< 1 Samweli 1 >

1 Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.
Il y avait un homme de Ramathaïm-Zophim, dans la montagne d'Éphraïm. Son nom était Elkana, fils de Jerocham, fils d'Élihu, fils de Tohu, fils de Zuph, Éphraïmite.
2 Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.
Il avait deux femmes. Le nom de l'une était Anne, et le nom de l'autre Peninna. Peninna eut des enfants, mais Anne n'eut point d'enfants.
3 Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana.
Cet homme montait d'année en année hors de sa ville pour se prosterner et sacrifier à l'Éternel des armées à Silo. Les deux fils d'Eli, Hophni et Phinées, prêtres de l'Éternel, étaient là.
4 Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.
Le jour où Elkana offrit un sacrifice, il donna des portions à Peninna, sa femme, à tous ses fils et à toutes ses filles;
5 Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
mais il donna une double portion à Anne, car il aimait Anne, mais l'Éternel lui avait fermé les entrailles.
6 Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi.
Son rival la provoquait durement, pour l'irriter, parce que Yahvé avait fermé ses entrailles.
7 Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.
Ainsi, année après année, quand elle montait à la maison de l'Éternel, sa rivale l'irritait. Elle pleurait donc, et ne mangeait pas.
8 Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”
Elkana, son mari, lui dit: « Anne, pourquoi pleures-tu? Pourquoi ne manges-tu pas? Pourquoi ton cœur est-il affligé? Ne suis-je pas meilleur pour toi que dix fils? »
9 Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana.
Et Anne se leva, après qu'on eut fini de manger et de boire à Silo. Or, le sacrificateur Eli était assis sur son siège, près du poteau de la porte du temple de Yahvé.
10 Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana.
Elle était dans l'amertume de l'âme, et elle priait Yahvé en pleurant amèrement.
11 Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”
Elle fit un vœu et dit: « Yahvé des armées, si tu regardes l'affliction de ton serviteur et te souviens de moi, et si tu n'oublies pas ton serviteur, mais que tu donnes à ton serviteur un garçon, je le donnerai à Yahvé tous les jours de sa vie, et aucun rasoir ne viendra sur sa tête. »
12 Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake.
Comme elle continuait à prier devant Yahvé, Eli vit sa bouche.
13 Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa
Or Anne parlait dans son cœur. Seules ses lèvres bougeaient, mais on n'entendait pas sa voix. Aussi Éli pensa-t-il qu'elle était ivre.
14 naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”
Eli lui dit: « Jusqu'à quand seras-tu ivre? Débarrasse-toi de ton vin! »
15 Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana.
Anne répondit: « Non, mon seigneur, je suis une femme à l'esprit chagrin. Je n'ai bu ni vin ni boisson forte, mais j'ai répandu mon âme devant Yahvé.
16 Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”
Ne considère pas ta servante comme une femme méchante, car j'ai parlé dans l'abondance de ma plainte et de ma provocation. »
17 Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”
Eli répondit: « Va en paix; et que le Dieu d'Israël exauce la demande que tu lui as adressée. »
18 Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.
Elle dit: « Que ta servante trouve grâce à tes yeux. » La femme s'en alla donc et mangea, et l'expression de son visage n'était plus triste.
19 Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka.
Ils se levèrent de bon matin et se prosternèrent devant l'Éternel, puis ils s'en retournèrent et rentrèrent dans leur maison à Rama. Elkana connut alors Hannah, sa femme, et Yahvé se souvint d'elle.
20 Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”
Lorsque le temps fut venu, Anne conçut et enfanta un fils; elle lui donna le nom de Samuel, en disant: « Parce que je l'ai demandé à l'Éternel. »
21 Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake,
L'homme Elkana et toute sa maison montèrent pour offrir à Yahvé le sacrifice annuel et son vœu.
22 Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”
Mais Anne ne monta pas, car elle dit à son mari: « Pas avant que l'enfant soit sevré; alors je l'amènerai, afin qu'il se présente devant l'Éternel et qu'il y reste pour toujours. »
23 Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.
Elkana, son mari, lui dit: « Fais ce qui te semble bon. Attends que tu l'aies sevré; seulement, que Yahvé accomplisse sa parole. » La femme attendit et allaita son fils jusqu'à ce qu'elle le sevrât.
24 Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo.
Lorsqu'elle l'eut sevré, elle l'emporta avec elle, avec trois taureaux, un épha de farine et un récipient de vin, et elle l'amena dans la maison de l'Éternel à Silo. L'enfant était jeune.
25 Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,
Ils tuèrent le taureau et amenèrent l'enfant à Eli.
26 naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana.
Elle dit: « Oh, mon seigneur, aussi vrai que ton âme est vivante, mon seigneur, je suis la femme qui s'est tenue ici près de toi, en priant l'Éternel.
27 Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba.
J'ai prié pour cet enfant, et Yahvé m'a accordé la demande que je lui ai adressée.
28 Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.
C'est pourquoi je l'ai aussi remis à Yahvé. Aussi longtemps qu'il vivra, il sera donné à Yahvé. » Il y a adoré Yahvé.

< 1 Samweli 1 >