< 1 Petro 1 >
1 Petro, mtume wa Yesu Kristo: Kwa wateule wa Mungu, wageni katika ulimwengu, waliotawanyika kote katika Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia.
Pierre, apôtre de Jésus-Christ, aux élus qui vivent comme des étrangers dans la Dispersion, dans le Pont, la Galatie, la Cappadoce, l'Asie et la Bithynie,
2 Ni ninyi ambao mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba kulingana na alivyotangulia kuwajua, kupitia kwa kazi ya utakaso wa Roho, katika utiifu kwa Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake: Neema na amani ziwe kwenu kwa wingi.
selon la prescience de Dieu le Père, dans la sanctification de l'Esprit, afin que vous obéissiez à Jésus-Christ et que vous soyez aspergés de son sang: Que la grâce et la paix vous soient multipliées.
3 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema zake kuu ametuzaa sisi mara ya pili katika tumaini lenye uzima kupitia kwa kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu,
Béni soit le Dieu et Père de notre Seigneur Jésus-Christ, qui, selon sa grande miséricorde, nous a fait renaître à une espérance vivante par la résurrection de Jésus-Christ d'entre les morts,
4 ili tuupate urithi usioharibika, usio na uchafu, ule usionyauka: uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu,
pour un héritage incorruptible, inaltérable et impérissable, qui vous est réservé dans les cieux,
5 ninyi ambao mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani, hadi uje ule wokovu ulio tayari kufunuliwa nyakati za mwisho.
vous qui, par la puissance de Dieu, êtes gardés par la foi pour un salut prêt à être révélé au dernier moment.
6 Katika hili mnafurahi sana, ingawa sasa kwa kitambo kidogo mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna nyingi.
C'est là votre grande joie, bien que pour un peu de temps encore, s'il le faut, vous ayez été affligés par diverses épreuves,
7 Haya yamewajia ili kwamba imani yenu, iliyo ya thamani kuliko dhahabu ipoteayo, ingawa hujaribiwa kwa moto, ionekane kuwa halisi na imalizie katika sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atadhihirishwa.
afin que l'épreuve de votre foi, qui est plus précieuse que l'or périssable, même si elle est éprouvée par le feu, donne lieu à la louange, à la gloire et à l'honneur, lors de la révélation de Jésus-Christ,
8 Ingawa hamjamwona, mnampenda; tena ingawa sasa hammwoni, mnamwamini na kujawa na furaha isiyoneneka yenye utukufu usioelezeka.
que vous aimez sans le connaître. En lui, bien que maintenant vous ne le voyiez pas, mais en croyant, vous vous réjouissez d'une joie indicible et pleine de gloire,
9 Maana mnaupokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.
recevant le résultat de votre foi, le salut de vos âmes.
10 Kwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa,
Pour ce qui est de ce salut, les prophètes ont cherché et cherché avec soin. Ils ont prophétisé la grâce qui vous sera accordée,
11 wakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ule ambao ungefuata.
cherchant à savoir à qui ou à quel moment l'Esprit du Christ qui était en eux se référait lorsqu'il prédisait les souffrances du Christ et les gloires qui les suivraient.
12 Walidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.
Il leur a été révélé qu'ils ne se servaient pas eux-mêmes, mais vous, dans ces choses qui vous ont été annoncées maintenant par ceux qui vous ont annoncé la Bonne Nouvelle par l'Esprit Saint envoyé du ciel, choses que les anges veulent examiner.
13 Kwa hiyo, tayarisheni nia zenu kwa kazi; mwe na kiasi, mkitumainia kikamilifu ile neema mtakayopewa Yesu Kristo atakapodhihirishwa.
Préparez donc vos esprits à l'action. Soyez sobres, et mettez toute votre espérance dans la grâce qui vous sera accordée lors de la révélation de Jésus-Christ -
14 Kama watoto watiifu, msifuate tamaa zenu mbaya wakati mlipoishi kwa ujinga.
comme des enfants obéissants, ne vous conformant pas à vos anciennes convoitises comme dans votre ignorance,
15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi kuweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.
mais, comme celui qui vous a appelés est saint, vous aussi, soyez saints dans toute votre conduite,
16 Kwa maana imeandikwa: “Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
car il est écrit: « Vous serez saints, car je suis saint. »
17 Kwa sababu mnamwita Baba ahukumuye kila mtu kulingana na matendo yake pasipo upendeleo, enendeni kwa hofu ya kumcha Mungu wakati wenu wa kukaa hapa duniani kama wageni.
Si vous l'invoquez comme Père, lui qui, sans acception de personnes, juge selon l'œuvre de chacun, passez ici le temps de votre vie d'étrangers dans une crainte respectueuse,
18 Kwa maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutoka mwenendo wenu usiofaa ambao mliurithi kutoka kwa baba zenu, si kwa vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu,
sachant que vous avez été rachetés, non avec des choses corruptibles, comme l'argent ou l'or, du mode de vie inutile transmis par vos pères,
19 bali kwa damu ya thamani ya Kristo, yule Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa.
mais par un sang précieux, comme celui d'un agneau sans défaut ni tache, le sang de Christ,
20 Yeye alichaguliwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
qui était déjà connu avant la fondation du monde, mais qui a été révélé dans ce dernier siècle à cause de vous,
21 Kupitia kwake mmemwamini Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu na akampa utukufu, ili imani yenu na tumaini lenu ziwe kwa Mungu.
vous qui, par lui, croyez en Dieu, qui l'a ressuscité des morts et lui a donné la gloire, afin que votre foi et votre espérance soient en Dieu.
22 Basi kwa kuwa mmejitakasa nafsi zenu kwa kuitii ile kweli hata mkawa na upendo wa ndugu usio na unafiki, basi pendaneni kwa dhati kutoka moyoni.
Ayant purifié vos âmes en obéissant à la vérité par l'Esprit, dans une affection fraternelle sincère, aimez-vous les uns les autres de tout votre cœur avec ferveur,
23 Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. (aiōn )
étant nés de nouveau, non d'une semence corruptible, mais d'une semence incorruptible, par la parole de Dieu, qui vit et demeure éternellement. (aiōn )
24 Maana, “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao ni kama maua ya kondeni; majani hunyauka na maua huanguka,
Car, « Toute chair est comme l'herbe, et toute la gloire de l'homme comme la fleur dans l'herbe. L'herbe se fane, et sa fleur tombe;
25 lakini neno la Bwana ladumu milele.” Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu. (aiōn )
mais la parole du Seigneur dure à jamais. » C'est la parole de la Bonne Nouvelle qui vous a été annoncée. (aiōn )