< 1 Wafalme 8 >
1 Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Potem je Salomon zbral Izraelove starešine in vse poglavarje rodov, vodilne izmed očetov Izraelovih otrok, h kralju Salomonu v Jeruzalem, da bi lahko prinesli gor skrinjo Gospodove zaveze iz Davidovega mesta, ki je Sion.
2 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.
Vsi možje iz Izraela so se na praznik zbrali h kralju Salomonu, v mesecu etanímu, ki je sedmi mesec.
3 Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano,
Prišli so vsi Izraelovi starešine in duhovniki so dvignili skrinjo.
4 nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba,
Gor so prinesli Gospodovo skrinjo, šotorsko svetišče skupnosti shoda in vse svete posode, ki so bile v šotorskem svetišču, celo te so duhovniki in Lévijevci prinesli gor.
5 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
Kralj Salomon in vsa Izraelova skupnost, ki je bila zbrana k njemu, so bili z njim pred skrinjo. Žrtvovali so ovce in vole, ki se jih zaradi množice ni dalo ne povedati ne prešteti.
6 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
Duhovniki so skrinjo Gospodove zaveze prinesli na njeno mesto, v hišni orakelj, k najsvetejšemu kraju, celo pod peruti kerubov.
7 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea.
Kajti keruba sta svoji dve peruti razprostirala nad prostorom skrinje in keruba sta od zgoraj pokrivala skrinjo in njena drogova.
8 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
Drogova so izvlekli, da sta se konca drogov videla iz svetega kraja pred orakljem, odzunaj pa nista bila vidna in tam sta do današnjega dne.
9 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
V skrinji ni bilo ničesar razen dveh kamnitih plošč, ki ju je Mojzes položil tja pri Horebu, ko je Gospod sklenil zavezo z Izraelovi otroci, ko so prišli iz egiptovske dežele.
10 Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana.
Pripetilo se je, ko so duhovniki prišli ven iz svetega kraja, da je oblak napolnil Gospodovo hišo,
11 Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.
tako da duhovniki zaradi oblaka niso mogli stati, da bi služili, kajti Gospodova slava je napolnila Gospodovo hišo.
12 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;
Potem je spregovoril Salomon: » Gospod je rekel, da bo prebival v gosti temi.
13 naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”
Zagotovo sem ti zgradil hišo, da prebivaš v njej, ustaljen kraj zate, da v njem prebivaš na veke.«
14 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
Kralj je obrnil svoj obraz naokrog in blagoslovil vso Izraelovo skupnost (in vsa Izraelova skupnost je stala)
15 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
in rekel je: »Blagoslovljen bodi Gospod, Izraelov Bog, ki je s svojimi usti spregovoril mojemu očetu Davidu in je to izpolnil s svojo roko, rekoč:
16 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
›Od dneva, ko sem svoje ljudstvo Izraela privedel ven iz Egipta, nisem izbral nobenega mesta izmed vseh Izraelovih rodov, da bi zgradil hišo, da bi bilo v njej lahko moje ime, temveč sem izbral Davida, da bo nad mojim ljudstvom Izraelom.‹
17 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
To je bilo na srcu mojega očeta Davida, da zgradi hišo za ime Gospoda, Izraelovega Boga.
18 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
Gospod je rekel mojemu očetu Davidu: ›Medtem ko je bilo to v tvojem srcu, da zgradiš hišo mojemu imenu, si storil dobro, da je bilo to v tvojem srcu.
19 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Vendar pa hiše ne boš gradil ti, temveč tvoj sin, ki bo izšel iz tvojih ledij, on bo zgradil hišo mojemu imenu.‹
20 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Gospod je izpolnil svojo besedo, ki jo je govoril in dvignjen sem bil na položaj svojega očeta Davida in sedim na Izraelovem prestolu, kakor je obljubil Gospod in zgradil sem hišo za ime Gospoda, Izraelovega Boga.
21 Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”
Tam sem pripravil prostor za skrinjo, v kateri je Gospodova zaveza, ki jo je on sklenil z našimi očeti, ko jih je privedel ven iz egiptovske dežele.«
22 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni
Salomon je stal pred Gospodovim oltarjem v prisotnosti vse Izraelove skupnosti in svoji roki razširil proti nebu
23 na kusema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
in rekel: » Gospod, Izraelov Bog, ni Boga, podobnega tebi, na nebu zgoraj ali na zemlji spodaj, ki ohranjaš zavezo in usmiljenje s svojimi služabniki, ki z vsem svojim srcem hodijo pred teboj,
24 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
ki si svojemu služabniku Davidu, mojemu očetu, ohranil to, kar si mu obljubil. Govoril si s svojimi usti in si to tudi izpolnil s svojo roko, kakor je to ta dan.
25 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
Zato zdaj Gospod, Izraelov Bog, ohrani s svojim služabnikom Davidom, mojim očetom, to, kar si mu obljubil, rekoč: ›Ne bo ti zmanjkalo moža v mojem pogledu, da bi sedel na Izraelovem prestolu; samo da tvoji otroci pazijo na svojo pot, da hodijo pred menoj, kakor si ti hodil pred menoj.‹
26 Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
Sedaj, oh Izraelov Bog, naj bo tvoja beseda, prosim te, resnična, ki si jo govoril svojemu služabniku, mojemu očetu Davidu.
27 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
Toda ali bo Bog zares prebival na zemlji? Glej, nebo in nebesa nebes te ne morejo obseči, kako veliko manj ta hiša, ki sem jo zgradil?
28 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
Vendar se ozri na molitev svojega služabnika in k njegovi ponižni prošnji, oh Gospod, moj Bog, da prisluhneš klicu in molitvi, ki jo ta dan tvoj služabnik moli pred teboj,
29 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
da bodo tvoje oči lahko ponoči in podnevi odprte proti tej hiši, torej proti kraju, o katerem si rekel: ›Moje ime bo tam, ‹ da boš lahko prisluhnil molitvi, ki jo bo tvoj služabnik naredil k temu kraju.
30 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
Prisluhni ponižni prošnji svojega služabnika in svojega ljudstva Izraela, ko bodo molili k temu kraju. Pozorno poslušaj v nebesih, svojem prebivališču. In ko si pozorno slišal, odpusti.
31 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
Če se katerikoli človek prekrši zoper svojega bližnjega in je nanj položena prisega, da mu povzroči, da priseže in prisega pride pred tvoj oltar v tej hiši,
32 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
potem pozorno poslušaj v nebesih, ukrepaj in sodi svoja služabnika, obsodi zlobnega, da privedeš njegovo pot na njegovo glavo in opraviči pravičnega, da mu daš glede na njegovo pravičnost.
33 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
Ko bo tvoje ljudstvo Izrael udarjeno pred sovražnikom, ker so grešili zoper tebe in se bo ponovno obrnilo k tebi, priznalo tvoje ime, molilo in naredilo ponižno prošnjo k tebi v tej hiši,
34 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
potem pozorno poslušaj v nebesih in odpusti greh svojega ljudstva Izraela in jih ponovno privedi v deželo, ki jo daješ njihovim očetom.
35 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
Ko je nebo zaprto in ni dežja, ker so grešili zoper tebe; če molijo k temu kraju in priznajo tvoje ime in se obrnejo od svojega greha, ko si jih ti prizadel,
36 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
potem pozorno poslušaj v nebesih in odpusti greh svojih služabnikov in svojega ljudstva Izraela, da jih naučiš dobro pot, po kateri naj bi hodili in jim daš dež na svojo deželo, ki si jo dal svojemu ljudstvu v dediščino.
37 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
Če bo v deželi lakota, če bo kužna bolezen, kvarjenje, plesen, leteča kobilica ali če bo tam gosenica; če jih njihov sovražnik oblega v deželi njihovih mest, kakršnakoli nadloga, kakršnakoli bolezen bo,
38 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili:
kakršnokoli molitev in ponižno prošnjo bo naredil katerikoli človek ali vse tvoje ljudstvo Izrael, ki bo spoznal, vsak mož nadlogo svojega lastnega srca in bo svoje roke razširil proti tej hiši,
39 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
potem pozorno poslušaj v nebesih, svojem prebivališču, odpusti, ukrepaj in daj vsakemu možu glede na njegove poti, čigar srce poznaš (kajti ti, celó le ti, poznaš srca vseh človeških otrok),
40 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
da se te bodo lahko bali vse dni, ki jih živijo v deželi, ki si jo dal našim očetom.
41 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako,
Poleg tega glede tujca, ki ni iz tvojega ljudstva Izraela, temveč zaradi tvojega imena prihaja iz daljne dežele
42 kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili,
(kajti slišali bodo o tvojem velikem imenu, o tvoji močni roki in o tvojem iztegnjenem laktu), ko bo prišel in molil k tej hiši,
43 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
pozorno poslušaj v nebesih, svojem bivališču in ukrepaj glede na vse, za kar bo tujec klical k tebi, da bo vse ljudstvo zemlje lahko spoznalo tvoje ime, da se te boji, kakor to dela tvoje ljudstvo Izrael in da bodo lahko vedeli, da je ta hiša, ki sem jo zgradil, imenovana po tvojem imenu.
44 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
Če gre tvoje ljudstvo ven na bitko zoper svojega sovražnika, kamorkoli jih boš poslal in bodo molili h Gospodu, k mestu, ki si ga ti izbral in k hiši, ki sem jo zgradil za tvoje ime,
45 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
potem pozorno poslušaj v nebesih njihovo molitev, njihovo ponižno prošnjo in obravnavaj njihov primer.
46 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu;
Če grešijo zoper tebe (kajti tam ni človeka, ki ne greši) in si jezen nanje in jih izročiš sovražniku, tako da jih odvedejo ujetnike v deželo sovražnika, daleč ali blizu,
47 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’;
vendar če si bodo premislili v deželi, kamor so bili odvedeni ujeti in se pokesajo in naredijo ponižno prošnjo k tebi, v deželi tistih, ki so jih odvedli ujete, rekoč: ›Grešili smo in storili pokvarjeno, zagrešili smo zlobnost‹
48 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako;
in se tako vrnejo k tebi z vsem svojim srcem in z vso svojo dušo v deželi svojih sovražnikov, ki so jih odvedli ujete in molijo k tebi, k svoji deželi, ki si jo dal njihovim očetom, mestu, ki si ga ti izbral in hiši, ki sem jo zgradil za tvoje ime,
49 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao.
potem pozorno poslušaj njihovo molitev in njihovo ponižno prošnjo v nebesih, svojem prebivališču in obravnavaj njihov primer
50 Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma;
in odpusti svojemu ljudstvu, ker so grešili zoper tebe in vse njihove prestopke, s katerimi so se prekršili zoper tebe in jim daj sočutje pred tistimi, ki so jih odvedli ujete, da bodo lahko imeli sočutje do njih,
51 kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.
kajti oni so tvoje ljudstvo in tvoja dediščina, ki si jo privedel iz Egipta, iz srede železne talilne peči,
52 “Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia.
da bodo tvoje oči lahko odprte k ponižni prošnji tvojega služabnika in k ponižni prošnji tvojega ljudstva Izraela, da jim prisluhneš v vsem, v čemer kličejo k tebi.
53 Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”
Kajti oddvojil si jih izmed vsega zemeljskega ljudstva, da bi bili tvoja dediščina, kakor si govoril po roki svojega služabnika Mojzesa, ko si naše očete privedel iz Egipta, oh Gospod Bog.«
54 Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni.
Bilo je tako, ko je Salomon nehal moliti vso to molitev in ponižno prošnjo h Gospodu, da je vstal izpred Gospodovega oltarja od klečanja na svojih kolenih, s svojima rokama, razširjenima k nebu.
55 Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:
Vstal je in z močnim glasom blagoslovil vso Izraelovo skupnost, rekoč:
56 “Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose.
»Blagoslovljen bodi Gospod, ki je svojemu ljudstvu Izraelu dal počitek, glede na vse, kar je obljubil. Niti ena beseda ni manjkala od vse njegove dobre obljube, ki jo je obljubil po roki svojega služabnika Mojzesa.
57 Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa.
Gospod, naš Bog, naj bo z nami, kakor je bil z našimi očeti. Naj nas ne pusti niti naj nas ne zapusti,
58 Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu.
da bo lahko naša srca nagnil k sebi, da hodimo po vseh njegovih poteh in da ohranjamo vse njegove zapovedi, njegove zakone in njegove sodbe, ki jih je zapovedal našim očetom.
59 Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku,
Naj bodo te moje besede, s katerimi sem naredil ponižno prošnjo pred Gospodom, blizu Gospodu, našemu Bogu, podnevi in ponoči, da ohrani zadevo svojega služabnika in zadevo svojega ljudstva Izraela ob vseh časih, kakor bo stvar zahtevala,
60 ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine.
da bo vse ljudstvo zemlje lahko vedelo, da Gospod je Bog in da tam ni nobenega drugega.
61 Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”
Naj bo vaše srce torej popolno z Gospodom, našim Bogom, da se ravna po njegovih zakonih in da ohranja njegove zapovedi, kakor je ta dan.«
62 Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana.
Kralj in ves Izrael z njim je daroval klavno daritev pred Gospodom.
63 Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.
Salomon je daroval žrtvovanje mirovnih daritev, ki jih je daroval Gospodu, dvaindvajset tisoč volov in sto dvajset tisoč ovc. Tako so kralj in vsi Izraelovi otroci posvetili Gospodovo hišo.
64 Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.
Istega dne je kralj posvetil sredino dvora, ki je bila pred Gospodovo hišo, kajti tam je daroval žgalne daritve, jedilne daritve in tolščo mirovnih daritev, ker je bil bronast oltar, ki je bil pred Gospodom, premajhen, da sprejme žgalne daritve, jedilne daritve in tolščo mirovnih daritev.
65 Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne.
Ob tistem času je Salomon priredil praznovanje in ves Izrael z njim, velika skupnost, od vhoda v Hamát do egiptovske reke, pred Gospodom, svojim Bogom, sedem dni in sedem dni, torej štirinajst dni.
66 Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.
Na osmi dan je ljudstvo odposlal proč in blagoslovili so kralja in radostni in veselega srca zaradi vse dobrote, ki jo je Gospod storil za svojega služabnika Davida in za svoje ljudstvo Izrael, odšli k svojim šotorom.