< 1 Samweli 11 >
1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
Tada doðe Nas Amonac, i stade u oko prema Javisu Galadovu. I svi ljudi iz Javisa rekoše Nasu: uèini vjeru s nama, pa æemo ti služiti.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
A Nas Amonac odgovori im: ovako æu uèiniti vjeru s vama: da vam svakome iskopam desno oko, i tu sramotu uèinim svemu Izrailju.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
A starješine Javiske rekoše mu: ostavi nam sedam dana, da pošljemo poslanike u sve krajeve Izrailjeve; pa ako ne bude nikoga da nas izbavi, tada æemo izaæi k tebi.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
I doðoše poslanici u Gavaju Saulovu, i kazaše ove rijeèi narodu; tada sav narod podiže glas svoj, i plakahu.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
A gle, Saul iðaše za govedima svojim iz polja, i reèe: šta je narodu te plaèe? I kazaše mu šta su poruèili Javišani.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
Tada siðe duh Božji na Saula kad èu te rijeèi, i on se razgnjevi vrlo.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
Pa uze dva vola, i isijeèe ih na komade, i razasla ih u sve krajeve Izrailjeve po istijem poslanicima poruèivši: ko ne poðe za Saulom i za Samuilom, ovako æe biti s govedima njegovijem. I strah Gospodnji popade narod, te izidoše jednodušno.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
I izbroji ih u Vezeku, i bješe sinova Izrailjevijeh trista tisuæa, a sinova Judinijeh trideset tisuæa.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
Potom rekoše poslanicima koji bijahu došli: ovako recite ljudima u Javisu Galadovu: sjutra æete se izbaviti, kad ogrije sunce. I poslanici se vratiše, i javiše ovo Javišanima, i oni se obradovaše.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
I rekoše Javišani Amoncima: sjutra æemo izaæi k vama, da uèinite od nas što vam bude drago.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
I sjutradan razdijeli Saul narod u tri èete, i uðoše usred okola o jutrenjoj straži, i biše Amonce dokle sunce ne ogrija, i koji ostaše, raspršaše se da ne ostaše ni dvojica zajedno.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
Tada reèe narod Samuilu: koji je ono što reèe: eda li æe Saul carovati nad nama? dajte ih da ih pogubimo.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
Ali Saul reèe: da se ne pogubi danas niko, jer je danas Gospod uèinio spasenje u Izrailju.
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
Tad Samuilo reèe narodu: hajdete da idemo u Galgal, da ondje ponovimo carstvo.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
I sav narod otide u Galgal, i postaviše ondje Saula carem pred Gospodom u Galgalu, i ondje prinesoše žrtve zahvalne pred Gospodom. I proveseli se ondje Saul i sav Izrailj veoma.