< 1 Samweli 13 >

1 Sauli alikuwa na miaka thelathini, alipokuwa mfalme, akatawala Israeli miaka arobaini na miwili.
Šaulu je bilo ... godina kad je postao kralj, a kraljevao je ... i dvije godine nad Izraelom.
2 Sauli alichagua watu 3,000 kutoka Israeli; miongoni mwa hao watu 2,000 walikuwa pamoja naye huko Mikmashi na katika nchi ya vilima ya Betheli, nao watu 1,000 walikuwa pamoja na Yonathani huko Gibea ya Benyamini. Watu waliosalia aliwarudisha nyumbani mwao.
Šaul izabra sebi tri tisuće Izraelaca: dvije tisuće od njih bijahu sa Šaulom u Mikmasu i u Betelskoj gori, a jedna tisuća bijaše s Jonatanom u Benjaminovoj Gebi. Ostali je narod Šaul otpustio svakoga u njegov šator.
3 Yonathani akashambulia ngome ya Wafilisti huko Geba, nao Wafilisti wakapata habari hizo. Kisha Sauli akaamuru tarumbeta ipigwe nchi yote na kusema, “Waebrania na wasikie!”
Jonatan sruši filistejski stup koji je stajao u Gibei i Filistejci saznaše da su se Hebreji pobunili. Šaul zapovjedi te zatrubiše u rog po svoj zemlji
4 Hivyo Israeli wote wakasikia habari kwamba: “Sauli ameshambulia ngome ya Wafilisti, nao sasa Israeli wamekuwa harufu mbaya kwa Wafilisti.” Basi watu waliitwa kuungana na Sauli huko Gilgali.
i sav Izrael doznade novost: “Šaul je srušio filistejski stup, Izrael se omrazio Filistejcima!” I narod se poče skupljati oko Šaula u Gilgalu.
5 Wafilisti wakakusanyika ili kupigana na Israeli, wakiwa na magari ya vita 3,000, waendesha magari ya vita 6,000 na askari wa miguu wengi kama mchanga wa ufuoni mwa bahari. Walipanda na kupiga kambi huko Mikmashi, mashariki ya Beth-Aveni.
A Filistejci se skupiše da vojuju na Izraela: tri tisuće bojnih kola, šest tisuća konja, a mnoštvo naroda kao pijeska na morskoj obali. I utaboriše se kod Mikmasa, istočno od Bet Avena.
6 Watu wa Israeli walipoona kuwa hali yao ni ya hatari na kuwa jeshi lao limesongwa sana, wakajificha katika mapango na katika vichaka, katikati ya miamba, kwenye mashimo na kwenye mahandaki.
Kad su Izraelci vidjeli da su u nevolji i da je narod pritisnut od neprijatelja, posakrivaše se u pećine, jame, kamenjake, jarke i čatrnje.
7 Hata baadhi ya Waebrania wakavuka Yordani mpaka nchi ya Gadi na Gileadi. Sauli akabaki huko Gilgali, navyo vikosi vyote vilivyokuwa pamoja naye vilikuwa vikitetemeka kwa hofu.
Neki su prešli i preko gazova Jordana u zemlju Gadovu i Gileadovu. Šaul je još bio u Gilgalu, a sav je narod oko njega drhtao od straha.
8 Akangoja kwa siku saba, muda uliowekwa na Samweli; lakini Samweli hakuja Gilgali, nao watu wa Sauli wakaanza kutawanyika.
On pričeka sedam dana kako mu je odredio Samuel; ali kad Samuel nije došao u Gilgal, narod se stade razilaziti od Šaula.
9 Basi akasema, “Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani.” Naye Sauli akatoa sadaka ya kuteketezwa.
Tada reče Šaul: “Donesite mi žrtvu paljenicu i žrtve pričesnice!” I prinese žrtvu paljenicu.
10 Mara alipomaliza kutoa hiyo sadaka, Samweli akatokea, naye Sauli akaondoka kwenda kumlaki.
I upravo je završavao žrtvu paljenicu, kad eto Samuela; Šaul mu iziđe u susret da ga pozdravi.
11 Samweli akamuuliza, “Umefanya nini?” Sauli akajibu, “Nilipoona kwamba watu wanatawanyika, na kwamba hukuja wakati uliopangwa na kwamba Wafilisti walikuwa wakikusanyika huko Mikmashi,
Samuel ga upita: “Što si učinio?” A Šaul odgovori: “Kad sam vidio da se narod razilazi od mene, a ti da ne dolaziš do određenoga dana, a Filistejci se skupili u Mikmasu,
12 nikawaza, ‘Sasa Wafilisti watateremka dhidi yangu huko Gilgali nami sijaomba kibali kwa Bwana.’ Hivyo nikalazimika kutoa sadaka ya kuteketezwa.”
pomislio sam: sad će udariti Filistejci na me u Gilgalu, a ja neću stići molitvom ublažiti Jahvu! Zato se odvažih i prinesoh žrtvu paljenicu.”
13 Samweli akasema, “Umetenda kwa upumbavu. Hukuyashika maagizo ya Bwana Mungu wako aliyokupa. Kama ungelitii, angeudumisha ufalme wako juu ya Israeli kwa wakati wote.
Samuel tada reče Šaulu: “Ludo si radio! Da si održao zapovijed koju ti je dao Jahve, tvoj Bog, Jahve bi učvrstio tvoje kraljevstvo nad Izraelom dovijeka.
14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amemtafuta mtu aupendezaye moyo wake, na amemchagua awe kiongozi wa watu wake, kwa sababu hukuyatii maagizo ya Bwana.”
A sada se tvoje kraljevstvo neće trajno održati: Jahve je potražio sebi čovjeka po svom srcu i odredio ga za kneza nad svojim narodom, jer ti nisi održao što ti je Jahve zapovjedio.”
15 Kisha Samweli akaondoka Gilgali, akapanda Gibea ya Benyamini, naye Sauli akawahesabu watu aliokuwa nao. Jumla yao walikuwa watu 600.
Nato Samuel ustade i ode iz Gilgala svojim putem. Što je naroda ostalo, pođe za Šaulom u susret ratnicima. Kad su došli iz Gilgala u Gebu Benjaminovu, Šaul pobroji narod koji je ostao uza nj i bijaše ga oko šest stotina ljudi.
16 Sauli, mwanawe Yonathani na watu waliokuwa pamoja nao walikuwa wakiishi huko Gibea ya Benyamini, wakati Wafilisti wakiwa wamepiga kambi huko Mikmashi.
Šaul i sin mu Jonatan s ljudima što bijahu s njima zaposjeli su Benjaminovu Gebu, a Filistejci se utaborili u Mikmasu.
17 Makundi ya wavamiaji walikuja kutoka kambi ya Wafilisti katika vikosi vitatu. Kikosi kimoja kilielekea Ofra karibu na Shuali,
Tada iz filistejskog tabora izađe četa pljačkaša u tri odjela: jedan odio udari prema Ofri u zemlju šualsku;
18 kikosi kingine kilielekea Beth-Horoni, nacho kikosi cha tatu kilielekea kwenye nchi ya mpakani ielekeayo Bonde la Seboimu linalotazamana na jangwa.
drugi odio krenu prema Bet Horonu, a treći odio udari prema Gebi koja se uz Dolinu hijena diže nad pustinjom.
19 Hapakuwa na mhunzi ambaye angeweza kupatikana katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walikuwa wamesema, “Waebrania wasije wakatengeneza panga au mikuki!”
A po svoj zemlji Izraelovoj nije bilo kovača, jer su Filistejci rekli: “Treba sve učiniti da Hebreji ne bi pravili sebi mačeva i kopalja.”
20 Hivyo Waisraeli wote huteremka kwa Wafilisti ili kunoa majembe ya plau, majembe ya mkono, mashoka na miundu.
Zato su svi Izraelci išli k Filistejcima ako je tko htio da prekuje svoj raonik ili motiku, svoju sjekiru ili ostan za volove.
21 Bei ilikuwa fedha theluthi mbili za shekeli kunoa majembe ya plau na majembe ya mkono, na theluthi moja ya shekeli kwa nyuma, mashoka na michokoo.
A cijena je bila dvije trećine šekela za raonike i motike, jedna trećina za oštrenje sjekire i za nasađivanje ostana.
22 Kwa hiyo siku ya vita hakuna askari yeyote aliyekuwa kambini na Sauli na Yonathani ambaye alikuwa na upanga wala mkuki mkononi mwake; Sauli tu na mwanawe Yonathani ndio waliokuwa navyo.
Tako se dogodilo da na dan bitke kod Mikmasa nitko od svega naroda koji bijaše sa Šaulom i Jonatanom nije imao ni mača ni koplja u ruci; samo ih imahu Šaul i njegov sin Jonatan.
23 Basi kikosi cha Wafilisti kilikuwa kimetoka kuelekea njia iendayo Mikmashi.
A dotle jedna straža filistejska bijaše izišla prema klancu kod Mikmasa.

< 1 Samweli 13 >