< 1 Petro 5 >

1 Kwa wazee waliomo miongoni mwenu, nawasihi mimi nikiwa mzee mwenzenu, shahidi wa mateso ya Kristo, na mshiriki katika utukufu utakaofunuliwa:
Tos vecajus jūsu starpā pamācu, es tas līdzvecākais un liecinieks par Kristus ciešanām un tās godības biedrs, kas taps redzams:
2 lichungeni kundi la Mungu mlilokabidhiwa, mkitumika kama waangalizi, si kwa kulazimishwa bali kwa hiari, kama Mungu anavyowataka mwe; si kwa tamaa ya fedha, bali mlio na bidii katika kutumika.
Ganiet Dieva ganāmo pulku, kas pie jums, un uzraugiet, ne piespiesti, bet ar labu prātu, ne negodīgas peļņas dēļ bet no sirds,
3 Msijifanye mabwana juu ya wale walio chini ya uangalizi wenu, bali kuweni vielelezo kwa hilo kundi.
Nedz kā valdīdami par Tā Kunga daļu, bet (par) priekšzīmi būdami tam ganāmam pulkam.
4 Naye Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtapokea taji ya utukufu isiyoharibika.
Un kad Tas Augstais Gans atspīdēs, tad jūs dabūsiet to nesavīstamo godības kroni.
5 Vivyo hivyo, ninyi mlio vijana watiini wazee. Nanyi nyote imewapasa kujivika unyenyekevu kila mtu kwa mwenzake, kwa kuwa, “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”
Tāpat, jūs jaunākie, esiet tiem vecajiem paklausīgi; bet visi, cits citam padodamies, esiet izpušķoti ar pazemību, jo Dievs lepniem turas pretī, bet pazemīgiem Viņš dod žēlastību.
6 Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake.
Tad nu pazemojaties apakš Dieva varenās rokas, lai Viņš jūs paaugstina savā laikā.
7 Mtwikeni yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana na mambo yenu.
Visu savu zūdīšanos metiet uz Viņu, jo Viņš gādā par jums.
8 Mwe na kiasi na kukesha, maana adui yenu ibilisi huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mtu ili apate kummeza.
Esiet skaidrā prātā, esiet nomodā, jo jūsu pretinieks, velns, staigā apkārt kā rūcošs lauva, un meklē, kuru tas aprītu.
9 Mpingeni, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kwamba mateso kama hayo yanawapata ndugu zenu pote duniani.
Tam stāviet pretim, stipri ticībā, zinādami, ka tās pašas ciešanas papilnam uziet jūsu brāļiem pasaulē.
10 Nanyi mkiisha kuteswa kwa kitambo kidogo, Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele ndani ya Kristo, yeye mwenyewe atawarejesha na kuwatia nguvu, akiwaimarisha na kuwathibitisha. (aiōnios g166)
Bet Tas visu žēlīgais Dievs, kas mūs aicinājis uz Savu mūžīgo godību iekš Kristus Jēzus, Tas jūs, kas mazu brīdi ciešat, Pats sataisīs, spēcinās, stiprinās, pastāvīgus darīs. (aiōnios g166)
11 Uweza una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Tam lai ir gods un vara mūžīgi mūžam. Āmen. (aiōn g165)
12 Kwa msaada wa Silvano, ambaye ninamhesabu kuwa ndugu mwaminifu, nimewaandikia waraka huu mfupi ili kuwatia moyo, na kushuhudia kwamba hii ni neema halisi ya Mungu. Simameni imara katika neema hiyo.
Caur Silvanu, to uzticīgo brāli, es jums, kā man šķiet īsiem vārdiem esmu rakstījis, pamācīdams un apliecinādams, ka tā ir tā patiesā Dieva žēlastība, kurā jūs stāvat.
13 Kanisa lililoko Babeli, lililochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu; vivyo hivyo mwanangu Marko anawasalimu.
Jūs sveicina tā līdz izvēlētā Bābeles draudze un mans dēls Marks.
14 Salimianeni kwa busu la upendo. Amani iwe nanyi nyote mlio katika Kristo.
Sveicinājaties savā starpā ar mīlestības skūpstu. Miers jums visiem, kas iekš Kristus Jēzus. Āmen.

< 1 Petro 5 >