< 1 Petro 1 >
1 Petro, mtume wa Yesu Kristo: Kwa wateule wa Mungu, wageni katika ulimwengu, waliotawanyika kote katika Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithinia.
Peter, an apostle of Jesus Christ, to the elect who are sojourners of the dispersion in Pontus, Galatia, Cappadocia, Roman Asia, and Bithynia,
2 Ni ninyi ambao mlichaguliwa tangu mwanzo na Mungu Baba kulingana na alivyotangulia kuwajua, kupitia kwa kazi ya utakaso wa Roho, katika utiifu kwa Yesu Kristo na kunyunyiziwa damu yake: Neema na amani ziwe kwenu kwa wingi.
according to the foreknowledge of God the Father, in the sanctification of the spirit, unto obedience and sprinkling of the blood of Jesus Christ; Grace and peace be multiplied to you.
3 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa rehema zake kuu ametuzaa sisi mara ya pili katika tumaini lenye uzima kupitia kwa kufufuka kwa Yesu Kristo kutoka kwa wafu,
Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, by whose great mercy we have been born anew into a living hope, through the resurrection of Jesus Christ from the dead;
4 ili tuupate urithi usioharibika, usio na uchafu, ule usionyauka: uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu,
and into an inheritance imperishable and undefiled and fadeless, which has been kept in heaven for you
5 ninyi ambao mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani, hadi uje ule wokovu ulio tayari kufunuliwa nyakati za mwisho.
who, through faith, are continuously guarded by the power of God for a salvation, ready to be revealed in the last days.
6 Katika hili mnafurahi sana, ingawa sasa kwa kitambo kidogo mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna nyingi.
Exult in this, though now for a brief moment, if need be, you have suffered many hardships.
7 Haya yamewajia ili kwamba imani yenu, iliyo ya thamani kuliko dhahabu ipoteayo, ingawa hujaribiwa kwa moto, ionekane kuwa halisi na imalizie katika sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atadhihirishwa.
These are in order that the test of your faith, more precious than gold that is perishable and yet is tested by fire, may redound to praise and glory and honor, at the revelation of Jesus Christ.
8 Ingawa hamjamwona, mnampenda; tena ingawa sasa hammwoni, mnamwamini na kujawa na furaha isiyoneneka yenye utukufu usioelezeka.
Him you love, though you have never seen him; in him you ever believe, though even now you see him not, and you are rejoicing with joy unspeakable and full of glory,
9 Maana mnaupokea wokovu wa roho zenu, ambao ndio lengo la imani yenu.
as you continually receive the reward of your faith, even the salvation of your souls.
10 Kwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa,
Concerning this salvation the Prophets who prophesied regarding the grace intended for you, diligently sought and searched.
11 wakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ule ambao ungefuata.
They were searching to know to what time, or to what manner of time the Spirit of Christ which was in them kept pointing, when he ever testified beforehand concerning the sufferings of Christ and the glories that would follow.
12 Walidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.
It was revealed to them that it was not for themselves, but for you, that they were ministering the truths which have now been announced to you, by those who preached the gospel to you, through the help of the Holy Spirit sent forth from heaven - truths into which angels long to look.
13 Kwa hiyo, tayarisheni nia zenu kwa kazi; mwe na kiasi, mkitumainia kikamilifu ile neema mtakayopewa Yesu Kristo atakapodhihirishwa.
So then brace up your minds, be steady in spirit, and fix your hope firmly in the grace that is coming to you, at the revelation of Jesus Christ.
14 Kama watoto watiifu, msifuate tamaa zenu mbaya wakati mlipoishi kwa ujinga.
Like obedient children, do not fashion yourselves according to the former passions of your days of ignorance,
15 Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi kuweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.
but become yourselves holy in your whole manner of living, as He who has called you is holy,
16 Kwa maana imeandikwa: “Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
as the Scripture says, You shall be holy, because I am holy.
17 Kwa sababu mnamwita Baba ahukumuye kila mtu kulingana na matendo yake pasipo upendeleo, enendeni kwa hofu ya kumcha Mungu wakati wenu wa kukaa hapa duniani kama wageni.
And since you call upon him as Father, who impartially judges each one according to his deeds, pass the time of your sojourning here in reverence.
18 Kwa maana mnafahamu kwamba mlikombolewa kutoka mwenendo wenu usiofaa ambao mliurithi kutoka kwa baba zenu, si kwa vitu viharibikavyo kama fedha na dhahabu,
For you well know that not with perishable things, with silver or gold, were you redeemed from the emptiness of your manner of life, received by tradition from your ancestors;
19 bali kwa damu ya thamani ya Kristo, yule Mwana-Kondoo asiye na dosari wala doa.
but with precious blood, like that of a lamb without spot or blemish, even the blood of Christ.
20 Yeye alichaguliwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, lakini akadhihirishwa katika siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
He was indeed foreknown before the foundation of the world, but was manifested at the end of the times for your sake.
21 Kupitia kwake mmemwamini Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu na akampa utukufu, ili imani yenu na tumaini lenu ziwe kwa Mungu.
Through him you believe in God who raised him from the dead and gave him glory; so that your faith and hope are now in God.
22 Basi kwa kuwa mmejitakasa nafsi zenu kwa kuitii ile kweli hata mkawa na upendo wa ndugu usio na unafiki, basi pendaneni kwa dhati kutoka moyoni.
Now that by obedience to the truth you have purified your lives for a brotherly love without hypocrisy, you must love one another from your hearts, fervently.
23 Kwa maana mmezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika, kupitia kwa neno la Mungu lililo hai na linalodumu milele. (aiōn )
For you have been born anew, not of perishable, but of imperishable seed, by the living, lasting word of God. (aiōn )
24 Maana, “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao ni kama maua ya kondeni; majani hunyauka na maua huanguka,
For, All flesh is grass And all its glory like the flower of the grass. The grass fades, The flower falls,
25 lakini neno la Bwana ladumu milele.” Hili ndilo neno lililohubiriwa kwenu. (aiōn )
But the word of the Lord abides forever. And this is the word of the gospel which has been told to you. (aiōn )