< 1 Petro 2 >

1 Kwa hiyo, wekeni mbali nanyi uovu wote na udanganyifu wote, unafiki, wivu na masingizio ya kila namna.
Having put aside, then, all evil, and all guile, and hypocrisies, and envyings, and all evil speakings,
2 Kama watoto wachanga, waliozaliwa sasa, yatamanini maziwa ya kiroho yasiyochanganywa na kitu kingine chochote, ili kwa hayo mpate kukua katika wokovu,
as newborn babies, desire the reasonable, unspoiled milk, so that you may grow up to salvation,
3 ikiwa kweli mmeonja ya kwamba Bwana ni mwema.
if [it] so be [that] you tasted that the LORD [is] good,
4 Mnapokuja kwake, yeye aliye Jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu bali kwa Mungu ni teule na la thamani kwake,
to whom coming—a living stone—having indeed been disapproved of by men, but with God—choice [and] precious,
5 ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mnajengwa kuwa nyumba ya kiroho, ili mpate kuwa ukuhani mtakatifu, mkitoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
and you yourselves are built up as living stones [into] a spiritual house, a holy priesthood, to offer up spiritual sacrifices acceptable to God through Jesus Christ.
6 Kwa maana imeandikwa katika Maandiko: “Tazama, naweka katika Sayuni, jiwe la pembeni teule lenye thamani, na yeyote atakayemwamini hataaibika kamwe.”
For this reason, also, it is contained in the Writing: “Behold, I lay in Zion a chief cornerstone, choice, precious, and he who is believing on Him may not be put to shame”;
7 Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hili ni la thamani. Lakini kwao wasioamini, “Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni,”
to you, then, who are believing—the preciousness; but to the unbelieving, [the] stone that the builders disapproved of—this One has become the head of [the] corner,
8 tena, “Jiwe lenye kuwafanya watu wajikwae, na mwamba wa kuwaangusha.” Wanajikwaa kwa sababu hawakulitii lile neno, kama walivyowekewa tangu zamani.
and a stone of stumbling and a rock of offense—who are stumbling at the word, being unbelieving—to which they were also set.
9 Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.
But you [are] a chosen race, a royal priesthood, a holy nation, a people acquired, that you may show forth the excellencies of Him who called you out of darkness into His wonderful light,
10 Mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni taifa la Mungu. Mwanzo mlikuwa hamjapata rehema, lakini sasa mmepata rehema.
who [were] once not a people, but [are] now the people of God; who had not found mercy, but now have found mercy.
11 Wapenzi, ninawasihi, mkiwa kama wageni na wapitaji hapa ulimwenguni, epukeni tamaa mbaya za mwili ambazo hupigana vita na roho zenu.
Beloved, I call on [you], as strangers and sojourners, to keep from the fleshly desires that war against the soul,
12 Kuweni na mwenendo mzuri mbele ya watu wasiomjua Mungu, ili kama wanawasingizia kuwa watenda mabaya, wayaone matendo yenu mema nao wamtukuze Mungu siku atakapokuja kwetu.
having your behavior right among the nations, so that whenever they speak against you as evildoers, seeing [your] good works, they may glorify God in [the] day of inspection.
13 Kwa ajili ya Bwana, tiini kila mamlaka iliyowekwa na wanadamu: Kwa mfalme kwani ndiye aliye na mamlaka ya juu zaidi,
Be subject, then, to every human creation, because of the LORD, whether to a king, as the highest,
14 au kwa maafisa aliowaweka, kwa kuwa mfalme amewatuma ili kuwaadhibu wale wanaokosa, na kuwapongeza wale watendao mema.
whether to governors, as to those sent through him, for punishment, indeed, of evildoers, and a praise of those doing good;
15 Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema mnyamazishe maneno ya kijinga ya watu wapumbavu.
because, so is the will of God, doing good, to put to silence the ignorance of the foolish men—
16 Ishini kama watu huru, lakini msitumie uhuru wenu kama kisingizio cha kutenda uovu, bali ishini kama watumishi wa Mungu.
as free, and not having freedom as the cloak of evil, but as servants of God;
17 Mheshimuni kila mtu ipasavyo: Wapendeni jamaa ya ndugu waumini, mcheni Mungu, mpeni heshima mfalme.
give honor to all; love the brotherhood; fear God; honor the king.
18 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wema na wapole peke yao, bali pia wale walio wakali.
Servants, be subject in all fear to the masters, not only to the good and gentle, but also to the crooked;
19 Kwa maana ni jambo la sifa kama mtu akivumilia anapoteswa kwa uonevu kwa ajili ya Mungu.
for this [is] grace: if anyone endures sorrows because of conscience toward God, suffering unrighteously;
20 Kwani ni faida gani kwa mtu kustahimili anapopigwa kwa sababu ya makosa yake? Lakini kama mkiteswa kwa sababu ya kutenda mema, nanyi mkastahimili, hili ni jambo la kusifiwa mbele za Mungu.
for what renown [is it], if sinning and being battered, you endure [it]? But if, doing good and suffering [for it], you endure, this [is] grace with God,
21 Ninyi mliitwa kwa ajili ya haya, kwa sababu Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akiwaachia kielelezo, ili mzifuate nyayo zake.
for to this you were called, because Christ also suffered for you, leaving to you an example, that you may follow His steps,
22 “Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.”
who did not commit sin, nor was guile found in His mouth,
23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutishia, bali alijikabidhi kwa yeye ahukumuye kwa haki.
who being reviled—was not reviling again, suffering—was not threatening, and was committing Himself to Him who is judging righteously,
24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, ili tufe kwa mambo ya dhambi, bali tupate kuishi katika haki. Kwa kupigwa kwake, ninyi mmeponywa.
who Himself bore our sins in His body on the tree that having died to sins, we may live to righteousness; by whose stripes you were healed;
25 Kwa maana mlikuwa mmepotea kama kondoo, lakini sasa mmerudi kwa Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.
for you were as sheep going astray, but now you turned back to the Shepherd and Overseer of your souls.

< 1 Petro 2 >