< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
And it was don as aftir a monethe, Naas of Amon stiede, and bigan to fiyte ayens Jabes of Galaad. And alle the men of Jabes seiden to Naas, Haue thou vs boundun in pees, and we schulen serue thee.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
And Naas of Amon answeride to hem, In this Y schal smyte boond of pees with you, that Y putte out the riyt iyen of alle you, and that Y sette you schenschip in al Israel.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
And the eldere men of Jabes seiden to him, Graunte thou to vs seuene daies, that we senden messangeris to alle the termes of Israel; and if noon be that defende vs, we schulen go out to thee.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
Therfor messangeris camen in to Gabaad of Saul, and spaken these wordis, `while the puple herde; and al the puple reiside her vois, and wepte.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
And lo! Saul cam, `and suede oxis fro the feeld; and he seide, What hath the puple, for it wepith? And thei telden to hym the wordis of men of Jabes.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
And the Spirit of the Lord skippide in to Saul, whanne he hadde herd these wordis, and his woodnesse was `wrooth greetli.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
And he took euer either oxe, and kittide in to gobetis, and sente in to alle the termes of Israel, bi the hondis of messangeris; and seide, Who euer goith not out, and sueth not Saul and Samuel, so it schal be don to hise oxun. Therfor the drede of the Lord asailide the puple, and thei yeden out as o man.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
And he noumbride hem in Besech; and thre hundrid thousynd weren of the sones of Israel; forsothe of the men of Juda weren thretti thousynde.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
And thei seiden to the messangeris that camen, Thus ye schulen seie to the men that ben in Jabes of Galaad, To morew schal be helthe to you, whanne the sunne is hoot. Therfor the messangeris camen, and telden to the men of Jabes; whiche weren glad,
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
and seiden, Eerli we schulen go out to you, and ye schulen do to vs al that plesith you.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
And it was don, whanne the morewe dai cam, Saul ordeynede the puple in to thre partis; and he entride in to the myddil tentis `in the wakyng of the morewtid, and he smoot Amon til the dai `was hoot; `forsothe the residues weren scaterid, so that tweyne togidere weren not left in hem.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
And the puple seide to Samuel, Who is this, that seide, Saul schal not regne on vs? Yyue ye the men, and we schulen sle hem.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
And Saul seide, No man schal be slayn in this dai, for to dai the Lord made helthe in Israel.
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
Forsothe Samuel seide to the puple, Come ye, and go we in to Galgala, and renule we there the rewme.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
And al the puple yede in to Galgala, and there thei maden Saul kyng bifor the Lord `in Galgala; and thei offriden pesible sacrifices bifor the Lord. And Saul was glad there, and alle the men of Israel greetli.

< 1 Samweli 11 >