< 1 Petro 1 >

1 Petro, mtume wa Yesu Kristo: Kwa wateule wa Mungu, wageni katika ulimwengu, waliotawanyika kote katika Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia.
Peter, an apostle of Jesus Christ, to the elect sojourners of the Dispersion in Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia and Bithynia,
2 Ni ninyi ambao mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba kulingana na alivyotangulia kuwajua, kupitia kwa kazi ya utakaso wa Roho, katika utiifu kwa Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake: Neema na amani ziwe kwenu kwa wingi.
elect according to the foreknowledge of God the Father, by the setting apart of the Spirit, unto obedience and sprinkling with the blood of Jesus Christ: May grace and peace be multiplied to you.
3 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema zake kuu ametuzaa sisi mara ya pili katika tumaini lenye uzima kupitia kwa kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu,
Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who according to His great mercy has given us another birth into a living hope through the resurrection of Jesus Christ from among the dead,
4 ili tuupate urithi usioharibika, usio na uchafu, ule usionyauka: uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu,
into an imperishable and undefiled and unfading inheritance, already reserved in the heavens for you,
5 ninyi ambao mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani, hadi uje ule wokovu ulio tayari kufunuliwa nyakati za mwisho.
who are being guarded by the power of God through faith unto a salvation ready to be revealed in the last time.
6 Katika hili mnafurahi sana, ingawa sasa kwa kitambo kidogo mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna nyingi.
You should be overjoyed about this, even if just now, briefly, of necessity, you have been distressed by a variety of trials,
7 Haya yamewajia ili kwamba imani yenu, iliyo ya thamani kuliko dhahabu ipoteayo, ingawa hujaribiwa kwa moto, ionekane kuwa halisi na imalizie katika sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atadhihirishwa.
so that the demonstrated genuineness of your faith (much more precious than gold that perishes, albeit tested through fire) may translate into praise, glory and honor at the revelation of Jesus Christ
8 Ingawa hamjamwona, mnampenda; tena ingawa sasa hammwoni, mnamwamini na kujawa na furaha isiyoneneka yenye utukufu usioelezeka.
—whom not having understood you love, into whom believing (not yet seeing) you exult with joy inexpressible, already glorified,
9 Maana mnaupokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.
obtaining for yourselves the end result of your faith, the salvation of your souls.
10 Kwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa,
Concerning this salvation the prophets, who prophesied about the grace that would come to you, searched and inquired diligently,
11 wakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ule ambao ungefuata.
investigating into whom, or what sort of time, the Spirit of Christ who was in them was indicating as He testified beforehand the sufferings that would be inflicted on Christ and the glories that would follow them.
12 Walidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.
It was revealed to them that they were not ministering these things to themselves, but to you; which things have now been announced to you by those who proclaimed the gospel to you, with the Holy Spirit sent from heaven—things that angels really desire to look into.
13 Kwa hiyo, tayarisheni nia zenu kwa kazi; mwe na kiasi, mkitumainia kikamilifu ile neema mtakayopewa Yesu Kristo atakapodhihirishwa.
Therefore, having girded up the loins of your mind, staying sober, rest your hope fully upon the grace being brought to you in the revelation of Jesus Christ—
14 Kama watoto watiifu, msifuate tamaa zenu mbaya wakati mlipoishi kwa ujinga.
as children of obedience, not conforming yourselves to the former lusts as in your ignorance,
15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi kuweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.
but just as He who called you is holy, you also be holy in all your way of life,
16 Kwa maana imeandikwa: “Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
because it is written, “You shall be holy, for I am holy.”
17 Kwa sababu mnamwita Baba ahukumuye kila mtu kulingana na matendo yake pasipo upendeleo, enendeni kwa hofu ya kumcha Mungu wakati wenu wa kukaa hapa duniani kama wageni.
Also, since you invoke as Father the One who without partiality judges according to each one's work, conduct yourselves during the time of your sojourn here in fear,
18 Kwa maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutoka mwenendo wenu usiofaa ambao mliurithi kutoka kwa baba zenu, si kwa vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu,
knowing that it was not with perishable things (silver or gold) that you were redeemed from the futile way of life handed down by your forefathers,
19 bali kwa damu ya thamani ya Kristo, yule Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa.
but with the precious blood of Christ, as of a faultless and pure lamb;
20 Yeye alichaguliwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
who was foreknown indeed before the foundation of the world, but was revealed in these last times for your sake,
21 Kupitia kwake mmemwamini Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu na akampa utukufu, ili imani yenu na tumaini lenu ziwe kwa Mungu.
who through Him are believing into God, who raised Him out from the dead and gave Him glory, so that your faith and hope are into God.
22 Basi kwa kuwa mmejitakasa nafsi zenu kwa kuitii ile kweli hata mkawa na upendo wa ndugu usio na unafiki, basi pendaneni kwa dhati kutoka moyoni.
Since you have purified your souls by obeying the truth through the Spirit, resulting in sincere brotherly love, you must love one another fervently from a pure heart,
23 Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. (aiōn g165)
having been begotten again, not from a corruptible seed but an incorruptible, through the living Word of God that remains valid forever. (aiōn g165)
24 Maana, “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao ni kama maua ya kondeni; majani hunyauka na maua huanguka,
For: “All flesh is as grass, and all man's glory as flower of grass. The grass withers and its flower falls off, but the Lord's word endures forever.”
25 lakini neno la Bwana ladumu milele.” Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu. (aiōn g165)
Now this is the good word that was proclaimed to you. (aiōn g165)

< 1 Petro 1 >