< 1 Samweli 10 >

1 Ndipo Samweli akachukua chupa ndogo ya mafuta na kuyamimina juu ya kichwa cha Sauli, akambusu, akisema, “Je, Bwana hakukutia mafuta uwe kiongozi juu ya watu wake Israeli?
Samuel prit une fiole d'huile, et la versa sur la tête de Saül; puis il le baisa et dit: « Yahweh ne t'a-t-il pas oint pour chef sur son héritage?
2 Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na watu wawili karibu na kaburi la Raheli, huko Selsa kwenye mpaka wa Benyamini. Watakuambia, ‘Punda wale uliotoka kwenda kuwatafuta, wamekwisha kupatikana. Sasa baba yako ameacha kufikiri kuhusu punda na sasa ana hofu kukuhusu wewe. Anauliza, “Nitafanyaje kuhusu mwanangu?”’
Quand tu m'auras quitté aujourd'hui, tu trouveras deux hommes près du sépulcre de Rachel, dans le territoire de Benjamin, à Selsach; ils te diront: « Les ânesses que tu es allé chercher sont retrouvées; et voici, ton père a perdu de vue l'affaire des ânesses, mais il est en peine de vous et dit: Que dois-je faire au sujet de mon fils? »
3 “Kisha utakwenda mbele kutoka hapa mpaka uufikie mwaloni wa Tabori. Watu watatu wanaopanda kwa Mungu huko Betheli watakutana nawe hapo. Mmoja atakuwa amechukua wana-mbuzi watatu, mwingine mikate mitatu, na mwingine kiriba cha divai.
De là, poursuivant ta route, tu arriveras au chêne de Thabor, et là tu seras rencontré par trois hommes montant vers Dieu à Béthel, et portant l'un trois chevreaux, l'autre trois miches de pain, et l'autre une outre de vin.
4 Watakusalimu na kukupa mikate miwili, ambayo utaipokea kutoka kwao.
Après qu'ils t'auront salué, ils te donneront deux pains, et tu les recevras de leurs mains.
5 “Baada ya hayo utakwenda Gibea ya Mungu, ambapo hapo kuna kambi ya Wafilisti. Unapokaribia mji utakutana na kundi la manabii wakiteremka kutoka mahali pa juu wakiwa na vinubi, matari, filimbi na zeze vikipigwa mbele yao, nao watakuwa wakitoa unabii.
Après cela, tu viendras à Gabaa de Dieu, où se trouve un poste de Philistins. En entrant dans la ville, tu rencontreras une troupe de prophètes descendant du haut lieu, précédés de luths, tambourins, flûtes et harpes, et prophétisant.
6 Roho wa Bwana atakuja juu yako kwa nguvu, nawe utatoa unabii pamoja nao; nawe utageuzwa kuwa mtu wa tofauti.
L'Esprit de Yahweh te saisira, et tu prophétiseras avec eux, et tu seras changé en un autre homme.
7 Mara ishara hizi zitakapotimizwa, fanya lolote mkono wako upasao kufanya, kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.
Lorsque ces signes se seront accomplis pour toi, fais ce qui se présentera, car Dieu est avec toi.
8 “Tangulia kushuka mbele yangu mpaka Gilgali. Hakika nami nitateremka nikujie ili kutoa dhabihu za sadaka za kuteketezwa na dhabihu za amani, lakini lazima ungoje kwa siku saba hata nitakapokujia na kukuambia likupasalo kufanya.”
Et tu descendras avant moi à Galgala; et voici, je descendrai vers toi, pour offrir des holocaustes et des sacrifices pacifiques. Tu attendras sept jours jusqu'à ce que je sois venu vers toi et je te ferai connaître ce que tu dois faire. »
9 Ikawa Sauli alipogeuka kumwacha Samweli, Mungu aliubadilisha moyo wa Sauli, na ishara hizi zote zikatimizwa siku ile.
Dès que Saül eut tourné le dos pour se séparer de Samuel, Dieu lui donna un autre cœur, et tous ces signes s'accomplirent le même jour.
10 Walipofika Gibea, akakutana na kundi la manabii. Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akajiunga nao katika kutoa unabii kwao.
Quand ils arrivèrent à Gabaa, voici qu'une troupe de prophètes vint à sa rencontre; et l'Esprit de Dieu le saisit, et il prophétisa au milieu d'eux.
11 Ikawa wale wote waliomfahamu hapo mwanzo walipomwona akitoa unabii pamoja na manabii, wakaulizana, “Ni nini hiki kilichomtokea mwana wa Kishi? Je, Sauli naye pia yumo miongoni mwa manabii?”
Quand tous ceux qui le connaissaient auparavant virent qu'il prophétisait avec les prophètes, tous ces gens se dirent l'un à l'autre: « Qu'est-il arrivé au fils de Cis? Saül est-il donc aussi parmi les prophètes? »
12 Mtu mmoja ambaye aliishi huko akajibu, “Je, naye baba yao ni nani?” Basi ikawa mithali, kusema, “Je, Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?”
Quelqu'un de la foule prit la parole et dit: « Et qui est leur père? » — C'est pourquoi cela est passé en proverbe: « Saül est-il aussi parmi les prophètes? » —
13 Baada ya Sauli kumaliza kutoa unabii, alikwenda mahali pa juu.
Lorsqu'il eut cessé de prophétiser, il se rendit en haut lieu.
14 Basi babaye mdogo akamuuliza Sauli na mtumishi wake, “Je, mlikuwa wapi?” Akajibu, “Tulikuwa tukiwatafuta punda. Lakini tulipoona hawapatikani, tulikwenda kwa Samweli.”
L'oncle de Saül dit à Saül et à son serviteur: « Où êtes-vous allés? » Saül répondit: « Chercher les ânesses; mais ne les ayant vues nulle part, nous sommes allés vers Samuel. »
15 Babaye mdogo Sauli akasema, “Niambie Samweli amekuambia nini.”
L'oncle de Saül dit: « Raconte-moi ce que vous a dit Samuel. »
16 Sauli akajibu, “Alituhakikishia kwamba punda wamepatikana.” Lakini hakumwambia babaye mdogo kila kitu Samweli alichomwambia kuhusu ufalme.
Et Saül répondit à son oncle: « Il nous a appris que les ânesses étaient retrouvées. » Mais quant à l'affaire de la royauté, il ne lui rapporta pas ce qu'avait dit Samuel.
17 Samweli akawaita watu wa Israeli kuja kwa Bwana huko Mispa,
Samuel convoqua le peuple devant Yahweh à Maspha,
18 naye akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Niliwatoa Israeli kutoka Misri, nami niliwaokoa toka nguvu za Misri na falme zote zilizowaonea.’
et il dit aux enfants d'Israël: « Ainsi parle Yahweh, le Dieu d'Israël: J'ai fait monter Israël d'Egypte, et je vous ai délivrés de la main des Egyptiens et de la main de tous les royaumes qui vous opprimaient.
19 Lakini sasa mmemkataa Mungu wenu, ambaye anawaokoa toka katika maafa yenu yote na taabu zenu zote. Nanyi mmesema, ‘Hapana, tuteulie mfalme atutawale.’ Sasa basi, jihudhurisheni wenyewe mbele za Bwana kwa kabila zenu na kwa koo zenu.”
Et vous, aujourd'hui, vous rejetez votre Dieu, qui vous a délivrés de tous vos maux et de toutes vos souffrances, et vous lui dites: Etablis un roi sur nous! Présentez-vous maintenant devant Yahweh, selon vos tribus et selon vos familles. »
20 Samweli alipoyasogeza makabila yote ya Israeli, kabila la Benyamini likachaguliwa.
Samuel fit approcher toutes les tribus d'Israël, et la tribu de Benjamin fut désignée par le sort.
21 Kisha akalisogeza mbele kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo, nao ukoo wa Matri ukachaguliwa. Mwishoni Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa. Lakini walipomtafuta, hakuonekana.
Il fit approcher la tribu de Benjamin par familles, et la famille de Métri fut désignée; puis Saül, fis de Cis fut désigné. On le chercha, mais on ne le trouva point.
22 Wakazidi kuuliza kwa Bwana, “Je, huyo mtu amekwisha kufika hapa?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, amejificha katikati ya mizigo.”
Alors ils interrogèrent de nouveau Yahweh: « Est-il venu ici encore quelqu'un? » Yahweh répondit: « Voici, il est caché parmi les bagages. »
23 Wakakimbia na kumleta kutoka huko, naye aliposimama katikati ya watu, alikuwa mrefu kuliko watu wengine wote.
On courut le tirer de là, et il se tint au milieu du peuple, dépassant tout le peuple de l'épaule et au delà.
24 Samweli akawaambia watu wote, “Je, mnamwona mtu ambaye Bwana amemchagua? Hayupo aliye kama yeye miongoni mwa watu wote.” Ndipo watu wakapiga kelele, wakasema, “Mfalme na aishi maisha marefu.”
Et Samuel dit à tout le peuple: « Voyez-vous celui que Yahweh a choisi? Il n'y a personne dans tout le peuple qui soit semblable à lui. » Et tout le peuple poussa des cris en disant: « Vive le roi! »
25 Samweli akawaeleza watu madaraka ya ufalme. Akayaandika kwenye kitabu na kuweka mbele za Bwana. Kisha Samweli akawaruhusu watu, kila mmoja aende nyumbani kwake.
Alors Samuel exposa au peuple le droit de la royauté, et il l'écrivit dans le livre, qu'il déposa devant Yahweh; puis il renvoya tout le peuple, chacun dans sa maison.
26 Sauli pia akaenda nyumbani kwake huko Gibea, akisindikizwa na watu hodari ambao Mungu alikuwa amegusa mioyo yao.
Saül aussi s'en alla dans sa maison à Gabaa, accompagné d'hommes de valeur, dont Dieu avait touché le cœur.
27 Lakini baadhi ya watu wakorofi walisema, “Huyu mtu atawezaje kutuokoa?” Wakamdharau na wala hawakumletea zawadi. Lakini Sauli akanyamaza kimya.
Toutefois les hommes de Bélial disaient: « Est-ce celui-là qui nous sauvera? » Et ils le méprisèrent et ne lui apportèrent pas de présents. Mais Saül n'y prit point garde.

< 1 Samweli 10 >