< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
Then came up Nachash the 'Ammonite, and encamped against Yabesh-gil'ad: and all the men of Yabesh said unto Nachash, Make a covenant with us, and we will serve thee.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
And Nachash the 'Ammonite said unto them, On this condition will I make it with you, that ye all have put out the right eye, that I may lay it as a reproach upon all Israel.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
And the elders of Yabesh said unto him, Grant us seven days' respite, that we may send messengers throughout all the boundary of Israel; and then, if there be none to save us, will we come out to thee.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
And the messengers came to Gib'ah of Saul, and spoke the words in the ears of the people; and all the people lifted up their voice, and wept.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
And, behold, Saul was coming after the herds out of the field; and Saul said, What aileth the people that they weep? And they told him the words of the men of Yabesh.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
And the spirit of God came suddenly over Saul when he heard these words, and his anger was kindled greatly,
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
And he took a yoke of oxen, and cut them in pieces, and sent them about throughout all the boundary of Israel by the hand of the messengers, saying, Whosoever goeth not forth after Saul and after Samuel, shall have his herds thus treated. And the dread of the Lord fell on the people, and they went out as one man.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
And he numbered them in Bezek; and the children of Israel were three hundred thousand, and the men of Judah thirty thousand.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
And they said unto the messengers that were come, Thus shall ye say unto the men of Yabesh-gil'ad, Tomorrow shall ye have help, when the sun shineth hot. And the messengers came and told it to the men of Yabesh; and these were glad.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
And the men of Yabesh said, Tomorrow will we go out unto you, and ye can do unto us in accordance with all that seemeth good in your eyes.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
And it happened on the morrow, that Saul put the people in three companies; and they came into the midst of the camp in the morning watch, and they smote the 'Ammonites until the heat of the day: and it came to pass, that those that remained were scattered, and no two among them were left together.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
And the people said unto Samuel, Who is there that saith, Shall Saul reign over us? give up the men, and we will put them to death.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
And Saul said, There shall not a man be put to death on this day; for today the Lord hath wrought deliverance in Israel.
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
And Samuel said to the people, Come and let us go to Gilgal, and renew there the choice of the king.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
And all the people went to Gilgal; and they appointed there Saul as king before the Lord in Gilgal; and they sacrificed there sacrifices of peace-offerings before the Lord; and Saul with all the men of Israel rejoiced there very greatly.

< 1 Samweli 11 >