< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
And it came to pass about a month after this that Naas, the Ammonite came up, and began to fight against Jabes Galaad. And all the men of Jabes said to Naas: Make a covenant with us, and we will serve thee.
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
And Naas the Ammonite answered them: On this condition will I make a covenant with you, that I may pluck out all your right eyes, and make you a reproach in all Israel.
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
And the ancients of Jabes said to him: Allow us seven days, that we may send messengers to all the coasts of Israel: and if there be no one to defend us, we will come out to thee.
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
The messengers therefore came to Gabaa of Saul: and they spoke these words in the hearing of the people: and all the people lifted up their voices, and wept.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
And behold Saul came, following oxen out of the field, and he said: What aileth the people that they weep? And they told him the words of the men of Jabes.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
And the spirit of the Lord came upon Saul, when he had heard these words, and his anger was exceedingly kindled.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
And taking both the oxen, he cut them in pieces, and sent them into all the coasts of Israel by messengers, saying: Whosoever shall not come forth, and follow Saul and Samuel, so shall it be done to his oxen. And the fear of the Lord fell upon the people, and they went out as one man.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
And he numbered them in Bezec: and there were of the children of Israel three hundred thousand: and of the men of Juda thirty thousand.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
And they said to the messengers that came: Thus shall you say to the men of Jabes Galaad: Tomorrow, when the sun shall be hot, you shall have relief. The messengers therefore came, and told the men of Jabes: and they were glad.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
And they said: In the morning we will come out to you: and you shall do what you please with us.
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
And it came to pass, when the morrow was come that Saul put the people in three companies: and he came into the midst of the camp in the morning watch, and he slew the Ammonites until the day grew hot, and the rest were scattered, so that two of them were not left together.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
And the people said to Samuel: Who is he that said: Shall Saul reign over us? Bring the men and we will kill them.
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
And Saul said: No man shall be killed this day, because the Lord this day hath wrought salvation in Israel:
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
And Samuel said to the people: Come and let us go to Galgal, and let us renew the kingdom there.
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
And all the people went to Galgal, and there they made Saul king before the Lord in Galgal, and they sacrificed there victims of peace before the Lord. And there Saul and all the men of Israel rejoiced exceedingly.

< 1 Samweli 11 >