< 1 Samweli 11 >

1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
And, about a month afterward, it happened that Nahash the Ammonite ascended and began to fight against Jabesh Gilead. And all the men of Jabesh said to Nahash, “Consider a pact with us, and we will serve you.”
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
And Nahash the Ammonite responded to them, “With this will I strike a pact with you: if I may pluck out all your right eyes, and set you as a disgrace against all of Israel.”
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
And the elders of Jabesh said to him: “Grant to us seven days, so that we may send messengers to all the borders of Israel. And if there is no one who may defend us, we will go out to you.”
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
Therefore, the messengers arrived at Gibeah of Saul. And they spoke these words in the hearing of the people. And all the people lifted up their voice and wept.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
And behold, Saul arrived, following oxen from the field. And he said, “What has happened to the people that they would weep?” And they explained to him the words of the men from Jabesh.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
And the Spirit of the Lord rose up within Saul when he had heard these words, and his fury was enraged exceedingly.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
And taking both the oxen, he cut them into pieces, and he sent them into all the borders of Israel, by the hands of messengers, saying, “Whoever will not go out and follow Saul and Samuel, so shall it be done to his oxen.” Therefore, the fear of the Lord entered into the people, and they went out like one man.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
And he took a census of them at Bezek. And there were three hundred thousand of the sons of Israel. And there were thirty thousand of the men of Judah.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
And they said to the messengers who had arrived: “So shall you say to the men who are of Jabesh Gilead: ‘Tomorrow, when the sun will be hot, you shall have salvation.’” Therefore, the messengers went and announced it to the men of Jabesh, who became joyful.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
And they said, “In the morning, we will go out to you. And you may do whatever you please with us.”
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
And it happened that, when the next day had arrived, Saul arranged the people into three parts. And he entered into the middle of the camp at the early morning watch, and he struck down the Ammonites until the day grew hot. Then the remainder were dispersed, so much so that not even two of them were left together.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
And the people said to Samuel: “Who is the one who said, ‘Should Saul reign over us?’ Present the men, and we will put them to death.”
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
And Saul said: “No one shall be killed on this day. For today the Lord has accomplished salvation in Israel.”
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
Then Samuel said to the people, “Come, and let us go to Gilgal, and let us renew the kingdom there.”
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
And all the people traveled to Gilgal. And there they made Saul king, in the sight of the Lord at Gilgal. And there they immolated victims of peace, before the Lord. And there Saul and all the men of Israel rejoiced exceedingly.

< 1 Samweli 11 >