< 1 Samweli 12 >
1 Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
Then Samuel said this to all the Israeli people: “I have done everything that you told me to do, and I have given/appointed a king to rule you.
2 Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
My own sons [are grown up and] with you now, but I have appointed Saul [instead of one of them], and he is now your leader. I am now old, and my hair is gray. I have been your leader ever since I was a boy.
3 Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
Now tell me, while Yahweh is listening, and while the king whom he has chosen is listening: whose ox or donkey have I stolen [during all those years]? Whom have I cheated? Whom have I oppressed/treated badly? From whom have I accepted a bribe, in order that I would ignore [the evil things he had done]? If I have done any of those things, tell me, and I will pay back what I owe.”
4 Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
They replied, “[No, ] you have never cheated anyone or oppressed anyone or accepted a bribe from anyone.”
5 Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
Then Samuel said, “Today Yahweh can testify, and the king whom you chose can testify, that I have not taken a bribe from anyone.” They replied, “Yes, Yahweh can say that he knows that is true.”
6 Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
Samuel continued by saying, “Yahweh is the one who appointed Moses and Aaron [to lead] our ancestors. He is the one who brought them out of Egypt. [And he is the one who will testify that what I am saying is true].
7 Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
Now while Yahweh is listening, stand here quietly while I accuse you [and tell you that your requesting a king instead of trusting Yahweh to lead you was wrong]. I will do that by reminding you of all the great miracles that Yahweh performed for you and your ancestors.
8 “Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
[“Many years] after Jacob went to Egypt, our ancestors pleaded to Yahweh to help them. So Yahweh sent Moses and Aaron to them, and they led our ancestors out of Egypt, and eventually they settled in this land.
9 “Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
“But our ancestors soon forgot about Yahweh, their God. So he allowed Sisera, the commander of the army from Hazor, to defeat them. He also allowed the Philistines and the army of the king of Moab to fight our ancestors and defeat them.
10 Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
Then our ancestors pleaded with Yahweh again to help them. They admitted, ‘Yahweh, we have sinned, and we have forsaken you. We have worshiped [idols that represent the god] Baal and [the goddess] Astarte. But if you rescue us from our enemies, we will worship you only.’
11 Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
So Yahweh sent men such as Gideon, Barak, Jephthah, and me to save you. And as a result, you did not have to worry about any enemies attacking you.
12 “Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
“But now, when king Nahash of Ammon came [with his army] to attack you, [you were afraid. So], you [came to me, and] said, ‘We want a king to rule us,’ even though Yahweh was already your king!
13 Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
So now, look, here is the king whom you have chosen. You asked for a king, and Yahweh has now appointed a king for you.
14 Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
If you will revere Yahweh and if you serve him, and if you listen to what he says and obey what he commands, and if you and the king who rules over you do what Yahweh your God wants you to do, [(things will go well for you all/Yahweh will bless you)].
15 Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
But if you do not listen to what Yahweh says, if you disobey what he commands, then he will punish [MTY] you all, just as he punished our ancestors.
16 “Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
“Now stand here quietly and see the great thing that Yahweh is about to do.
17 Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
You know that [RHQ] [it does not rain at this time of the year], during the time when you harvest wheat. But I will ask Yahweh to send thunder [and lightning] and rain today. When he does that, you will realize that Yahweh considers that you have done a very wicked thing by requesting a king.”
18 Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
Then Samuel prayed to Yahweh, and Yahweh caused it to thunder [and lightning] and rain. So all the people became very afraid of Yahweh and of Samuel.
19 Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
They cried out to Samuel, “Pray for us! We have added to our previous sins by requesting a king! Pray to Yahweh, your God, in order that we will not die [because of having done that]!”
20 Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
Samuel replied, “Do not be afraid! You have done this evil thing, but do not turn away from doing the things that Yahweh wants you to do. Instead, serve Yahweh wholeheartedly.
21 Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
Do not abandon [Yahweh] and worship useless idols. They cannot help you or save you [from your enemies], because they are truly useless.
22 Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
Yahweh decided to make us his people. So he will not abandon us people whom he has chosen, because he would injure his own reputation [of being completely faithful] if he did that.
23 Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
But as for me, I have solemnly promised that I will not sin against Yahweh by ceasing to pray for you. And I will continue to teach you what things are good and right [for you to do].
24 Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
But you must revere Yahweh and serve him wholeheartedly. Never forget all the great things that he has done for you.
25 Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”
But if you keep doing wicked things, he will get rid of you and your king!”