< 1 Samweli 1 >

1 Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.
Et il y avait un homme de Ramathaïm-Tsophim, de la montagne d’Éphraïm, et son nom était Elkana, fils de Jerokham, fils d’Élihu, fils de Thohu, fils de Tsuph, Éphratien;
2 Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.
et il avait deux femmes: le nom de l’une était Anne, et le nom de la seconde, Peninna. Et Peninna avait des enfants, mais Anne n’avait pas d’enfants.
3 Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana.
Et cet homme montait chaque année de sa ville pour adorer l’Éternel des armées et lui sacrifier à Silo; et là étaient les deux fils d’Éli, Hophni et Phinées, sacrificateurs de l’Éternel.
4 Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.
Et il arriva que, le jour où Elkana sacrifia, il donna des portions à Peninna, sa femme, et à chacun de ses fils et de ses filles;
5 Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
mais à Anne il donna une portion double, car il aimait Anne; mais l’Éternel avait fermé sa matrice.
6 Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi.
Et son ennemie la chagrinait aigrement, afin de la pousser à l’irritation, parce que l’Éternel avait fermé sa matrice.
7 Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.
Et [Elkana] faisait ainsi d’année en année. Chaque fois qu’elle montait à la maison de l’Éternel, [Peninna] la chagrinait ainsi; et elle pleurait, et ne mangeait pas.
8 Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”
Et Elkana, son mari, lui dit: Anne, pourquoi pleures-tu? et pourquoi ne manges-tu pas? et pourquoi ton cœur est-il chagrin? Est-ce que je ne vaux pas mieux pour toi que dix fils?
9 Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana.
Et Anne se leva, après qu’on eut mangé à Silo, et après qu’on eut bu; (et Éli, le sacrificateur, était assis sur un siège près de l’un des poteaux du temple de l’Éternel);
10 Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana.
et elle avait l’amertume dans l’âme, et elle pria l’Éternel et pleura abondamment.
11 Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”
Et elle fit un vœu, et dit: Éternel des armées! si tu veux regarder à l’affliction de ta servante, et si tu te souviens de moi et n’oublies pas ta servante, et que tu donnes à ta servante un enfant mâle, je le donnerai à l’Éternel [pour] tous les jours de sa vie; et le rasoir ne passera pas sur sa tête.
12 Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake.
Et il arriva que, comme elle priait longuement devant l’Éternel, Éli observa sa bouche.
13 Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa
Et Anne parlait dans son cœur; ses lèvres seulement remuaient, mais on n’entendait pas sa voix; et Éli pensa qu’elle était ivre.
14 naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”
Et Éli lui dit: Jusques à quand seras-tu ivre? Ôte ton vin d’avec toi.
15 Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana.
Et Anne répondit et dit: Non, mon seigneur; je suis une femme qui a l’esprit accablé; je n’ai bu ni vin ni boisson forte, mais je répandais mon âme devant l’Éternel.
16 Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”
Ne mets pas ta servante au rang d’une fille de Bélial; car c’est dans la grandeur de ma plainte et de mon chagrin que j’ai parlé jusqu’à présent.
17 Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”
Et Éli répondit et dit: Va en paix; et que le Dieu d’Israël t’accorde la demande que tu lui as faite!
18 Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.
Et elle dit: Que ta servante trouve grâce à tes yeux! Et la femme s’en alla son chemin; et elle mangea, et elle n’eut plus le même visage.
19 Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka.
Et ils se levèrent de bonne heure le matin, et se prosternèrent devant l’Éternel; et ils s’en retournèrent et vinrent dans leur maison, à Rama. Et Elkana connut Anne, sa femme; et l’Éternel se souvint d’elle.
20 Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”
Et il arriva que, quand les jours furent révolus, Anne, ayant conçu, enfanta un fils; et elle appela son nom Samuel: car je l’ai demandé à l’Éternel.
21 Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake,
Et Elkana, son mari, monta avec toute sa maison pour sacrifier à l’Éternel le sacrifice annuel et son vœu.
22 Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”
Mais Anne ne monta pas, car elle dit à son mari: [J’attendrai] jusqu’à ce que l’enfant soit sevré; alors je le mènerai, afin qu’il paraisse devant l’Éternel et qu’il habite là pour toujours.
23 Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.
Et Elkana, son mari, lui dit: Fais ce qui est bon à tes yeux, demeure jusqu’à ce que tu l’aies sevré; seulement, que l’Éternel accomplisse sa parole! Et la femme demeura, et elle allaita son fils jusqu’à ce qu’elle l’ait sevré.
24 Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo.
Et sitôt qu’elle l’eut sevré, elle l’emmena avec elle, avec trois jeunes taureaux, et un épha de farine et une outre de vin; et elle le mena à la maison de l’Éternel à Silo; et l’enfant était très jeune.
25 Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,
Et ils égorgèrent le taureau, et ils amenèrent le jeune garçon à Éli.
26 naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana.
Et elle dit: Ah, mon seigneur! ton âme est vivante, mon seigneur, je suis la femme qui se tenait ici près de toi pour prier l’Éternel.
27 Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba.
J’ai prié pour cet enfant, et l’Éternel m’a accordé la demande que je lui ai faite.
28 Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.
Et aussi, moi je l’ai prêté à l’Éternel; [pour] tous les jours de sa vie, il est prêté à l’Éternel. Et il se prosterna là devant l’Éternel.

< 1 Samweli 1 >