< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
Nionjoñe mb’eo amy zao t’i Nakase nte-Amone, nitobe am-piatrefañe Iabese-Gilade eo: le nanao ty hoe amy Nakase iaby o nte-Iabeseo: Mifañinà ama’ay vaho hitoroña’ay.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
Le hoe t’i Nakase nte-Amone am’ iereo: Inao arè ty fepètse hanoeko ama’ areo, te songa hakatrake o fihaino’ areo ankavanao ho fañinjeañe am’ Israele iaby.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
Le hoe o mpiaolo’ Iabeseo ama’e: Toloro fito androm-panintsiñan-jahay hañitrifa’ay mb’an-tane’ Israele iaby; ie amy zay naho tsy eo ty handrombak’ anay le hiakatse mb’ama’o mb’eo.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
Nivotrake e Gibàn-tSaole ao o ìrakeo le nisaontsie’e an-dravembia’ondatio i entañe zay vaho fonga nipoñake ty rovetse ondatio.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
Nañorike mpirai-troke boak’ an-tetek’ ao t’i Saole, le hoe t’i Saole: Ino ty mañore ondatio t’ie mirovetse? Aa le nitalilia’ iareo ty saon­tsi’ o nte-Iabeseo.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
Ie nahajanjiñe i entañe zay t’i Saole le nentoe’ ty Arofon’ Añahare, vaho nisolebotse ty haviñera’e.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
Rinambe’e i katràka mpirai-joka rey, le linili-lili’e, naho nahitri’e mb’an-tane’ Israele mb’eo mb’eo am-pitàn’ ìrake, ami’ty hoe: Ze tsy mionjoñe mb’eo am-panonjohizañe i Saole naho am-pañorihañe i Samoele, le zao ka ty hanoañe o katràka’eo. Aa le nife­tsak’ am’ondatio ty fañeveñañe am’ Iehovà, vaho niakatse mb’eo hoe ondaty raike.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
Niahe’e e Betseke ao: telo hetse ty ana’ Israele vaho telo-ale o nte-Iehodao.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
Aa le hoe ty asa’ iareo amo ìrake nivotrakeo: Zao ty ho enta’ areo amo nte-Iabese-giladeo: hamaray aolo’ ty mafana-voho t’ie hitendreke rombake. Nibalike naho nitalily amo nte-Iabeseo o irakeo le niehake,
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
vaho hoe o nte-Iabeseo: Hamaray ty hiakara’ay mb’ ama’ areo vaho hanoe’ areo ama’ay ze satrin’ arofo’ areo.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
Aa ie maraiñe, zinara’ i Saole an-dia-rai’e telo ondatio le nimoak’ an-tobe ao am-pijilovañe maraindraiñey vaho zinevo’ iereo o nte-Amoneo am-para’ te mafana-voho; niparaitake iaby ze nisisa kanao tsy nahaisahañe roe miharo lia.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
Le hoe ondatio amy Samoele; Ia o nivolañe ty hoe: Hahafehe antika hao t’i Saoleo? Aseseo mb’atoa indaty rezay hañohofan-doza.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
Fe hoe t’i Saole: Leo raik’ am’ondatio tsy havetrake te anito, fa nanao fandrombahañe e Israele ao t’Iehovà anindroany.
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
Le hoe t’i Samoele am’ondatio, Antao homb’ e Gilgale mb’eo hamentesan-tika ty fifeheañe.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
Aa le niheo mb’e Gilgale mb’eo ondaty iabio naho nanoe’ iereo mpanjaka añatrefa’ Iehovà e Gilgale t’i Saole; le nisoroñe engam-panintsi­ñañe añatrefa’ Iehovà; vaho nandia taroba t’i Saole naho o ana’ Israele iabio.

< 1 Samweli 11 >