< 1 Petro 1 >
1 Petro, mtume wa Yesu Kristo: Kwa wateule wa Mungu, wageni katika ulimwengu, waliotawanyika kote katika Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia.
Peter, Jesu Kristi Apostel, til Udlændingene i Adspredelse i Pontus, Galatien, Kappadokien, Asien og Bithynien,
2 Ni ninyi ambao mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba kulingana na alivyotangulia kuwajua, kupitia kwa kazi ya utakaso wa Roho, katika utiifu kwa Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake: Neema na amani ziwe kwenu kwa wingi.
udvalgte efter Gud Faders Forudviden, ved Aandens Helligelse, til Lydighed og Bestænkelse med Jesu Kristi Blod: Naade og Fred vorde eder mangfoldig til Del!
3 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema zake kuu ametuzaa sisi mara ya pili katika tumaini lenye uzima kupitia kwa kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu,
Lovet være Gud og vor Herres Jesu Kristi Fader, som efter sin store Barmhjertighed har genfødt os til et levende Haab ved Jesu Kristi Opstandelse fra de døde,
4 ili tuupate urithi usioharibika, usio na uchafu, ule usionyauka: uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu,
til en uforkrænkelig og ubesmittelig og uvisnelig Arv, som er bevaret i Himlene til eder,
5 ninyi ambao mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani, hadi uje ule wokovu ulio tayari kufunuliwa nyakati za mwisho.
I, som ved Guds Kraft bevogtes ved Tro til en Frelse, som er rede til at aabenbares i den sidste Tid,
6 Katika hili mnafurahi sana, ingawa sasa kwa kitambo kidogo mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna nyingi.
i hvilken I skulle fryde eder, om I end nu en liden Stund, hvis saa skal være, bedrøves i mange Haande Prøvelser,
7 Haya yamewajia ili kwamba imani yenu, iliyo ya thamani kuliko dhahabu ipoteayo, ingawa hujaribiwa kwa moto, ionekane kuwa halisi na imalizie katika sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atadhihirishwa.
for at eders prøvede Tro, som er meget dyrebarere end det forgængelige Guld, der dog prøves ved Ild, maa findes til Ros og Herlighed og Ære i Jesu Kristi Aabenbarelse,
8 Ingawa hamjamwona, mnampenda; tena ingawa sasa hammwoni, mnamwamini na kujawa na furaha isiyoneneka yenye utukufu usioelezeka.
ham, som I ikke have set og dog elske, ham, som I, skønt I nu ikke se, men tro, skulle fryde eder over med en uudsigelig og forherliget Glæde,
9 Maana mnaupokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.
naar I naa Maalet for eders Tro, Sjælenes Frelse.
10 Kwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa,
Om denne Frelse have Profeter gransket og ransaget, de, som profeterede om den Naade, der skulde blive eder til Del,
11 wakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ule ambao ungefuata.
idet de granskede over, hvilken eller hvordan en Tid Kristi Aand, som var i dem, henviste til, naar den forud vidnede om Kristi Lidelser og den derpaa følgende Herlighed.
12 Walidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.
Og det blev dem aabenbaret, at det ikke var dem selv, men eder, de tjente med disse Ting, som nu ere blevne eder kundgjorte ved dem, der have forkyndt eder Evangeliet i den Helligaand, som blev sendt fra Himmelen, hvilke Ting Engle begære at skue ind i.
13 Kwa hiyo, tayarisheni nia zenu kwa kazi; mwe na kiasi, mkitumainia kikamilifu ile neema mtakayopewa Yesu Kristo atakapodhihirishwa.
Derfor, binder op om eders Sinds Lænder, være ædrue, og sætter fuldt ud eders Haab til den Naade, som bliver eder til Del i Jesu Kristi Aabenbarelse.
14 Kama watoto watiifu, msifuate tamaa zenu mbaya wakati mlipoishi kwa ujinga.
Som lydige Børn skulle I ikke skikke eder efter de forrige Lyster i eders Vankundighed;
15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi kuweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.
men efter den hellige, som kaldte eder, skulle ogsaa I vorde hellige i al eders Vandel;
16 Kwa maana imeandikwa: “Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
thi der er skrevet: „I skulle være hellige, thi jeg er hellig.”
17 Kwa sababu mnamwita Baba ahukumuye kila mtu kulingana na matendo yake pasipo upendeleo, enendeni kwa hofu ya kumcha Mungu wakati wenu wa kukaa hapa duniani kama wageni.
Og dersom I paakalde ham som Fader, der dømmer uden Persons Anseelse efter enhvers Gerning, da bør I vandre i Frygt eders Udlændigheds Tid,
18 Kwa maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutoka mwenendo wenu usiofaa ambao mliurithi kutoka kwa baba zenu, si kwa vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu,
vel vidende, at det ikke var med forkrænkelige Ting, Sølv eller Guld, at I bleve løskøbte fra eders tomme Vandel, som var overleveret eder fra Fædrene,
19 bali kwa damu ya thamani ya Kristo, yule Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa.
men med Kristi dyrebare Blod som et lydeløst og uplettet Lams,
20 Yeye alichaguliwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
han, som var forud kendt før Verdens Grundlæggelse, men blev aabenbaret ved Tidernes Ende for eders Skyld,
21 Kupitia kwake mmemwamini Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu na akampa utukufu, ili imani yenu na tumaini lenu ziwe kwa Mungu.
der ved ham tro paa Gud, som oprejste ham fra de døde og gav ham Herlighed, saa at eders Tro ogsaa er Haab til Gud.
22 Basi kwa kuwa mmejitakasa nafsi zenu kwa kuitii ile kweli hata mkawa na upendo wa ndugu usio na unafiki, basi pendaneni kwa dhati kutoka moyoni.
Lutrer eders Sjæle i Lydighed imod Sandheden til uskrømtet Broderkærlighed, og elsker hverandre inderligt af Hjertet,
23 Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. (aiōn )
genfødte, som I ere, ikke af forkrænkelig, men af uforkrænkelig Sæd, ved Guds levende og blivende Ord. (aiōn )
24 Maana, “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao ni kama maua ya kondeni; majani hunyauka na maua huanguka,
Thi „alt Kød er som Græs, og al dets Herlighed som Græssets Blomst; Græsset visner, og Blomsten falder af;
25 lakini neno la Bwana ladumu milele.” Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu. (aiōn )
men Herrens Ord bliver evindelig.” Og dette er det Ord, som er forkyndt eder ved Evangeliet. (aiōn )