< 1 Samweli 10 >

1 Ndipo Samweli akachukua chupa ndogo ya mafuta na kuyamimina juu ya kichwa cha Sauli, akambusu, akisema, “Je, Bwana hakukutia mafuta uwe kiongozi juu ya watu wake Israeli?
Then Samuel took a little vial of oil, and poured it on his head. And he kissed him, and said: “Behold, the Lord has anointed you as first ruler over his inheritance. And you shall free his people from the hands of their enemies, who are all around them. And this shall be a sign for you that God has anointed you as ruler:
2 Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na watu wawili karibu na kaburi la Raheli, huko Selsa kwenye mpaka wa Benyamini. Watakuambia, ‘Punda wale uliotoka kwenda kuwatafuta, wamekwisha kupatikana. Sasa baba yako ameacha kufikiri kuhusu punda na sasa ana hofu kukuhusu wewe. Anauliza, “Nitafanyaje kuhusu mwanangu?”’
When you will have departed from me this day, you will find two men beside the sepulcher of Rachel, in the parts of Benjamin to the south. And they will say to you: ‘The donkeys have been found, which you had been seeking as you traveled. And your father, forgetting about the donkeys, has been anxious for you, and he says, “What shall I do about my son?”’
3 “Kisha utakwenda mbele kutoka hapa mpaka uufikie mwaloni wa Tabori. Watu watatu wanaopanda kwa Mungu huko Betheli watakutana nawe hapo. Mmoja atakuwa amechukua wana-mbuzi watatu, mwingine mikate mitatu, na mwingine kiriba cha divai.
And when you will have departed from there, and will have traveled farther, and will have arrived at the oak of Tabor, in that place three men, who are going up to God at Bethel, will find you. One will be bringing three young goats, and another three loaves of bread, and another will be carrying a bottle of wine.
4 Watakusalimu na kukupa mikate miwili, ambayo utaipokea kutoka kwao.
And when they will have greeted you, they will give you two loaves. And you shall accept these from their hand.
5 “Baada ya hayo utakwenda Gibea ya Mungu, ambapo hapo kuna kambi ya Wafilisti. Unapokaribia mji utakutana na kundi la manabii wakiteremka kutoka mahali pa juu wakiwa na vinubi, matari, filimbi na zeze vikipigwa mbele yao, nao watakuwa wakitoa unabii.
After these things, you shall arrive at the hill of God, where the garrison of the Philistines is. And when you will have entered the city there, you will meet a company of prophets, descending from the high place, with a psaltery, and a timbrel, and a pipe, and a harp before them, and they will be prophesying.
6 Roho wa Bwana atakuja juu yako kwa nguvu, nawe utatoa unabii pamoja nao; nawe utageuzwa kuwa mtu wa tofauti.
And the Spirit of the Lord will spring up within you. And you shall prophesy with them, and you shall be changed into another man.
7 Mara ishara hizi zitakapotimizwa, fanya lolote mkono wako upasao kufanya, kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.
Therefore, when these signs will have happened to you, do whatever your hand will find, for the Lord is with you.
8 “Tangulia kushuka mbele yangu mpaka Gilgali. Hakika nami nitateremka nikujie ili kutoa dhabihu za sadaka za kuteketezwa na dhabihu za amani, lakini lazima ungoje kwa siku saba hata nitakapokujia na kukuambia likupasalo kufanya.”
And you shall descend before me into Gilgal, (for I will descend to you), so that you may offer an oblation, and may immolate victims of peace. For seven days, you shall wait, until I come to you, and reveal to you what you should do.”
9 Ikawa Sauli alipogeuka kumwacha Samweli, Mungu aliubadilisha moyo wa Sauli, na ishara hizi zote zikatimizwa siku ile.
And so, when he had turned his shoulder, so that he might go away from Samuel, God changed him to another heart. And all these signs occurred on that day.
10 Walipofika Gibea, akakutana na kundi la manabii. Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akajiunga nao katika kutoa unabii kwao.
And they arrived at the above-stated hill, and behold, a group of prophets met him. And the Spirit of the Lord leapt up within him, and he prophesied in their midst.
11 Ikawa wale wote waliomfahamu hapo mwanzo walipomwona akitoa unabii pamoja na manabii, wakaulizana, “Ni nini hiki kilichomtokea mwana wa Kishi? Je, Sauli naye pia yumo miongoni mwa manabii?”
Then all those who had known him yesterday and the day before, seeing that he was with the prophets, and that he was prophesying, said to one other: “What is this thing that has happened to the son of Kish? Could Saul also be among the prophets?”
12 Mtu mmoja ambaye aliishi huko akajibu, “Je, naye baba yao ni nani?” Basi ikawa mithali, kusema, “Je, Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?”
And one would respond to the other, saying, “And who is their father?” Because of this, it turned into a proverb, “Could Saul also be among the prophets?”
13 Baada ya Sauli kumaliza kutoa unabii, alikwenda mahali pa juu.
Then he ceased to prophesy, and he went to the high place.
14 Basi babaye mdogo akamuuliza Sauli na mtumishi wake, “Je, mlikuwa wapi?” Akajibu, “Tulikuwa tukiwatafuta punda. Lakini tulipoona hawapatikani, tulikwenda kwa Samweli.”
And the uncle of Saul said to him, and to his servant, “Where did you go?” And they responded: “To seek the donkeys. But when we did not find them, we went to Samuel.”
15 Babaye mdogo Sauli akasema, “Niambie Samweli amekuambia nini.”
And his uncle said to him, “Tell me what Samuel said to you.”
16 Sauli akajibu, “Alituhakikishia kwamba punda wamepatikana.” Lakini hakumwambia babaye mdogo kila kitu Samweli alichomwambia kuhusu ufalme.
And Saul said to his uncle, “He told us that the donkeys would be found.” But the word about the kingdom, which Samuel had spoken to him, he did not reveal to him.
17 Samweli akawaita watu wa Israeli kuja kwa Bwana huko Mispa,
And Samuel called the people together, to the Lord at Mizpah.
18 naye akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Niliwatoa Israeli kutoka Misri, nami niliwaokoa toka nguvu za Misri na falme zote zilizowaonea.’
And he said to the sons of Israel: “Thus says the Lord God of Israel: I led Israel away from Egypt, and I rescued you from the hand of the Egyptians, and from the hand of all the kings who were afflicting you.
19 Lakini sasa mmemkataa Mungu wenu, ambaye anawaokoa toka katika maafa yenu yote na taabu zenu zote. Nanyi mmesema, ‘Hapana, tuteulie mfalme atutawale.’ Sasa basi, jihudhurisheni wenyewe mbele za Bwana kwa kabila zenu na kwa koo zenu.”
But today you have rejected your God, who alone saved you from all your evils and tribulations. And you have said: ‘By no means! Instead, appoint a king over us.’ Now therefore, stand in the sight of the Lord, by your tribes and by your families.”
20 Samweli alipoyasogeza makabila yote ya Israeli, kabila la Benyamini likachaguliwa.
And Samuel brought near all the tribes of Israel, and the lot fell upon the tribe of Benjamin.
21 Kisha akalisogeza mbele kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo, nao ukoo wa Matri ukachaguliwa. Mwishoni Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa. Lakini walipomtafuta, hakuonekana.
And he brought near the tribe of Benjamin, with its families, and the lot fell upon the family of Matri. And then it went to Saul, the son of Kish. Therefore, they sought him, but he was not found.
22 Wakazidi kuuliza kwa Bwana, “Je, huyo mtu amekwisha kufika hapa?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, amejificha katikati ya mizigo.”
And after these things, they consulted the Lord as to whether he would soon arrive there. And the Lord responded, “Behold, he is hidden at home.”
23 Wakakimbia na kumleta kutoka huko, naye aliposimama katikati ya watu, alikuwa mrefu kuliko watu wengine wote.
And so they ran and brought him there. And he stood in the midst of the people, and he was taller than the entire people, from the shoulders upward.
24 Samweli akawaambia watu wote, “Je, mnamwona mtu ambaye Bwana amemchagua? Hayupo aliye kama yeye miongoni mwa watu wote.” Ndipo watu wakapiga kelele, wakasema, “Mfalme na aishi maisha marefu.”
And Samuel said to all the people: “Certainly, you see the one whom the Lord has chosen, that there is not anyone like him among all the people.” And all the people cried out and said, “Long live the king!”
25 Samweli akawaeleza watu madaraka ya ufalme. Akayaandika kwenye kitabu na kuweka mbele za Bwana. Kisha Samweli akawaruhusu watu, kila mmoja aende nyumbani kwake.
Then Samuel spoke to the people the law of the kingdom, and he wrote it in a book, and he stored it in the sight of the Lord. And Samuel dismissed all the people, each one to his own house.
26 Sauli pia akaenda nyumbani kwake huko Gibea, akisindikizwa na watu hodari ambao Mungu alikuwa amegusa mioyo yao.
And then Saul went away to his own house at Gibeah. And a portion of the army, whose hearts had been touched by God, went away with him.
27 Lakini baadhi ya watu wakorofi walisema, “Huyu mtu atawezaje kutuokoa?” Wakamdharau na wala hawakumletea zawadi. Lakini Sauli akanyamaza kimya.
Yet the sons of Belial said, “How could this one be able to save us?” And they despised him, and they brought him no presents. But he pretended not to hear them.

< 1 Samweli 10 >