< 1 Wafalme 8 >
1 Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Then Solomon assembled the elders of Israel, all the heads of the tribes, and the leaders of the families of the people of Israel, before himself in Jerusalem, to bring up the ark of the covenant of Yahweh from the city of David, that is, Zion.
2 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.
All the men of Israel assembled before King Solomon at the feast, in the month of Ethanim, which is the seventh month.
3 Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano,
All the elders of Israel came, and the priests took up the ark.
4 nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba,
They brought up the ark of Yahweh, the tent of meeting, and all the holy furnishings that were in the tent. The priests and the Levites brought these things up.
5 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
King Solomon and all the assembly of Israel came together before the ark, sacrificing sheep and oxen that could not be counted.
6 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
The priests brought in the ark of the covenant of Yahweh to its place, into the inner room of the house, to the most holy place, under the wings of the cherubim.
7 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea.
For the cherubim spread out their wings to the place of the ark, and they covered the ark and the poles by which it was carried.
8 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
The poles were so long that their ends were seen from the holy place in front of the inner room, but they could not be seen from outside. They are there to this day.
9 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
There was nothing in the ark except the two tablets of stone that Moses had put there at Horeb, when Yahweh made a covenant with the people of Israel when they came out of the land of Egypt.
10 Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana.
It came about that when the priests came out of the holy place, the cloud filled the temple of Yahweh.
11 Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.
The priests could not stand to serve because of the cloud, for the glory of Yahweh filled his house.
12 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;
Then Solomon said, “Yahweh has said that he would live in thick darkness,
13 naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”
But I have built you a lofty residence, a place for you to live in forever.”
14 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
Then the king turned around and blessed all the assembly of Israel, while all the assembly of Israel was standing.
15 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
He said, “May Yahweh, the God of Israel, be praised, who spoke to David my father, and has fulfilled it with his own hands, saying,
16 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
'Since the day that I brought my people Israel out of Egypt, I chose no city out of all the tribes of Israel in which to build a house, in order for my name to be there. However, I chose David to rule over my people Israel.'
17 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Now it was in the heart of David my father to build a house for the name of Yahweh, the God of Israel.
18 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
But Yahweh said to David my father, 'In that it was in your heart to build a house for my name, you did well for it to be in your heart.
19 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Nevertheless you will not build the house; instead, your son, one who will be born from your loins, will build the house for my name.'
20 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Yahweh has carried out the word that he had said, for I have arisen in the place of David my father, and I sit on the throne of Israel, as Yahweh promised. I have built the house for the name of Yahweh, the God of Israel.
21 Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”
I have made a place for the ark there, in which is Yahweh's covenant, which he made with our fathers when he brought them out of the land of Egypt.”
22 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni
Solomon stood before the altar of Yahweh, before all the assembly of Israel, and spread out his hands toward the heavens.
23 na kusema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
He said, “Yahweh, God of Israel, there is no God like you in the heavens above or on the earth below, who keeps his covenant faithfulness with your servants who walk before you with all their heart;
24 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
you who have kept with your servant David my father, what you promised him. Yes, you spoke with your mouth and have fulfilled it with your hand, as it is today.
25 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
Now then, Yahweh, God of Israel, carry out what you have promised to your servant David my father, when you said, 'You will not fail to have a man in my sight to sit on the throne of Israel, if only your descendants are careful to walk before me, as you have walked before me.'
26 Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
Now then, God of Israel, let your word be confirmed, which you have spoken to your servant David my father.
27 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
But will God actually live on the earth? Look, the entire universe and heaven itself cannot contain you—how much less can this temple that I have built!
28 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
Yet please respect this prayer of your servant and his request, Yahweh my God; listen to the cry and prayer that your servant prays before you today.
29 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
May your eyes be open toward this temple night and day, to the place about which you have said, 'My name and my presence will be there'—in order to listen to the prayers that your servant will pray toward this place.
30 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
So listen to the request of your servant and of your people Israel when we pray toward this place. Yes, listen from the place where you live, from the heavens; and when you listen, forgive.
31 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
If a man sins against his neighbor and is required to swear an oath, and if he comes and swears an oath before your altar in this house,
32 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
listen from the heavens and act. Judge your servants, condemning the guilty and bringing what he has done upon his own head. Declare the innocent not guilty and give to him according to his righteousness.
33 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
When your people Israel are defeated by an enemy because they have sinned against you, if they turn back to you, confess your name, pray, and request forgiveness from you in this temple—
34 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
then please listen in the heavens and forgive the sin of your people Israel; bring them back to the land that you gave to their ancestors.
35 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
When the skies are shut up and there is no rain because the people have sinned against you—if they pray toward this place, confess your name, and turn from their sin when you have afflicted them—
36 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
then listen in heaven and forgive the sin of your servants and of your people Israel, when you teach them the good way in which they should walk. Send rain on your land, which you have given to your people as an inheritance.
37 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
Suppose there is famine in the land, or suppose that there is disease, blight or mildew, locusts or caterpillars; or suppose that an enemy attacks the city gates in their land, or that there is any plague or sickness—
38 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili:
and suppose then that prayers and requests are made by a person or by all your people Israel—each knowing the plague in his own heart as he spreads out his hands toward this temple.
39 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
Then listen from heaven, the place where you live, forgive and act, and reward every person for all he does; you know his heart, because you and you only know the hearts of all human beings.
40 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
Do this so that they may fear you all the days that they live on the land that you gave to our ancestors.
41 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako,
In addition, concerning the foreigner who does not belong to your people Israel: When he comes from a distant country because of your name—
42 kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili,
for they will hear of your great name, your mighty hand, and your raised arm—when he comes and prays toward this temple,
43 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
then please listen from heaven, the place where you live, and do whatever the foreigner asks of you. Do this so that all the peoples on earth may know your name and fear you, as do your own people Israel. Do this so they might know that this house I have built is called by your name.
44 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
Suppose that your people go out to battle against an enemy, by whatever way you may send them, and suppose that they pray to you, Yahweh, toward the city that you have chosen, and toward the house that I have built for your name.
45 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
Then listen in the heavens to their prayer and their request, and help their cause.
46 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu;
Suppose that they sin against you, since there is no one who does not sin, and suppose that you are angry with them and deliver them to the enemy, so that the enemy takes them away captive to their land, whether distant or near.
47 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’;
Then suppose that they realize they are in the land where they have been exiled, and suppose that they repent and seek favor from you from the land of their captors. Suppose that they say, 'We have acted perversely and sinned. We have behaved wickedly.'
48 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako;
Suppose that they return to you with all their heart and with all their soul in the land of their enemies who captured them, and suppose that they pray to you toward their land, which you gave to their ancestors, and toward the city that you chose, and toward the house that I have built for your name.
49 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao.
Then from heaven, the place where you live, listen to their prayer and their request for help, and you will make matters right for them.
50 Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma;
Forgive your people who have sinned against you, and all their transgressions that they have committed against you, and make them objects of compassion before their conquerors, and cause their conquerors to have compassion on them.
51 kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.
They are your people whom you have chosen, whom you rescued out of Egypt as if from the middle of a furnace where iron is forged.
52 “Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia.
May your eyes be open to the request of your servant and to the requests of your people Israel, to listen to them whenever they cry to you.
53 Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”
For you separated them from among all the peoples of the earth to belong to you and receive your promises, just as you explained by Moses your servant, when you brought our fathers out of Egypt, Lord Yahweh.”
54 Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni.
So it was that when Solomon had finished praying all this prayer and request to Yahweh, he arose from before the altar of Yahweh, from kneeling on his knees with his hands spread out toward the heavens.
55 Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:
He stood and blessed all the assembly of Israel in a loud voice, saying,
56 “Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose.
“May Yahweh be praised, who has given rest to his people Israel, keeping all his promises. Not one word has failed out of all Yahweh's good promises that he made with Moses his servant.
57 Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa.
May Yahweh our God be with us, as he was with our ancestors. May he never leave us or forsake us,
58 Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu.
that he may incline our hearts to him, to live in all his ways and keep his commandments and his regulations and his statutes, which he commanded our fathers.
59 Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku,
Let these words I have spoken, by which I have made request before Yahweh, be near Yahweh our God day and night, so that he may help the cause of his servant and the cause of his people Israel, as every day will require;
60 ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine.
that all the peoples of the earth may know that Yahweh, he is God, and there is no other God!
61 Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”
Therefore let your heart be true to Yahweh our God, to walk in his statutes and keep his commandments, as on this day.”
62 Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana.
So the king and all Israel with him offered sacrifices to Yahweh.
63 Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.
Solomon offered a sacrifice of fellowship offerings to Yahweh: twenty-two thousand oxen and 120,000 sheep. So the king and all the people of Israel dedicated the house of Yahweh.
64 Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.
The same day the king set apart the middle of the courtyard in front of the temple of Yahweh, for there he offered the burnt offerings, the grain offerings, and the fat of the fellowship offerings, because the bronze altar that was before Yahweh was too small to receive the burnt offering, the grain offerings, and the fat of the fellowship offerings.
65 Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne.
So Solomon held the feast at that time, and all Israel with him, a great assembly, from Lebo Hamath to the brook of Egypt, before Yahweh our God for seven days and also for another seven days, a total of fourteen days.
66 Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.
On the eighth day he sent the people away, and they blessed the king and went to their homes with joyful and glad hearts for all the goodness that Yahweh had shown to David, his servant, and to Israel, his people.