< 1 Wafalme 8 >
1 Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Solomon ni Isarel kacuenaw hoi miphun a lû lah la kaawmnaw hai Isarel catoun imthungkhu tongpanaw hah Devit khopui Zion hoi Bawipa thingkong kâkayawt hanelah Jerusalem e siangpahrang Solomon koevah ceikhai hanelah a pâkhueng awh.
2 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.
Hatdawkvah, Isarelnaw pueng teh, Ethanim thapa yung sari nah, pawi dawk siangpahrang Solomon koevah a kamkhueng awh.
3 Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano,
Isarel kacuenaw pueng ni a tho awh teh, vaihmanaw ni BAWIPA thingkong hah a la awh.
4 nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba,
BAWIPA e thingkong teh, kamkhuengnae hoi bawknae rim dawk e kathounge hlaamnaw pueng hah a la awh teh, vaihma hoi Levihnaw ni a ceikhai awh.
5 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
Siangpahrang Solomon hoi ahni koe kamkhuengnaw Isarel maya pueng hah thingkong hmalah ao awh teh, tu hoi maitotan apap lawi touklek thai hoeh e hoi panue thai hoeh totouh thuengnae hah a sak awh.
6 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
Hahoi vaihmanaw ni, Bawipa lawkkam thingkong a onae hmuen bawkim thung athung patuen hmuen kathoung thung vah, cherubim a rathei kadai e rahim vah hmuen kathoungpounge hmuen koe a kâenkhai awh.
7 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea.
Cherubim ni a rathei kahni touh hah thingkong onae lathueng a kadai teh, cherubim ni thingkong hoi kâkayawtnae acung hah a ramuk.
8 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
Kâkayawtnae acung a saw poung dawkvah, athung patuen hmuen kathoung koehoi a kâhmu thai han eiteh, alawilah hoi kâhmawt thai hoeh. Sahnin totouh hawvah ao.
9 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
Izip ram hoi a tâco awh teh, BAWIPA ni Isarel catounnaw koe lawkkamnae a sak navah, Mosi ni Horeb mon dawk e lungphen kahni touh a la e hloilah thingkong thung banghai awm hoeh.
10 Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana.
Hahoi vaihmanaw hmuen kathoung koehoi a tâco awh toteh, BAWIPA im teh tâmai muen a kawi.
11 Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.
Tâmai kecu dawk vaihma ni thaw kahawicalah tawk thai hoeh. Bangkongtetpawiteh, BAWIPA bawilennae hoi BAWIPA im muen akawi.
12 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;
Solomon ni lawk a dei e teh, kathapoung e tâmai dawk ka o han telah BAWIPA ni a ti.
13 naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”
A yungyoe na onae hmuen tawmrasang e im teh, ka sak pouh katang toe telah a ti.
14 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
Kamkhueng e Isarelnaw pueng ni a kangdue awh teh, siangpahrang ni a hnuklah a kamlang teh. ka kamkhueng e Isarelnaw pueng hah yawhawi a poe.
15 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
Ahni ni Isarel BAWIPA Cathut, apa Devit koevah, amae pahni dawk hoi roeroe vah, Izip ram hoi ka tami Isarel ka tâcokhai nah hnin hoi Isarel miphunnaw thung dawk nâ lahai ka min ao nahane im sak hanlah rawi boihoeh.
16 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
Hatei ka tami Isarel kaukkung hanlah, Devit heh ka rawi e doeh telah kadeikung ama kut dawk hoi roeroe ka kuepsakkung teh pholen lah awm seh.
17 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Apa Devit niyah Isarel BAWIPA min lahoi im sak hanlah a lungthung hoi pou a noe.
18 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
Hatei BAWIPA ni apa Devit koevah, na lungthin hoi ka min hanlah im sak hane ouk na noe e lungthin na tawn e hah ahawi.
19 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Hatei, nang ni teh im na sak mahoeh. Hatei, na capa nange cati dawk hoi ka tâcawt e ni ka min hanlah im teh a sak han telah ati toe.
20 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
BAWIPA ni a kam tangcoung e hah a caksak teh, BAWIPA e a kam e patetlah apa Devit e hmuen teh ka coe teh, Isarel bawitungkhung dawk ka tahung teh, Isarel BAWIPA Cathut min hanlah, im teh ka sak toe.
21 Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”
Hawvah, thingkong o nahane hmuen lah ka pouk teh, hawvah, Izip ram hoi a tâcokhai navah, mintoenaw koe a kam e BAWIPA lawkkam ao telah a ti.
22 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni
Solomon teh BAWIPA koe thuengnae khoungroe hmalah vah, kamkhueng e Isarelnaw pueng ni a hmunae koe a kangdue teh, kalvan lah a kut hah a dâw teh,
23 na kusema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
Isarel BAWIPA Cathut kalvan hai thoseh, talai thung hai thoseh, a lungthin abuemlah na hmalah kahawicalah kaawm e naw koevah, lawkkam hoi pahrennae kakuepsakkung nang patet lae Cathut awm hoeh.
24 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
Na san apa Devit koevah, lawk na kam e hah na pahnim hoeh teh, na pahni hoi na dei e hah na kut hoi na kuepsak. Sahnin totouh nama paroup lah na o.
25 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
Hatdawkvah, Isarel BAWIPA Cathut, na san apa Devit koevah, na capanaw ni a hringnae nuencang kâhruetcuet teh, ka mithmu vah, hring awh pawiteh, ka hmaitung vah Isarel bawitungkhung dawk ka tahung hane vout mahoeh na ti telah na kam e hah kuep sak haw.
26 Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
Oe Isarel Cathut, na san Devit koevah na dei e kuep sak haw telah ka ratoum.
27 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
Hatei Cathut nang teh, talai van kho na ka sak han tangngak na maw. Khenhaw, kalvan hoi kalvannaw dawk patenghai na ka cawng hoeh e, hete ka sak e im dawkvah, banghloimaw cawng laipalah hoe ao han vai.
28 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
Hatei Oe BAWIPA Cathut, sahnin vah na san ni na kaw e hoi ka ratoumnae hoi ka dei e na thai pouh haw. Na san ni ratoumnae hoi ka heinae hah na thai pouh haw.
29 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
Hete hmuen koe ka min a kamtue han na tie patetlah, hete hmuen hoi hete impui hah karum khodai pou khen nateh, na san ni hete hmuen koe ka ratoum e lawk hah na thai pouh haw.
30 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
Na san hoi na tami Isarelnaw ni hete hmuen koelah kangvawi haw. A ratoum awh toteh a hei awh e hah thai pouh haw.
31 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
Tami bang patet ni hai a imrinaw koe yon a sak awh toteh, thama lahoi lawk hah kam sak pawiteh, hete na bawkim khoungroe hmalah a tho hoi lawk a kam toteh,
32 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
Kalvan lahoi na thai pouh nateh, tami kathoungnaw e tawksaknae teh amamae lû dawk letlang phat sak haw. Tami kalan teh, a lannae patetlah yonpen laipalah na san heh lawkceng pouh.
33 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
Na tami Isarelnaw ni nang taranlahoi yonnae a sak awh kecu, a tarannaw ni tâ awh pawiteh, nang koe a kamlang awh teh, na min hah a pâpho awh teh, hete bawkim dawk ratoum awh pawiteh, hno a hei awh navah,
34 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
Kalvan hoi thai pouh nateh, na tami Isarelnaw e yonnae hah ngaithoum haw. A na mintoenaw koe na poe e ram lah bout bankhai haw.
35 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
Nang taranlahoi yonnae sak kecu dawk kalvan hah a pâbing, kho a rak hoeh toteh, het hmuen koe kangvawi a ratoum teh, na min a pâpho teh, a pataw nahan na poe e thung hoi a yonnae kamlang takhai pawiteh,
36 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
Kalvan hoi thai pouh nateh, a cei nahane lam kalan pâtu nateh, râw lah na poe e ram dawk kho a rak thai nahanlah na san Isarelnaw e yonnae ngaithoum pouh haw.
37 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
Ram dawk takang a tho teh, lacik thoseh, kehramnae thoseh, pawknae thoseh, samtong thoseh, ahriai thoseh awm boilah, a taran ni a khopui longkha koehoi koe kalup awh pawiteh, patawnae lacik aphunphun a pha toteh,
38 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili:
Tami bangpatet ni hai ratoum hoi kâheinae a sak nakunghai, na tami Isarelnaw pueng ni, amae a lungthin hoi lacik ao e hah a panue awh teh, hete bawkim koe kangvawi hoi a kut a dâw awh toteh,
39 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
Na onae hmuen kalvan hoi thai pouh haw. Ngaithoum haw. Kâroe haw. Lungthin na kapanuekkung nang ni a hringnae hoi kamcu e hah, poe haw. Bangkongtetpawiteh, nang dueng doeh tami lungthin na kapanuekkung lah na o.
40 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
A mintoenaw na poe e ram dawk hoi nang na taki nahanlah,
41 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako,
Hothloilah, na tami Isarel lah kaawm hoeh e miphun alouke na min kecu ram ahlanae koehoi kathonaw kong dawk,
42 kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili,
Na lentoenae na min hoi thaonae kut hoi na kut na dâwnae kong hah a panue awh han doeh. Hotnaw ni hai hete bawkim dawk a ratoum awh toteh,
43 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
Na onae hmuen kalvan hoi thai pouh haw. Na tami Isarelnaw patetlah talai miphun tangkuem ni na min a panue hoi nang barilawa na ta awh teh, hete ka sak e bawkim heh na min lahoi kaw e doeh ti a panue thai awh nahan, nang koe ka kâhet e miphun ni a hei awh e naw pueng hah sak pouh haw.
44 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
Na taminaw ni a tarantuk han na tha awhnae koe a cei awh toteh na rawi e khopui koe kangvawi hoi na min hanlah sak e bawkim koe kangvawi hoi BAWIPA koe a ratoum awh toteh,
45 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
A ratoumnae hoi a kâheinae hah kalvan hoi na thai pouh haw. A lawknaw hah pouk pouh haw.
46 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu;
Na tak dawk yonnae a sak awh teh, bangtelamaw yonnae ka sak hoeh e apihai awm hoeh bo. Ahnimouh koe na lungkhuek teh, a taran kut dawk na poe teh ahlanae koe thoseh, a hnainae koe thoseh, a tarannaw ni san lah man pawiteh,
47 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’;
San lah a ceikhainae ram dawk a lung a ang awh teh, pan a kângai awh teh, yonnae koe ka sak awh toe, kalan hoeh e hno hoi, puenghoi yonnae ka sak awh toe titeh, san lah a hrawinae hmuen koehoi kâhet awh pawiteh,
48 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako;
A taran lah kahrawikungnaw e ram hoi a lungthin katang hoi a hringnae katang hoi nang koelah kangvawi hoi a na mintoenaw koevah, na poe e hoi na rawi e khopui hoi nang han ka sak e bawkim koe lah kangvawi laihoi nang koe a ratoum awh toteh,
49 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao.
A ratoumnae hoi a kâheinae hah kalvan na onae koehoi thai pouh nateh a lawknaw hah pouk pouh haw.
50 Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma;
San lah kamankungnaw ni a pahren awh thai nahan, na hmalah pahren sak awh haw. Nang koe yonnae kasaknaw hoi na hmalah, kâtapoenae kong dawk na taminaw e kâtapoenae naw pueng hah ngaithoum haw.
51 kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.
Bangkongtetpawiteh, ahnimouh teh, na taminaw teh Izip ram hoi sumthawngnae tahmanghmai thung hoi na tâco sak e naw doeh.
52 “Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia.
Na kaw awh toteh, na thai pouh nahanelah, na san ni a kâheinae hai na tami Isarel ni a kâheinae koe lah, na mit na ta thai nahan,
53 Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”
Bangtelane Oe Bawipa Jehovah, ka na mintoenaw Izip ram hoi na tâcokhai navah, na san Mosi hno lahoi na dei tangcoung e patetlah miphunnaw pueng thung hoi na râw lah na kapek telah a ti.
54 Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni.
Solomon ni BAWIPA koevah ratoumnae hoi a kâheinae naw pueng koung a dei hnukkhu, BAWIPA e thuengnae khoungroe koelah a khokpakhu a cuengkhuem teh, kalvan lah kut a dâwnae koehoi a thaw.
55 Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:
A kangdue teh lawk kacaipoung lahoi,
56 “Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose.
a lawkkam patetlah a tami Isarelnaw hanlah, kâhatnae kapoekung BAWIPA teh pholen lah awm naseh. A san Mosi hno lahoi kahawi e lawkkamnaw pueng hah, lawklung buet touh hai phen hoeh.
57 Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa.
Maimae BAWIPA ka Cathut teh, mintoenaw koevah ao e patetlah maimouh koehai awm naseh. Maimanaw hah khoeroe na pahnawt hanh naseh.
58 Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu.
A lamnaw pueng tarawi hane hoi mintoenaw koe kâ a poe tangcoung e patetlah kâpoelawknaw, phunglamnaw hoi, lawkcengnaenaw dâw pouh hanlah, maimae lungthin ama koe lah a kangvawi thai nahan,
59 Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku,
Cathut Jehovah lah a onae, alouke awm hoeh tie miphun pueng ni a panue thai awh nahan, a san kong dawk thoseh,
60 ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine.
A tami Isarelnaw kong dawk thoseh, a panki e patetlah hnin touh hoi hnin touh a kâroe thai nahan, hete ka dei e naw pueng hah, BAWIPA hmalah ka kâhei e pueng hah karum khodai pouk laipalah, BAWIPA Cathut hmalah pou kangning lawiseh.
61 Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”
Hatdawkvah, sahnin e na o e boiboelah, a phunglawknaw dawk na hring awh teh, kâpoelawknaw tarawi hane hoi, maimae BAWIPA Cathut koe na lungthin hah yuemkamcu lah awm seh telah Isarelnaw pueng hah yawhawinae a poe.
62 Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana.
Siangpahrang hoi Isarelnaw pueng ni BAWIPA e hmalah sathei thuengnae hah a poe awh.
63 Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.
Solomon ni BAWIPA hanelah a poe e roum thuengnae maitotan 22, 000 hoi, tu 120, 000 touh a poe awh. Hottelah siangpahrang hoi Isarelnaw pueng ni BAWIPA e im dawk a poe awh.
64 Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.
Hat hnin vah, siangpahrang ni BAWIPA im e a thongma hah a thoung sak. Hawvah, hmaisawi thuengnae hoi tavai thuengnae e hoi, roum thuengnae satui hah a poe awh. Bangkongtetpawiteh, BAWIPA e hmalah rahum khoungroe hah kapoenaw hanelah a thoungca.
65 Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne.
Hatnavah, Solomon hoi Isarelnaw pueng kamkhueng e ni Hamath kho kâennae koehoi, Izip ram palang totouh, kaawm e naw hah, maimae BAWIPA hmalah hnin 7 touh hoi hnin 7 kâhlat lah hnin 14 touh thung pawi a sak awh.
66 Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.
Hnin 8 hnin vah tamimaya teh a ban sak awh. Siangpahrang teh ahnimouh ni yawhawi a poe awh teh, BAWIPA ni a san Devit hoi a tami Isarelnaw hanelah, a sak e ahawinae naw kecu dawk lungthin nawmnae hoi, lunghawinae hoi, amamae rim dawk a cei awh.