< 1 Petro 1 >
1 Petro, mtume wa Yesu Kristo: Kwa wateule wa Mungu, wageni katika ulimwengu, waliotawanyika kote katika Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia.
Peter, an apostle of Jesus Christ, to the sojourners scattered abroad in Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia, and Bithynia, chosen
2 Ni ninyi ambao mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba kulingana na alivyotangulia kuwajua, kupitia kwa kazi ya utakaso wa Roho, katika utiifu kwa Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake: Neema na amani ziwe kwenu kwa wingi.
according to the foreknowledge of God the Father and sanctified by the Spirit to be obedient to Jesus Christ and to be sprinkled with his blood: Grace and peace be multiplied to you.
3 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema zake kuu ametuzaa sisi mara ya pili katika tumaini lenye uzima kupitia kwa kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu,
Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ! In his great mercy he caused us to be born again to a living hope through the resurrection of Jesus Christ from the dead,
4 ili tuupate urithi usioharibika, usio na uchafu, ule usionyauka: uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu,
to an inheritance that is imperishable, undefiled, and unfading, reserved in heaven for you,
5 ninyi ambao mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani, hadi uje ule wokovu ulio tayari kufunuliwa nyakati za mwisho.
who by the power of God are being guarded through faith for a salvation ready to be revealed in the last time.
6 Katika hili mnafurahi sana, ingawa sasa kwa kitambo kidogo mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna nyingi.
In this you rejoice, even if now for a little while you have had to suffer various trials
7 Haya yamewajia ili kwamba imani yenu, iliyo ya thamani kuliko dhahabu ipoteayo, ingawa hujaribiwa kwa moto, ionekane kuwa halisi na imalizie katika sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atadhihirishwa.
so that the proven character of your faith—far more precious than gold that perishes even though it is tested by fire—may result in praise, honor, and glory when Jesus Christ is revealed.
8 Ingawa hamjamwona, mnampenda; tena ingawa sasa hammwoni, mnamwamini na kujawa na furaha isiyoneneka yenye utukufu usioelezeka.
Although you once did not know him, you love him; although you do not now see him, you believe in him and rejoice with an unspeakable and glorious joy,
9 Maana mnaupokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.
because you are receiving the end result of your faith—the salvation of your souls.
10 Kwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa,
Concerning this salvation, the prophets who prophesied about the grace that would come to you searched and carefully investigated,
11 wakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ule ambao ungefuata.
inquiring about the time and circumstances that the Spirit of Christ within them was indicating when he testified in advance to the sufferings of Christ and the glories that would follow.
12 Walidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.
It was revealed to them that they were not serving themselves, but you, in regard to the things that have now been announced to you through those who preached the gospel to you by the Holy Spirit sent from heaven. Even angels long to catch a glimpse of these things.
13 Kwa hiyo, tayarisheni nia zenu kwa kazi; mwe na kiasi, mkitumainia kikamilifu ile neema mtakayopewa Yesu Kristo atakapodhihirishwa.
Therefore, with minds that are alert and fully sober, set your hope completely on the grace that will be brought to you when Jesus Christ is revealed.
14 Kama watoto watiifu, msifuate tamaa zenu mbaya wakati mlipoishi kwa ujinga.
As children of obedience, do not conform yourselves to the evil desires you had when you lived in ignorance.
15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi kuweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.
But just as he who called you is holy, you also must be holy in all your conduct,
16 Kwa maana imeandikwa: “Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
for it is written, “Be holy, because I am holy.”
17 Kwa sababu mnamwita Baba ahukumuye kila mtu kulingana na matendo yake pasipo upendeleo, enendeni kwa hofu ya kumcha Mungu wakati wenu wa kukaa hapa duniani kama wageni.
If you call on the Father who judges without partiality according to each person's work, pass the time of your sojourn in reverent fear.
18 Kwa maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutoka mwenendo wenu usiofaa ambao mliurithi kutoka kwa baba zenu, si kwa vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu,
For you know that you were redeemed from the empty way of life handed down to you from your fathers, not with perishable things like silver or gold,
19 bali kwa damu ya thamani ya Kristo, yule Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa.
but with the precious blood of Christ, a lamb without blemish or spot.
20 Yeye alichaguliwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
He was foreknown before the foundation of the world, but was revealed in the last times for your sake.
21 Kupitia kwake mmemwamini Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu na akampa utukufu, ili imani yenu na tumaini lenu ziwe kwa Mungu.
Through him you believe in God, who raised him from the dead and gave him glory, so that your faith and hope might be in God.
22 Basi kwa kuwa mmejitakasa nafsi zenu kwa kuitii ile kweli hata mkawa na upendo wa ndugu usio na unafiki, basi pendaneni kwa dhati kutoka moyoni.
Since you have purified your souls by your obedience to the truth through the Spirit, resulting in genuine brotherly love, love one another deeply, from a pure heart.
23 Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. (aiōn )
For you have been born again, not of perishable seed but of imperishable, through the word of God that lives and abides forever. (aiōn )
24 Maana, “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao ni kama maua ya kondeni; majani hunyauka na maua huanguka,
For, “All flesh is like grass, and all the glory of man is like a flower of grass. The grass withers, and its flower falls,
25 lakini neno la Bwana ladumu milele.” Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu. (aiōn )
but the word of the Lord endures forever.” This word is the good news that was preached to you. (aiōn )