< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
Et il arriva environ un mois après que Naas, roi des Ammonites, monta et commença à combattre contre Jabès-Galaad. Et tous les hommes de Jabès dirent à Naas: Acceptez-nous comme alliés, et nous vous servirons.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
Et Naas, l’Ammonite, leur répondit: L’alliance que je ferai avec vous, sera que je vous arracherai à tous l’œil droit et que je vous rendrai l’opprobre de tout Israël.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
Et les anciens de Jabès lui répliquèrent: Accordez-nous sept jours, afin que nous envoyions des messagers dans tous les confins d’Israël, et s’il n’y a personne pour nous défendre, nous viendrons à vous.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
Les messagers vinrent donc à Gabaa, patrie de Saül, et rapportèrent ces paroles, le peuple l’entendant; alors tout le peuple éleva sa voix, et pleura.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
Et voilà que Saul venait de la campagne, suivant les bœufs, et il dit: Qu’a le peuple, qu’il pleure? Et on lui raconta les paroles des hommes de Jabès.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
Or, l’esprit du Seigneur se saisit de Saül, lorsqu’il eut entendu ces paroles, et sa fureur fut très irritée.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
Et prenant l’un et l’autre bœufs, il les coupa en morceaux, et les envoya dans tous les confins d’Israël par la main des messagers, disant: Quiconque ne sortira pas et ne suivra pas Saül et Samuel, c’est ainsi qu’il sera fait à ses bœufs. Ainsi la crainte du Seigneur saisit le peuple, et ils sortirent comme un seul homme.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
Et Saül en fit la revue à Bézech, et il y eut trois cent mille enfants d’Israël; mais des hommes de Juda, trente mille.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
Et ils dirent aux messagers qui étaient venus: C’est ainsi que vous direz aux hommes qui sont à Jabès-Galaad: Demain, le salut sera pour vous, lorsque le soleil sera devenu chaud. Les messagers vinrent donc, et apportèrent cette nouvelle aux hommes de Jabès, qui se livrèrent à la joie.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
Et ils dirent: Demain nous nous donnerons à vous, et vous nous ferez tout ce qui vous plaira.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
Or, il arriva, que lorsque le lendemain fut venu, Saül partagea le peuple en trois parties; et il entra au milieu du camp pendant la veille du matin, et il battit Ammon, jusqu’à ce que le soleil fût devenu chaud. Ceux qui échappèrent furent dispersés, de manière qu’il n’en resta pas deux ensemble.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
Alors le peuple dit à Samuel: Quel est celui qui a dit: Est-ce que Saul régnera sur nous? Donnez-nous ces hommes, et nous les tuerons.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
Et Saül répondit: Personne ne sera mis à mort en ce jour, parce que le Seigneur a accordé aujourd’hui le salut dans Israël.
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
Mais Samuel dit au peuple: Venez, et allons à Galgala, et proclamons-y de nouveau la royauté.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
Et tout le peuple alla à Galgala, et ils y firent Saul roi devant le Seigneur, à Galgala; et ils immolèrent là des victimes pacifiques devant le Seigneur. Et Saül se livra là, ainsi que tous les peuples d’Israël, à une joie très grande.

< 1 Samweli 11 >