< 1 Samweli 11 >
1 Nahashi yule Mwamoni, akakwea kuuzunguka kwa jeshi mji wa Yabeshi-Gileadi. Watu wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba na sisi, na tutakuwa chini yako.”
Siden efter drog Ammoniten Nahasj op og belejrede Jabesj i Gilead. Da sagde alle Mændene i Jabesj til Nahasj: »Slut Pagt med os, saa vil vi underkaste os!«
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitangʼoa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
Men Ammoniten Nahasj svarede: »Ja, paa det Vilkaar vil jeg slutte Pagt med eder, at jeg maa stikke det højre Øje ud paa enhver af eder til Forsmædelse for hele Israel!«
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote, kama hakuna hata mmoja anayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
Da sagde de Ældste i Jabesj til ham: »Giv os syv Dages Frist, saa vi kan sende Bud rundt i hele Israels Land; hvis saa ingen kommer os til Hjælp, vil vi overgive os til dig!«
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa juu ya masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
Da Sendebudene kom til Sauls Gibea og forebragte Folket Sagen, brast hele Folket i Graad.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza jinsi watu wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
Og se, Saul kom netop hjem med sine Okser fra Marken, og han spurgte: »Hvad er der i Vejen med Folket, siden det græder?« De fortalte ham da, hvad Mændene fra Jabesj havde sagt;
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
og da Saul hørte det, overvældede Guds Aand ham, og hans Vrede blussede heftigt op.
7 Akachukua jozi ya maksai na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha hofu ya Bwana ikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
Saa tog han et Spand Okser og sønderhuggede dem, sendte Folk ud med Stykkerne i hele Israels Land og lod sige: »Hvis nogen ikke følger Saul og Samuel, skal der handles saaledes med hans Okser!« Da faldt en HERRENS Rædsel over Folket, saa de alle som een drog ud.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa Yuda 30,000.
Og han mønstrede dem i Bezek, og der var 300 000 Israeliter og 30 000 Judæere.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni watu wa Yabeshi-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’” Wajumbe walipokwenda na kutoa taarifa hii kwa watu wa Yabeshi, wakafurahi.
Derpaa sagde han til Sendebudene, som var kommet: »Saaledes skal I sige til Mændene i Jabesj i Gilead: I Morgen, naar Solen begynder at brænde, skal I faa Hjælp!« Da Sendebudene kom og meddelte Mændene i Jabesj det, blev de glade.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
Og Mændene i Jabesj sagde: »I Morgen vil vi overgive os til eder, saa kan I gøre med os, hvad I finder for godt!«
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja mpaka mchana. Wale walionusurika wakasambaa, kiasi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
Dagen efter delte Saul Hæren i tre Afdelinger, og de trængte ind i Lejren ved Morgenvagten og huggede ned blandt Ammoniterne, til det blev hedt; og de, som undslap, splittedes til alle Sider, saa ikke to og to blev sammen.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatawala juu yetu?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
Da sagde Folket til Samuel: »Hvem var det, som sagde: Skal Saul være Konge over os? Bring os de Mænd, at vi kan slaa dem ihjel!«
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Bwana ameokoa Israeli.”
Men Saul sagde: »I Dag skal ingen slaas ihjel; thi i Dag har HERREN givet Israel Sejr!«
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
Da sagde Samuel til Folket: »Kom, lad os gaa til Gilgal og gentage Kongevalget der!«
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Bwana, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
Saa gik hele Folket til Gilgal og gjorde Saul til Konge for HERRENS Aasyn der i Gilgal, og de bragte Takofre der for HERRENS Aasyn. Og Saul og alle Israels Mænd var højlig glade.