< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
Or Nahas Hammonite monta, et se campa contre Jabés de Galaad. Et tous ceux de Jabés dirent à Nahas: Traite alliance avec nous, et nous te servirons.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
Mais Nahas Hammonite leur répondit: Je traiterai [alliance] avec vous à cette condition, que je vous crève à tous l'œil droit, et que je mette cela pour opprobre sur tout Israël.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
Et les Anciens de Jabés lui dirent: Donne-nous sept jours de trêve, et nous enverrons des messagers par tous les quartiers d'Israël, et s'il n'y a personne qui nous délivre, nous nous rendrons à toi.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
Les messagers donc vinrent en Guib-ha-Saül, et dirent ces paroles devant le peuple; et tout le peuple éleva sa voix, et pleura.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
Et voici Saül revenait des champs derrière ses bœufs; et il dit: Qu'est-ce qu'a ce peuple pour pleurer ainsi? Et on lui récita ce qu'avaient dit ceux de Jabés.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
Or l'Esprit de Dieu saisit Saül, lorsqu'il entendit ces paroles, et il fut embrasé de colère.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
Et il prit une couple de bœufs, et les coupa en morceaux, et en envoya dans tous les quartiers d'Israël par des messagers exprès, en disant: On en fera de même aux bœufs de tous ceux qui ne sortiront point, et qui ne suivront point Saül et Samuel. Et la frayeur de l'Eternel tomba sur le peuple, et ils sortirent comme si ce n'eût été qu'un seul homme.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
Et [Saül] les dénombra en Bézec; et il y eut trois cent mille hommes des enfants d'Israël, et trente mille des gens de Juda.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
Après ils dirent aux messagers qui étaient venus: Vous parlerez ainsi à ceux de Jabés de Galaad: Vous serez délivrés demain quand le soleil sera en sa force. Les messagers donc s'en revinrent, et rapportèrent cela à ceux de Jabés, qui [s'en] réjouirent.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
Et ceux de Jabés dirent [aux Hammonites]: Demain nous nous rendrons à vous, et vous nous ferez tout ce qui vous semblera bon.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
Et dès le lendemain Saül mit le peuple en trois bandes, et ils entrèrent dans le camp sur la veille du matin, et ils frappèrent les Hammonites jusques vers la chaleur du jour; et ceux qui demeurèrent de reste furent tellement dispersés çà et là, qu'il n'en demeura pas deux ensemble.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
Et le peuple dit à Samuel: Qui est-ce qui dit: Saül régnera-t-il sur nous? Donnez-nous ces hommes-là, et nous les ferons mourir.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
Alors Saül dit: On ne fera mourir personne en ce jour, parce que l'Eternel a délivré aujourd'hui Israël.
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
Et Samuel dit au peuple: Venez, et allons à Guilgal, et nous y renouvellerons la Royauté.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
Et tout le peuple s'en alla à Guilgal; et là ils établirent Saül pour Roi devant l'Eternel à Guilgal, et ils offrirent là des sacrifices de prospérité devant l'Eternel; et là, Saül et tous ceux d'Israël se réjouirent beaucoup.

< 1 Samweli 11 >