio waliokuwa navyo.
And it hath been, in the day of battle, that there hath not been found sword and spear in the hand of any of the people who [are] with Saul and with Jonathan — and there is found to Saul and to Jonathan his son.
23 Basi kikosi cha Wafilisti kilikuwa kimetoka kuelekea njia iendayo Mikmashi.
And the station of the Philistines goeth out unto the passage of Michmash.