< 1 Samweli 12 >

1 Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
Şamuelee İzrailybışde gırgıng'uk'le eyhen: – Haane, zı şu eyhençil k'ırı alixhxhı şos paççah gixhxhına.
2 Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
Həşde şoqa vuşda paççah vor, zımee q'əs qıxha, ç'ərbı cagvara qeetxha. Yizın dixbımee şoka vob. Zı cehilyranang'ançile g'iyniyne yiğılqamee vuşde ögee ark'ın.
3 Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
G'iyna zı vuşde ögil ulyorzuling'a, şu zak'le eyhelan, zı şavna yatsne, əməlene alyapt'ı? Vuşune zı horç'un? Vuşuyiy zı azırda hı'ı? Şavuke pıl alyaat'uye, mang'une pisde işilqa ul gyapxı? Rəbbineyiy Mangv'ee g'əyxı'ne paççahne ögee, yizde aq'veeqa aqqe. Zı şoke alyat'uyn sak'al ha'as.
4 Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
Manbışe mang'us inəxüd alidghıniy qele: – Ğu şi mısacab hopç'un deş, azırbab g'alyav'uynbı deş, şavnecad xılençe vuççudud g'ayşuyn deş.
5 Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
Şamuelee manbışik'le eyhen: – Şok'le g'iyna yizde aq'vee aqqasın vuççud ivdeeke ıxhay, Rəbbik'led, Mang'vee g'əyxı'yne paççahık'led g'acuyn. Manbışed «Ho'o, şaqa yiğne aq'vee aqqasın kar deşinva» eyhe.
6 Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
Şamueleecad meed milletık'le eyhen: – Mane Rəbbee Haruniy Mısa g'əvxü, vuşun dekkarıb Misirğançe Mang'veecab qığav'u.
7 Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
Həşde Rəbbine ögil ulyoozre. Zı şok'le Rəbbee şosiy vuşde dekkaaşis hav'una yugvalla eyhes, mana vuşde aq'val avqas.
8 “Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
Yaaq'ub Misireeqa qarayle. Qiyğa mang'uke g'abıynbışilqa Misirbışe yiğbı examee, manbışe Rəbbilqa xıleppı aaqa. Rəbbeeyib, Haruniy Mısa vuşun dekkar Misirğançe qığav'u, inyaqa qavaalesva g'uxoole.
9 “Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
Manbışemee Rəbb, cona Allah, yik'el hixan ha'a. Rəbbeeyib manbı Xatsorne g'oşunne xərıng'une Sisrayne, Moavne paççahne sayib Filiştinaaşde xılyaqa qoole. Manbışe vuşde dekkaaşika dəv'ə haa'a.
10 Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
Manke milletın gyaaşe-gyaaşe Rəbbilqa xıleppı aaqı, eyhen: «Rəbb, şi Ğu yik'el hixan hı'ı, Ba'aliy Aştoret donane byuttyaaşis ı'bəədat hı'ı, bınah hav'u. Ğu şi həşde duşmanaaşine xılençe g'attivxhan hav'uynxhiy, şi Vas ı'bəədat ha'ayiy».
11 Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
Rəbbeeyib manke Yerubba'al, Bedan, İftah, Şamuel g'uxoole. Şu nişilecab qı'məəq'ənceva Mang'vee şu məxüb hiqiy-allane duşmanaaşine xılençe g'attivxhan haa'a.
12 “Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
Şok'le Ammonbışda paççah, Naxaş, şolqa ı'qqə g'acumee, vuşda paççah Rəbb Allah ıxhayka, şu ilydyaakkı, zak'le uvhuyn: «De'eş, şaqa yişda paççah ıxha ıkkan».
13 Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
Haane şos ıkkiykın, şu g'əyxı'na paççah. İlyaake Rəbbee şos paççah gixhxhına.
14 Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
Rəbbile qəpq'ı'n Mang'us ı'bəədat he'eene, Mang'vee eyhençil k'ırıbı alixhxhı, Mang'une əmrbışeençe qığdepç'eene, şunab şol oğa gixhxhına paççahır vuşde Allahee, Rəbbee, eyhençika gyuv'ur oza qeepxheene, geed yugda ixhes!
15 Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
De'eş, şu Rəbbine cuvabıl k'ırı ilydiyxhı, Rəbbine əmreençe qığeepç'eene, nəxdiy Rəbbin xıl vuşde dekkaaşilqa satk'ıl, həməxdıd şolqad sak'alas.
16 “Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
Həşdemee ulyobzur, Rəbbee vuşde ulene ögil haa'asde xənne işiqa ilyaake!
17 Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
G'iyna suk qiviyşalan yiğ dişde vod? Zı həşde Rəbbilqa xıleppı aaqı, Mang'uk'le xəybı g'əhətqe'eva, gyoğiy g'axıleva eyhes. Manke şok'lecad ats'axhxhesın, şos paççah heqqıyka, şu Rəbbine ögil nimeena bınahiy hav'uva.
18 Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
Şamuelee Rəbbilqa ona'a, Rəbbeyid manecad yiğıl xəybı g'əhətqı'ı, gyoğiy gyoğa'a. Manke millet Rəbbiled, Şamueliled qətqı'niyn.
19 Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
Milletıncad Şamuelik'le eyhen: – Yişdemee, yiğne g'ulaaşinemee, yiğne Allahılqa, Rəbbilqa, düə hee'e, Mang'vee şi gimabat'acen. Şi yişde manisa bınahbışilqa, paççah heqqıyka sayıb hexxav'una.
20 Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
Şamuelemee milletık'le eyhen: – Qı'məəq'ən, şu mana bınah hav'u vuxheeyib, Rəbbile sivmiyk'al, Rəbbis ı'bəədat yik'eençe he'e.
21 Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
Nişiscad karaı'dəəne byutyaaşinemee, Rəbbile sivmiyk'al. Manbı nişiscad karaı'dəən karbı ıxhayke, mançisse şos nəxbınacab yugvallab haa'as vəəxəs deş, nişikecabıb g'attivxhan haa'as deş.
22 Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
Rəbbee Cune xənne doyunemee, şu dağaa'as deş. Rəbbis Cus ıkkiykın, şoke Cun millet hı'ı.
23 Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
Zalqa axvee, zı şol-alla düə hav'uy g'aleççes deş. Mançike zas Rəbbine ögil bınah vuxhes. Zı şos yugna, qopkuna yəq haagvas.
24 Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
Saccu Rəbbile qəvəq'ne, Mang'us gırgıne gahbışil yik'eençe ı'bəədat he'e. Yik'el aqqe, Rəbbee vuşdemee nəxdın ç'ak'ın işbı hı'ı ıxhay.
25 Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”
Şu pisvalybışike xıl ts'its'dyav'eene, şunab, vuşda paççahır ç'iyene aq'vayle havaakal haa'asınbı.

< 1 Samweli 12 >