< 1 Samweli 1 >

1 Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.
Un viens vīrs bija no Ramatajim-Cofim, no Efraīma kalniem, Elkanus vārdā, Jeroama dēls, tas bija Elihus dēls, tas Tous dēls, tas Cuva dēls, no Efraīma cilts.
2 Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.
Šim bija divas sievas, vienai bija vārds Anna, un otras vārds bija Pennina, un Peninnai bija bērni, bet Annai bērnu nebija.
3 Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana.
Un šis vīrs nogāja ik gadus no savas pilsētas, Dievu pielūgt un upurēt Tam Kungam Cebaot Šīlo. Un tur bija tie divi Elus dēli, Hofnus un Pinehas, Tam Kungam par priesteriem.
4 Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.
Un tai dienā, kad Elkanus upurēja, viņš savai sievai Peninnai un visiem viņas dēliem un meitām deva daļas.
5 Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
Bet Annai viņš deva divkārtīgu daļu, jo viņš to Annu mīlēja, bet Tas Kungs viņas miesas bija aizslēdzis.
6 Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi.
Un viņas pretiniece viņu daudz apbēdināja un skumdināja kaitinādama, tādēļ ka Tas Kungs viņas miesas bija aizslēdzis.
7 Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.
Un tā viņš darīja ik gadus, kad viņa nogāja Tā Kunga namā. Un šī viņu skumdināja, ka viņa raudāja un neēda.
8 Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”
Tad Elkanus, viņas vīrs, uz viņu sacīja: Anna, kāpēc tu raudi? Un kāpēc tu neēdi? Un kāpēc tava sirds noskumusi? Vai es tev neesmu labāks nekā desmit dēli?
9 Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana.
Tad Anna cēlās, kad bija ēdusi un dzērusi Šīlo. Un Elus, tas priesteris, sēdēja uz krēsla pie stenderes Tā Kunga namā.
10 Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana.
Un viņas sirds dziļumā bija noskumusi un pielūdza To Kungu un raudāja gauži.
11 Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”
Un viņa solīja solījumu un sacīja: Kungs Cebaot, ja Tu Savas kalpones bēdas uzlūkosi un mani pieminēsi un Savu kalponi neaizmirsīsi un dosi Savai kalponei dēlu, tad es to Tam Kungam došu visu viņa mūžu, un dzenamam nazim nebūs nākt uz viņa galvu.
12 Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake.
Un kad viņa ilgi lūdza Tā Kunga priekšā, tad Elus viņas mutes (kustēšanu) lika vērā.
13 Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa
Jo Anna runāja savā sirdī un viņas lūpas tikai kustējās, bet viņas balss netapa dzirdēta, tāpēc Elum šķita, viņu esam piedzērušu.
14 naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”
Un Elus uz to sacīja: cik ilgi tu būsi piedzērusi? Lai tavs vīns no tevis atstājās.
15 Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana.
Bet Anna atbildēja un sacīja: nē, mans kungs, es esmu sieva ar bēdīgu sirdi, es neesmu ne vīna nedz stipra dzēriena dzērusi, bet savu sirdi esmu izgāzusi priekš Tā Kunga.
16 Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”
Neturi savu kalponi par tādu negodīgu sievu, jo es līdz šim esmu runājusi aiz lielām sirds nopūtām un bēdām.
17 Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”
Tad Elus atbildēja un sacīja: ej ar mieru, lai Israēla Dievs tev dod tavu lūgumu, ko tu no Viņa lūgusi.
18 Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.
Un viņa sacīja: lai tava kalpone žēlastību atrod tavās acīs. Tad tā sieva nogāja savu ceļu un ēda un viņas vaigs vairs neraudzījās tik noskumis.
19 Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka.
Un tie cēlās rītā agri un pielūdza Tā Kunga priekšā un griezās atpakaļ un nāca savā namā Rāmatā. Un Elkanus atzina Annu, savu sievu, un Tas Kungs viņu pieminēja.
20 Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”
Un pēc kāda laika Anna tapa grūta un dzemdēja dēlu un nosauca viņa vārdu Samuēli, jo (viņa sacīja) es no Tā Kunga to esmu izlūgusies.
21 Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake,
Kad nu tas vīrs, Elkanus, ar visu savu namu aizgāja, Tam Kungam upurēt to gadskārtējo upuri un savu solījumu,
22 Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”
Tad Anna negāja līdz, bet sacīja uz savu vīru: kad tas puisītis būs atšķirts, tad es viņu vedīšu, lai viņš rādās Tā Kunga priekšā un tur paliek mūžam.
23 Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.
Un Elkanus, viņas vīrs, uz to sacīja: dari, kā tev patīk, paliec šeitan, tiekams tu viņu būsi atšķīrusi; bet Tas Kungs lai piepilda Savu vārdu. Tā tā sieva palika un zīdīja savu dēlu, tiekams viņa to atšķīra.
24 Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo.
Un kad viņa to bija atšķīrusi, tad viņa to veda sev līdz ar trim vēršiem un vienu ēfu miltu un vienu trauciņu ar vīnu, un noveda Tā Kunga namā uz Šīlo; un tas zēns bija vēl jauns.
25 Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,
Un tie nokāva vērsi un pieveda to zēnu pie Elus.
26 naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana.
Un tā sacīja: mans kungs, tik tiešām kā tava dvēsele dzīvo, mans kungs, es esmu tā sieva, kas šeitan pie tevis stāvēja, To Kungu lūgdama.
27 Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba.
Es par šo bērnu esmu lūgusi, un Tas Kungs man devis manu lūgumu, ko es no Viņa esmu lūgusi.
28 Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.
Tādēļ es to arī Tam Kungam kā izlūgtu esmu nodevusi visu mūžu, kamēr tas dzīvos, - viņš ir no Tā Kunga izlūgts. Un tie tur pielūdza To Kungu.

< 1 Samweli 1 >