< 1 Samweli 1 >
1 Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.
И бысть человек от Армафем Сифы, от горы Ефремли, и имя ему Елкана сын Иеремииль, сына Илиина, сына Фокеля в Насиве от Армафема от горы Ефремли:
2 Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.
и сему две жены (быша): имя единей Анна и имя вторей Феннана: и бяху Феннане дети, Анне же не бяше отрочате.
3 Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana.
И восхождаше человек от дне до дне из града своего Армафема покланятися и жрети Господу Богу Саваофу в Силом. И тамо бе Илий и два сына его Офни и Финеес, жерцы Господни.
4 Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.
И бысть день, и пожре Елкана и даде Феннане жене своей и сыном ея и дщерем ея части:
5 Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
Анне же даде часть едину, яко не бе ей чада, обаче Анну любляше Елкана паче Феннаны. И Господь затвори ложесна ея:
6 Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi.
занеже не даде ей Господь чада по скорби ея и по сетованию оскорбления ея, и сетоваше сего ради, яко затвори Господь утробу ея не дати ей чада.
7 Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.
Тако творяше от года до года, внегда приходити ей в дом Господень: (укоряше ея тако, ) и сетоваше, и плакаше, и не ядяше.
8 Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”
И рече ей Елкана муж ея: Анна. И рече ему: се, аз, господи. И рече ей: что ти есть, яко плачешися? И почто не яси? И почто биеши сердце твое? Несмь ли аз тебе добрее паче десяти чад?
9 Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana.
И воставши Анна по ядении их в Силоме, и ста пред Господем. Илий же жрец седяше на престоле, при празе двери храма Господня.
10 Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana.
И та умиленна душею, и помолися Господу и плачущи проплака,
11 Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”
и обеща обет Господу, глаголющи: Адонаи Господи Елои Саваоф, аще призирая призриши на смирение рабы Твоея и помянеши мя, и даси рабе Твоей семя мужеско, то дам е пред Тобою в дар до дне смерти его: и вина и пиянственнаго не испиет, и железо не взыдет на главу его.
12 Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake.
И бысть егда умножи молящися пред Господем, Илий же жрец смотряше на уста ея.
13 Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa
И та глаголаше в сердцы своем, токмо устне ея двизастеся, а глас ея не слышашеся: и мняше ю Илий пияну сущу.
14 naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”
И рече ей Илий: доколе пияна будеши? Отими вино твое и иди от места Господня.
15 Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana.
И отвеща Анна и рече: ни, господи: жена в жесток день аз есмь, вина и пиянства не пих, но изливаю пред Господем душу мою:
16 Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”
не даждь рабы твоея во дщерь погибели, яко от множества глумления моего и от множества сетования моего истаях даже доселе.
17 Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”
И отвеща Илий и рече к ней: иди с миром, Бог Израилев да даст ти все прошение твое, еже просила еси от Него.
18 Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.
И рече Анна: обрете раба твоя благодать пред очима твоима. И иде жена в путь свой, и вниде во обитель свою, и яде с мужем своим и пи, и лице ея не испаде ктому.
19 Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka.
И утреневаша заутра, и поклонишася Господу, и идоша путем своим. И вниде Елкана в дом свой во Армафем и позна Елкана жену свою Анну: и помяне ю Господь, и зачат.
20 Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”
И бысть во время дний, и роди Анна сына и нарече имя ему Самуил: и рече: яко от Господа Бога Саваофа испросих его.
21 Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake,
И взыде человек Елкана и весь дом его в Силом пожрети жертву дний и обеты своя и вся десятины земли своея.
22 Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”
Анна же не взыде с ним, яко рече мужеви своему: дондеже взыдет отроча, и аще отдою е, тогда явится лицу Господню и пребудет тамо до века.
23 Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.
И рече ей Елкана муж ея: твори благое пред очима твоима, седи дондеже отдоиши е: но да утвердит Господь (слово твое), изшедшее из уст твоих. И седе жена, и млеком питаше сына своего, дондеже отдои его.
24 Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo.
И взыде с ним в Силом, егда отдои его, с телцем трилетным и с хлебы и со ефи муки пшеничны и мехом вина: и внидоша в дом Господень в Силом, и отроча с ними.
25 Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,
И приведоша е пред Господа: и закла отец его жертву, юже творяше от дний на дни Господеви: и приведоша отроча, и закла телца. И приведе Анна мати отроча ко Илию
26 naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana.
и рече: во мне, господи, да живет душа твоя, господине мой, аз жена стоявшая пред тобою, о сем помолитися Господу:
27 Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba.
о отрочати сем молихся, и даде ми Господь прошение мое, еже просих у Него:
28 Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.
и аз отдаю е Господеви во вся дни живота его на служение Господеви. И поклонися тамо Господеви.