< 1 Samweli 1 >

1 Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.
Il y avait dans les montagnes d'Ephraïm un homme d'Armathaïm-Sipha; il se nommait Elcana, fils de Jéréméel, fils d'Eliu, fils de Thocé, l'un des Nasib d'Ephraïm.
2 Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.
Il avait deux femmes: le nom de la première était Anne; le nom de la seconde, Phenenna; or, Phenenna avait des enfants, et Anne n'en avait point.
3 Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana.
Les jours s'écoulèrent, et l'homme partit de la ville d'Armathaïm pour adorer le Seigneur Dieu sabaoth, et lui sacrifier en Silo; Héli et ses deux fils Ophni et Phinéès étaient alors prêtres du Seigneur.
4 Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.
Le jour venu, Elcana sacrifia; puis, il donna des parts à Phenenna, sa femme, et à ses fils.
5 Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
Mais il ne donna qu'une part à Anne, parce qu'elle n'avait pas d'enfants. Cependant, Elcana aimait Anne plus que la première; et le Seigneur avait clos ses entrailles;
6 Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi.
Car le Seigneur, quels que fussent son affliction et l'abattement causé par son affliction, ne lui avait point donné d'enfants. Elle était découragée, parce que le Seigneur avait clos ses entrailles, et ne lui avait point donné d'enfants.
7 Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.
Les choses se passaient de la sorte tous les ans lorsqu'elle montait à la maison du Seigneur; elle était abattue, et elle pleurait, et elle ne mangeait point.
8 Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”
Et son époux Elcana lui dit: Anne; et elle répondit: Me voici, seigneur; et il reprit: Qu'as-tu à pleurer? Pourquoi ne manges-tu point? Pourquoi ton cœur te fait-il souffrir? Ne suis-je pas pour toi meilleur que dix enfants?
9 Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana.
Et, après qu'ils eurent mangé à Silo, Anne se leva, puis elle alla se placer devant le Seigneur, pendant qu'Héli le prêtre était sur son siège, devant le seuil du temple du Seigneur.
10 Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana.
Là, tout affligée en son cœur, elle fit au Seigneur une prière, et elle se prit à pleurer amèrement.
11 Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”
Et elle fit un vœu au Seigneur, disant: Adonaï, Seigneur, Eloé sabaoth, si vous jetez les yeux sur l'humiliation de votre servante, si vous vous souvenez de moi, si vous donnez à votre servante un fils, je vous le consacrerai jusqu'au jour de sa mort; il ne boira ni vin ni boisson enivrante, et le fer ne passera jamais sur sa tête.
12 Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake.
Et pendant qu'elle prolongeait sa prière devant le Seigneur, Héli le prêtre était attentif au mouvement de ses lèvres,
13 Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa
Car elle parlait en son cœur, et elle remuait les lèvres, mais on n'entendait point sa voix; or, Héli la crut ivre.
14 naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”
Et le serviteur d'Héli alla lui dire: Jusqu'à quand seras-tu donc ivre? Va-t'en avec ton vin; retire-toi de devant le Seigneur.
15 Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana.
Anne répondit, et elle dit au prêtre: Non, seigneur, je suis aujourd'hui une femme pleine d'affliction, je n'ai bu ni vin ni boisson enivrante, et je répands mon âme devant le Seigneur.
16 Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”
Ne prends pas ta servante pour une fille de pestilence; c'est à cause de l'abondance de mes méditations que j'ai prolongé jusqu'à ce moment ma prière.
17 Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”
Héli reprenant, lui dit: Va en paix, que le Dieu d'Israël t'accorde toute ta prière, tout ce que tu lui as demandé.
18 Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.
Alors, elle dit: Ta servante a trouvé grâce devant tes yeux. Et la femme s'en alla, elle rentra à son logis, elle mangea et but avec son mari, et son visage cessa d'être abattu.
19 Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka.
Ensuite, s'étant levés de grand matin, ils adorèrent le Seigneur, et reprirent leur chemin; Elcana rentra dans sa maison d'Armathaïm, et il connut Anne; or, le Seigneur se souvint d'elle, et elle conçut.
20 Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”
Le temps révolu, elle enfanta un fils, et elle l'appela Samuel, parce que, dit-elle, je l'avais demandé au Seigneur Dieu sabaoth.
21 Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake,
Or, son époux Elcana, avec toute sa famille, monta à Silo pour offrir au Seigneur le sacrifice de la saison, ses oblations votives, et la dîme de tous les fruits de ses champs.
22 Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”
Mais Anne ne partit pas avec lui, et elle dit à son époux: J'irai quand l'enfant ira, quand je l'aurai sevré, et qu'il sera présenté au Seigneur pour y rester toujours.
23 Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.
Son époux Elcana lui répondit: Fais ce que bon te semble, demeure ici jusqu'à ce que tu l'aies sevré; que le Seigneur accomplisse toutes les paroles qui sont sorties de ta bouche. Et la femme ne bougea pas, et elle allaita son fils jusqu'à ce qu'elle le sevrât.
24 Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo.
Alors, elle partit avec Elcana pour Silo; ils avaient un bœuf de trois ans, des pains, un éphi de fleur de farine et un nébel de vin; elle entra à Silo dans la maison du Seigneur, et son enfant était avec eux.
25 Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,
Et ils le conduisirent devant le Seigneur; son père égorgea la victime que de saison en saison il sacrifiait au Seigneur; il présenta l'enfant après avoir égorgé le bœuf; et Anne, la mère de l'enfant, le conduisit à Héli,
26 naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana.
Et elle dit: Je te prie, seigneur, aussi vrai que tu vis, je suis la femme que tu as vue assise devant toi, priant le Seigneur.
27 Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba.
J'ai prié pour obtenir cet enfant, et le Seigneur a exaucé la prière que je lui avais faite.
28 Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.
Cet enfant, je le donne au Seigneur pour être tous les jours de sa vie au service du Seigneur; puis, elle dit:

< 1 Samweli 1 >