< 1 Petro 2 >
1 Kwa hiyo, wekeni mbali nanyi uovu wote na udanganyifu wote, unafiki, wivu na masingizio ya kila namna.
Derfor aflægger al Ondskab og al Svig og Hykleri og Avind og al Bagtalelse,
2 Kama watoto wachanga, waliozaliwa sasa, yatamanini maziwa ya kiroho yasiyochanganywa na kitu kingine chochote, ili kwa hayo mpate kukua katika wokovu,
og higer som nyfødte Børn efter Ordets uforfalskede Mælk, for at I kunne vokse ved den til Frelse,
3 ikiwa kweli mmeonja ya kwamba Bwana ni mwema.
om I da have smagt, at Herren er god.
4 Mnapokuja kwake, yeye aliye Jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu bali kwa Mungu ni teule na la thamani kwake,
Kommer til ham, den levende Sten, der vel er forkastet af Menneskene, men er udvalgt og dyrebar for Gud,
5 ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mnajengwa kuwa nyumba ya kiroho, ili mpate kuwa ukuhani mtakatifu, mkitoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
og lader eder selv som levende Stene opbygge som et aandeligt Hus, til et helligt Præsteskab, til at frembære aandelige Ofre, velbehagelige for Gud ved Jesus Kristus.
6 Kwa maana imeandikwa katika Maandiko: “Tazama, naweka katika Sayuni, jiwe la pembeni teule lenye thamani, na yeyote atakayemwamini hataaibika kamwe.”
Thi det hedder i et Skriftsted: „Se, jeg lægger i Zion en Hovedhjørnesten, som er udvalgt og dyrebar; og den, som tror paa ham, skal ingenlunde blive til Skamme.”
7 Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hili ni la thamani. Lakini kwao wasioamini, “Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni,”
Eder altsaa, som tro, hører Æren til; men for de vantro er denne Sten, som Bygningsmændene forkastede, bleven til en Hovedhjørnesten og en Anstødssten og en Forargelses Klippe;
8 tena, “Jiwe lenye kuwafanya watu wajikwae, na mwamba wa kuwaangusha.” Wanajikwaa kwa sababu hawakulitii lile neno, kama walivyowekewa tangu zamani.
og de støde an, idet de ere genstridige imod Ordet, hvortil de ogsaa vare bestemte.
9 Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.
Men I ere en udvalgt Slægt, et kongeligt Præsteskab, et helligt Folk, et Folk til Ejendom, for at I skulle forkynde hans Dyder, som kaldte eder fra Mørke til sit underfulde Lys,
10 Mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni taifa la Mungu. Mwanzo mlikuwa hamjapata rehema, lakini sasa mmepata rehema.
I, som fordum ikke vare et Folk, men nu ere Guds Folk, I, som ikke fandt Barmhjertighed, men nu have fundet Barmhjertighed.
11 Wapenzi, ninawasihi, mkiwa kama wageni na wapitaji hapa ulimwenguni, epukeni tamaa mbaya za mwili ambazo hupigana vita na roho zenu.
I elskede! jeg formaner eder som fremmede og Udlændinge til at afholde eder fra kødelige Lyster, som jo føre Krig imod Sjælen,
12 Kuweni na mwenendo mzuri mbele ya watu wasiomjua Mungu, ili kama wanawasingizia kuwa watenda mabaya, wayaone matendo yenu mema nao wamtukuze Mungu siku atakapokuja kwetu.
saa I føre en god Vandel iblandt Hedningerne, for at de paa Grund af de gode Gerninger, som de faa at se, kunne prise Gud paa Besøgelsens Dag for det, som de bagtale eder for som Ugerningsmænd.
13 Kwa ajili ya Bwana, tiini kila mamlaka iliyowekwa na wanadamu: Kwa mfalme kwani ndiye aliye na mamlaka ya juu zaidi,
Underordner eder under al menneskelig Ordning for Herrens Skyld, være sig en Konge som den højeste,
14 au kwa maafisa aliowaweka, kwa kuwa mfalme amewatuma ili kuwaadhibu wale wanaokosa, na kuwapongeza wale watendao mema.
eller Landshøvdinger som dem, der sendes af ham til Straf for Ugerningsmænd, men til Ros for dem, som gøre det gode.
15 Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema mnyamazishe maneno ya kijinga ya watu wapumbavu.
Thi saaledes er det Guds Villie, at I ved at gøre det gode skulle bringe de uforstandige Menneskers Vankundighed til at tie;
16 Ishini kama watu huru, lakini msitumie uhuru wenu kama kisingizio cha kutenda uovu, bali ishini kama watumishi wa Mungu.
som frie, og ikke som de, der have Friheden til Ondskabs Skjul, men som Guds Tjenere.
17 Mheshimuni kila mtu ipasavyo: Wapendeni jamaa ya ndugu waumini, mcheni Mungu, mpeni heshima mfalme.
Ærer alle, elsker Broderskabet, frygter Gud, ærer Kongen!
18 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wema na wapole peke yao, bali pia wale walio wakali.
I Trælle! underordner eder under eders Herrer i al Frygt, ikke alene de gode og milde, men ogsaa de urimelige.
19 Kwa maana ni jambo la sifa kama mtu akivumilia anapoteswa kwa uonevu kwa ajili ya Mungu.
Thi dette finder Yndest, dersom nogen, bunden til Gud i sin Samvittighed, udholder Genvordigheder, skønt han lider uretfærdigt.
20 Kwani ni faida gani kwa mtu kustahimili anapopigwa kwa sababu ya makosa yake? Lakini kama mkiteswa kwa sababu ya kutenda mema, nanyi mkastahimili, hili ni jambo la kusifiwa mbele za Mungu.
Thi hvad Ros er det, om I holde ud, naar I synde og derfor faa Næveslag? Men dersom I holde ud, naar I gøre det gode og lide derfor, dette finder Yndest hos Gud.
21 Ninyi mliitwa kwa ajili ya haya, kwa sababu Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akiwaachia kielelezo, ili mzifuate nyayo zake.
Thi dertil bleve I kaldede, efterdi ogsaa Kristus har lidt for eder, efterladende eder et Forbillede, for at I skulle følge i hans Fodspor,
22 “Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.”
han, som ikke gjorde Synd, ikke heller blev der fundet Svig i hans Mund,
23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutishia, bali alijikabidhi kwa yeye ahukumuye kwa haki.
han, som ikke skældte igen, da han blev udskældt, ikke truede, da han led, men overgav det til ham, som dømmer retfærdigt,
24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, ili tufe kwa mambo ya dhambi, bali tupate kuishi katika haki. Kwa kupigwa kwake, ninyi mmeponywa.
han, som selv bar vore Synder paa sit Legeme op paa Træet, for at vi, afdøde fra vore Synder, skulle leve for Retfærdigheden, han, ved hvis Saar I ere blevne lægte.
25 Kwa maana mlikuwa mmepotea kama kondoo, lakini sasa mmerudi kwa Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.
Thi I vare vildfarende som Faar, men ere nu vendte om til eders Sjæles Hyrde og Tilsynsmand.