< 1 Samweli 12 >
1 Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
Forsothe Samuel seide to al Israel, Lo! Y herde youre vois bi alle thingis whiche ye spaken to me, and Y ordeynede a kyng on you;
2 Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
and now the king goith bifor you. Sotheli Y wexide eld and hoor; forsothe my sones ben with you; therfor Y lyuyde bifor you fro my yong wexynge age `til to this dai. And lo!
3 Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
Y am redi; speke ye to me bifor the Lord, and bifor `the crist of hym; whether Y took `the oxe of ony man, ether the asse; if Y falsly chalengide ony mon; yf Y oppresside ony man; if Y took yifte of `the hond of ony man; and Y schal `dispise it to dai, and Y schal restore to you.
4 Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
And thei seiden, Thou hast not falsly chalengid vs, nether hast oppressid vs, nether hast take ony thing of `the hond of ony man.
5 Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
And he seide to hem, The Lord is witnesse ayens you, and his crist is witnesse in this day; for ye han not founde ony thing in myn hond. And thei seiden, Witnesse.
6 Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
And Samuel seide to the puple, The Lord, that made Moises and Aaron, and ledde youre fadris out of the lond of Egipt, is present;
7 Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
now therfor stonde ye, that Y stryue bi doom ayens you bifor the Lord, of alle the mercyes of the Lord, whiche he dide with you, and with youre fadris.
8 “Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
Hou Jacob entride in to Egipt, and youre fadris crieden to the Lord; and the Lord sente Moises and Aaron, and ledde youre fadris out of Egipt, and settide hem in this place.
9 “Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
Whiche foryaten her Lord God; and he bitook hem in the hond of Sisara, maystir of the chyualrie of Asor, and in the hond of Filisteis, and in the hond of the kyng of Moab; and thei fouyten ayens hem.
10 Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
Sotheli afterward thei crieden to the Lord, and seiden, We synneden, for we forsoken the Lord, and seruyden Baalym and Astroth; now therfor delyuere thou vs fro `the hond of oure enemyes, and we schulen serue thee.
11 Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
And the Lord sente Gerobaal, and `Bedan, that is, Sampson, and Barach, and Jepte, and Samuel, and delyuerede you fro the hond of youre enemyes bi cumpass; and ye dwelliden tristili.
12 “Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
Forsothe ye sien, that Naas, kyng of the sones of Amon, cam ayens you; and ye seiden to me, counseilynge to axe noon other kyng than God, Nay, but a kyng schal comaunde to vs; whanne `youre Lord God regnede in you.
13 Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
Now therfor youre kyng is redi, whom ye han chose and axid; lo! the Lord yaf to you a kyng.
14 Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
If ye dreden the Lord, and seruen hym, and heren his vois, and wraththen not the `mouth of the Lord; ye and youre kyng, that comaundith to you, schulen sue youre Lord God.
15 Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
Forsothe if ye heren not the vois of `the Lord, but wraththen his word, the hond of the Lord schal be on you, and on youre fadris.
16 “Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
But also now stonde ye, and se this gret thing which the Lord schal make in youre siyt.
17 Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
Whether heruest of whete is not `to dai? I schal inwardli clepe the Lord, and he schal yyue voices, `that is, thundris, and reynes; and ye schulen wite, and schulen se, for ye axynge a kyng on you han do greuouse yuel to you in the siyt of the Lord.
18 Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
And Samuel criede to the Lord, and the Lord yaf voices and reynes in that dai.
19 Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
And al the puple dredde greetli the Lord and Samuel; and al the puple seide to Samuel, Preye thou for thi seruauntis to thi Lord God, that we die not; for we addiden yuel to alle oure synnes, that we axiden a kyng to vs.
20 Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
Forsothe Samuel seide to the puple, `Nyle ye drede; ye han do al this yuel; netheles `nyle ye go awey fro the bak of the Lord, but serue ye the Lord in al youre herte;
21 Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
and nyle ye bowe aftir veyn thingis, that schulen not profite to you, nether schulen delyuere you; for tho ben veyn thingis.
22 Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
And the Lord schal not forsake his puple for his grete name; for the Lord swoor to make you a puple to hym silf.
23 Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
Forsothe this synne be fer fro me in the Lord, that Y ceesse to preye for you; and Y schal teche you a riytful weie and good.
24 Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
Therfor drede ye the Lord, and `serue ye hym in treuthe, and of al youre herte; for ye sien tho grete thingis, whiche he `dide in you;
25 Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”
that if ye contynuen in malice, bothe ye and youre kyng schulen perische to gidere.