< 1 Petro 4 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni nia iyo hiyo kwa maana mtu aliyekwisha kuteswa katika mwili ameachana na dhambi.
Since, then, Christ suffered in body, arm yourselves with the same resolve as he; for he who has suffered in body has ceased to sin,
2 Kwa hivyo, haishi maisha yake yaliyobaki ya kuishi hapa duniani kwa tamaa mbaya za wanadamu, bali anaishi kwa mapenzi ya Mungu.
and so will live the rest of his earthly life guided, not by human passions, but by the will of God.
3 Maana wakati uliopita mmekwisha kutumia muda wa kutosha katika maisha yenu mkifanya yale ambayo wapagani hupenda kutenda: wakiishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, vileo, ngoma mbaya, na ibada chukizo za sanamu.
Surely in the past you have spent time enough living as the Gentiles delight to live. For your path has lain among scenes of debauchery, licentiousness, drunkenness, revelry, hard-drinking, and profane idolatry.
4 Wao hushangaa kwamba ninyi hamjiingizi pamoja nao katika huo wingi wa maisha ya ufisadi, nao huwatukana ninyi.
And, because you do not run to the same extremes of profligacy as others, they are astonished, and malign you.
5 Lakini itawapasa wao kutoa hesabu mbele zake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.
But they will have to answer for their conduct to him who is ready to judge both the living and the dead.
6 Kwa kuwa hii ndiyo sababu Injili ilihubiriwa hata kwa wale waliokufa, ili wahukumiwe sawasawa na wanadamu wengine katika mwili, lakini katika roho waishi kulingana na Mungu aishivyo.
For that was why the good news was told to the dead also – that, after they have been judged in the body, as people are judged, they might live in the spirit, as God lives.
7 Mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo kuweni na akili tulivu na kiasi, mkikesha katika kuomba.
But the end of all things is near. Therefore exercise self-restraint and be calm, so that you may be able to pray.
8 Zaidi ya yote, dumuni katika upendo kwa maana upendo husitiri wingi wa dhambi.
Above all things, let your love for one another be earnest, for ‘Love throws a veil over countless sins.’
9 Kuweni wakarimu kila mtu na mwenzake pasipo manungʼuniko.
Never grudge hospitality to one another.
10 Kila mmoja na atumie kipawa chochote alichopewa kuwahudumia wengine, kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu.
Whatever the gift that each has received, use it in the service of others, as good stewards of the varied bounty of God.
11 Yeyote asemaye hana budi kusema kama mtu asemaye maneno ya Mungu mwenyewe. Yeyote ahudumuye hana budi kuhudumu kwa nguvu zile anazopewa na Mungu, ili Mungu apate kutukuzwa katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
When anyone speaks, they should speak as one who is delivering the oracles of God. When anyone is endeavoring to serve others, they should do so in reliance on the strength which God supplies; so that in everything God may be honored through Jesus Christ – to whom be ascribed all honor and might for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
12 Wapenzi, msione ajabu kwa yale mateso yanayotukia miongoni mwenu, kana kwamba ni kitu kigeni kinachowapata.
Dear friends, do not be astonished at the trial of fire that you are passing through, to test you, as though something strange were happening to you.
13 Bali furahini kuwa mnashiriki katika mateso ya Kristo, ili mpate kufurahi zaidi wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
No, the more you share the sufferings of the Christ, the more may you rejoice, that, when the time comes for the manifestation of his glory, you may rejoice and exult.
14 Kama mkitukanwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu Roho wa utukufu na wa Mungu anakaa juu yenu.
If you are insulted for bearing the name of Christ, count yourselves blessed; because the divine glory and the Spirit of God are resting on you.
15 Lakini asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu anayeteswa kwa kuwa ni muuaji, au mwizi, au mhalifu wa aina yoyote, au anayejishughulisha na mambo ya watu wengine.
I need hardly say that no one among you must suffer as a murderer, or a thief, or a criminal, or for interfering in matters which do not concern Christians.
16 Lakini kama ukiteseka kwa kuwa Mkristo, usihesabu jambo hilo kuwa ni aibu, bali mtukuze Mungu kwa sababu umeitwa kwa jina hilo.
But, if someone suffers as a Christian, they should not be ashamed of it; they should bring honor to God even though they bear that name.
17 Kwa maana wakati umewadia wa hukumu kuanzia katika nyumba ya Mungu. Basi kama ikianzia kwetu sisi, mwisho wa hao wasiotii Injili ya Mungu utakuwaje?
For the time has come for judgment to begin with the house of God; and, if it begins with us, what will be the end of those who reject God’s good news?
18 Basi, “Ikiwa ni vigumu kwa mwenye haki kuokoka, itakuwaje kwa mtu asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?”
If ‘a good person is saved only with difficulty, what will become of the godless and the sinful?’
19 Kwa hiyo, wale wanaoteswa kulingana na mapenzi ya Mungu, wajikabidhi kwa Muumba wao aliye mwaminifu, huku wakizidi kutenda mema.
Therefore, I say, let those who suffer, because God wills it so, commit their lives into the hands of a faithful Creator, and persevere in doing right.

< 1 Petro 4 >