< 1 Wafalme 7 >

1 Ilimchukua Solomoni miaka kumi na mitatu kukamilisha ujenzi wa Jumba lake la kifalme.
И дом свой созда Соломон треминадесять леты, и соверши Соломон весь дом свой.
2 Alijenga Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni, urefu wake ulikuwa dhiraa 100, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini, likiwa na safu nne za nguzo za mierezi zikishikilia boriti za mierezi zilizorembwa.
И созда дом древом Ливанским, сто лакот долгота его, и тридесять лакот высота его, и пятьдесят лакот широта его, и три ряды столпов кедровых, и рамена кедрова столпом.
3 Ilipauliwa kwa mierezi juu ya boriti zile zilizolala juu ya nguzo arobaini na tano, kumi na tano kwa kila safu.
И покры дсками кедровыми дом свыше над странами столпов: и число столпов четыредесять и пять,
4 Madirisha yake yaliwekwa juu kwa safu tatu, yakielekeana.
по пятинадесяти ряд: и окон три ряда, и камара над камарою трегубо.
5 Milango yote ilikuwa na miimo ya mstatili, ilikuwa upande wa mbele katika safu tatu, ikielekeana.
И вся двери и камары четвероуголны притворени: от дверий над дверми трегубо.
6 Akajenga ukumbi wa nguzo, ambao urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa thelathini. Mbele ya jengo hilo kulikuwepo baraza. Mbele ya baraza kulikuwepo na nguzo na paa lililoningʼinia.
И елам столпов, пятьдесят лакот в долготу, и тридесять лакот в широту привязани ко Еламу пред лицем их: и столпи и толстота пред лицем того елама.
7 Akajenga ukumbi wa kiti cha enzi, Ukumbi wa Hukumu, mahali ambapo angelitolea hukumu, akaufunika kwa mierezi kutoka sakafuni hadi darini.
И елам престолов идеже судити, елам судилища, и покры и от земли даже до верха дщицами кедровыми.
8 Kwenye jumba la kifalme ambamo angeliishi, aliiweka nyuma zaidi, ikiwa na mjengo wa aina moja na hiyo nyingine. Pia Solomoni akajenga jumba la kifalme linalofanana na huo ukumbi mkubwa kwa ajili ya binti Farao, aliyekuwa amemwoa.
И дом в немже живяше, двор един распростерт сим по делу сему: и дом созда дщери фараони, юже взя Соломон, по еламу сему.
9 Ujenzi huu wote, kuanzia nje mpaka kwenye ua mkuu na kuanzia kwenye msingi hadi upenuni, ulifanywa kwa mawe ya ubora wa hali ya juu yaliyokuwa yamechongwa kwa vipimo na kusawazishwa kwa msumeno nyuso zake za ndani na za nje.
Вся сия бяху от каменей драгоценных изваяна от разстояния внутрьуду, и от основания до крова.
10 Misingi iliwekwa kwa mawe makubwa yaliyo bora, yenye urefu wa dhiraa kumi na mengine yenye urefu wa dhiraa nane
И внеуду ко двору великому основаному камением драгим великим, камением десяти лакот и осми лакот,
11 Sehemu za juu kulikuwepo na mawe yenye ubora wa hali ya juu, yaliyokatwa kwa vipimo na boriti za mierezi.
и с верху честным камением, по тойже мере несеченых, и кедрами.
12 Ule ua mkuu ulizungukwa na ukuta wa safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa, kama ulivyokuwa ua wa ndani wa Hekalu la Bwana na baraza yake.
Окрест двора великаго три ряда нетесаных, и ряд тесанаго кедра: и созда двор храма внутреннейший притвора дому Сущаго пред лицем храма.
13 Mfalme Solomoni akatuma watu Tiro kumleta Hiramu,
И посла царь Соломон в Тир, и взя Хирама от Тира,
14 ambaye mama yake alikuwa mjane kutoka kabila la Naftali na baba yake alikuwa mtu wa Tiro tena fundi wa shaba. Hiramu alikuwa na ustadi wa hali ya juu na mzoefu katika aina zote za kazi ya shaba. Alikuja kwa Mfalme Solomoni na kufanya kazi zake zote alizopangiwa.
сына жены вдовицы, и той бе от колена Неффалимля: и отец его бе муж Тирин, делатель меди, и исполнен художества и разума и ведения, еже делати всяко дело медяное. И приведоша его ко царю Соломону: и сотвори вся дела:
15 Hiramu akasubu nguzo mbili za shaba, kila moja ikiwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kila nguzo ikiwa na mzingo wa dhiraa kumi na mbili kwa mstari.
и слия два столпа еламу храма, осминадесяти лакот высота столпа, и окрест мера его четыренадесятих лакот окружаше его толстота столпа: четырех перстов вглубления: такожде бе и вторый столп:
16 Pia alitengeneza mataji mawili ya shaba ya kusubu ili kuyaweka juu ya hizo nguzo; kila taji lilikuwa na kimo cha dhiraa tano kwenda juu.
и два возложения сотвори, лежати на главах столпов излиянная от меди: пяти лакот высота возложения единаго, и пяти лакот высота возложения втораго:
17 Wavu wa mikufu iliyosokotewa kwenye zile taji juu ya zile nguzo, saba kwa kila taji.
и сотвори две мрежи еже покрыти возложения столпов: и мрежу возложению единому, и мрежу возложению второму:
18 Akatengeneza makomamanga katika safu mbili kuzunguka kila wavu kuremba mataji yaliyo juu ya nguzo. Alifanya hivyo kwa kila nguzo.
и дело висимо, два ряда яблок медяных сомрежены, дело висимо, ряд над рядом: такожде сотвори возложению второму:
19 Mataji yaliyokuwa juu ya nguzo kwenye baraza, yalikuwa katika umbo la yungiyungi, kimo chake ni dhiraa nne
и возложения на главах столпов, подобна крину, якоже во еламе, четырех лакот:
20 Juu ya mataji ya zile nguzo mbili, juu ya ile sehemu yenye umbo kama bakuli, karibu na ule wavu, kulikuwa na yale makomamanga 200 katika safu kuzunguka pande zote.
и строение над обоими столпами, и свыше стран возложение строения, и яблоков двести рядов около на вторей главе.
21 Hiramu akasimamisha nguzo kwenye baraza ya Hekalu. Nguzo ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ile ya upande wa kaskazini Boazi.
И постави столпы во еламе храма: и постави столп един и нарече имя ему Иахун, и постави столп вторый и нарече имя ему Воос.
22 Mataji yaliyokuwa juu yalikuwa na umbo la yungiyungi. Hivyo kazi ya nguzo ikakamilika.
И на главах столпов дело криново, и сконча дело столпов.
23 Hiramu akasubu Bahari ya chuma, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Mzunguko wake ulikuwa dhiraa thelathini.
И сотвори море лияно десять лакот от края до края его, кругло окрест его: пять лакот высота его, и объятие его тридесять лактей окружаше е окрест:
24 Chini ya ukingo, ilizungukwa na maboga, kumi kwenye kila dhiraa moja. Maboga yalikuwa yamesubiwa katika safu mbili ili kuwa kitu kimoja na hiyo bahari.
и подкрепления под краем его окрест, окружаху е десять лакот около: два ряда подкреплений слиты во слиянии его стояща.
25 Bahari iliwekwa juu ya mafahali kumi na wawili, watatu wakielekea kaskazini, watatu wakielekea magharibi, watatu wakielekea kusini na watatu wakielekea mashariki. Bahari iliwekwa juu yao na sehemu zao za nyuma zilielekeana.
И дванадесять волов под морем, три зрящии на север, и три зрящии на юг, и три на запад, и три на восток, и вся задняя их внутрьуду, и море верху их.
26 Ilikuwa na unene wa nyanda nne na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 2,000.
И устие его бяше яко устие потиря прозябающаго крина, и толстота его на длань.
27 Pia akatengeneza vitako kumi vya shaba vinavyoweza kuhamishika, kila kimoja kilikuwa na urefu wa dhiraa nne, upana dhiraa nne na kimo chake dhiraa tatu
И сотвори десять мехонофов медяных, пять лакот долгота мехонофа единаго, и четыри лакти широта его, и шесть лакот высота его:
28 Hivi ndivyo vile vitako vilivyotengenezwa: Vilikuwa na mbao za pembeni zilizoshikamanishwa na mihimili.
и сие дело мехонофов, споеное о себе и споеное посреде произницающих:
29 Juu ya mbao kati ya hiyo mihimili kulikuwa na simba, mafahali na makerubi, pia kwenye mihimili yake. Juu na chini ya simba na mafahali kulikuwa kumesokotewa taji za kufuliwa.
и на споениих их посреде произницающих львы и волы и херувимы, и над произницающими, такожде и свыше и снизу львов и волов места, дело низхождения:
30 Kila kitako kilikuwa na magurudumu manne ya shaba, na vyuma vya katikati vya kuyazungusha hayo magurudumu na kila kimoja kilikuwa na sinia kwenye vishikizo vinne vya taji iliyosubiwa kila upande.
и четыри колеса медна и мехонофу коемуждо, и придержания медяна, и четыри части их, и рамена их под умывалницами, и рамена слияная об ону страну коегождо прилежаще.
31 Ndani ya kitako kulikuwa na nafasi ya wazi iliyokuwa na umbile la mviringo lenye kina cha dhiraa moja. Nafasi hii ya wazi ilikuwa ya mviringo, pamoja na kitako chake ilikuwa dhiraa moja na nusu. Kuzunguka huo mdomo wake kulitiwa nakshi. Papi za vitako zilikuwa mraba na si za mviringo.
И уста его внутрь главы, и выше единаго лактя, и уста его кругла: дело такожде лактя единаго и пол лактя: и на устах его изваяния, и междустолпия их четвероуголна, а не кругла.
32 Magurudumu manne yalikuwa chini ya papi, na vyuma vya katikati vya kuzungushia magurudumu hayo vilikuwa vimeunganishwa kwenye kitako. Kipenyo cha kila gurudumu kilikuwa dhiraa moja na nusu.
И четыри колеса под междустолпиями, и руце в колесех в мехонофе: и высота единаго колеса лакоть и пол.
33 Magurudumu yalitengenezwa kama ya magari ya vita ya kukokotwa, vyuma vya katikati vya magurudumu, duara zake, matindi yake na vikombe vyake vyote vilikuwa vya kusubu.
И дело колес, яко дело колес колесницы: руце их и выи их, и хребты их и делания их вся лияна.
34 Kila kitako kilikuwa na mikono minne, moja kwenye kila pembe, ukitokeza kutoka kwenye kitako.
Четыри рамена на четырех углех мехонофа единаго, и от мехонофа рамена его.
35 Juu ya kitako kulikuwepo na utepe wa mviringo wenye kina cha nusu dhiraa. Vishikio na papi vilishikamana upande wa juu wa kitako.
И на главе мехонофа пол лактя величество его, кругло окрест над главою мехонофовою: и начало рук его и спаяния его от него: и отверзашеся в началех рук своих.
36 Alitia nakshi za makerubi, simba na miti ya mitende juu ya uso wa vishikio na juu ya papi, katika kila nafasi iliyopatikana, pamoja na mataji yaliyosokotwa kuzunguka pande zote.
И спаяния его подобия херувимов и львов и фиников стоящая, держащееся коеждо противу лица его внутрь и окрест.
37 Hivi ndivyo Hiramu alivyotengeneza vile vitako kumi. Vyote vilikuwa vya kusubu kwenye kalibu za kufanana kwa vipimo na kwa umbo.
По томужде сотвори вся десять мехонофы, по чину единому и по мере единей, мера едина всем.
38 Kisha akatengeneza masinia kumi ya shaba, kila moja likiwa na ujazo wa bathi arobaini, yakiwa na kipenyo cha dhiraa nne kila sinia moja kwa kila kimoja ya vile vitako kumi.
И сотвори десять конобов медяных вмещающих по четыредесяти мер во един коноб, мерою четырех лактей: коноб един на коемждо мехонофе, от десяти мехонофов.
39 Aliweka vitako vitano upande wa kusini wa Hekalu na vingine vitano upande wa kaskazini. Akaweka ile bahari upande wa kusini, katika pembe ya kusini ya Hekalu.
И постави пять мехонофов по десней стране храма на восток, и пять по левей стране храма: и море от страны храма одесную на востоки в угле полуденнем.
40 Pia akatengeneza masinia, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi zote katika Hekalu la Bwana kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
И сотвори Хирам конобы и теплицы и фиалы: и сконча Хирам вся дела творя, яже творяше цареви Соломону во храме Господни:
41 nguzo mbili; mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo; nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo;
столпа два, и обвития столпов над главами столпов два: и мрежи две, еже покрывати оба обвития изваяных, яже на столпех суть:
42 makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
яблоков медяных четыреста обема мрежема, два ряда яблоков мрежи единей, покрывати оба обвития мехонофа, яже на обоих столпех:
43 vitako kumi pamoja na masinia yake kumi;
и мехонофов десять и конобов десять на мехонофе:
44 ile Bahari ya chuma na yale mafahali kumi na wawili chini yake;
и море едино, и волов дванадесять под морем:
45 masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Vyombo hivi vyote ambavyo Huramu alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyongʼarishwa.
и конобы и теплицы и фиалы, и вся сосуды, яже сотвори Хирам царю Соломону во храме Господни: и столпов четыредесять и осмь дому царева и дому Господня: вся дела царева, яже сотвори Хирам, быша медяна вся.
46 Mfalme akaamuru wavisubu katika kalibu ya udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani ulio kati ya Sukothi na Sarethani.
Близ Иордана слия их царь в толстоте земли, между Сокхофом и между Сирамом.
47 Solomoni akaviacha vitu hivi vyote bila kupima uzani wake, kwa sababu vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
Не бе веса меди, от неяже творяше вся дела сия, от множества зело, не бе предела весу меди.
48 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana: madhabahu ya dhahabu; meza ya dhahabu za kuweka mikate ya Wonyesho;
И даде царь Соломон вся сосуды, яже сотвори во храм Господень: олтарь златый и трапезу, на нейже хлебы приношения, златую,
49 vinara vya taa vya dhahabu safi (vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto, mbele ya Patakatifu pa Patakatifu); kazi ya maua ya dhahabu na taa na makoleo;
и свещники пять одесную и пять ошуюю пред лицем давира (Святая святых) златыя спаяны, и лампады, и светилники, и щипцы златыя,
50 masinia ya dhahabu safi, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, vyano na vyetezo; na bawaba za dhahabu kwa ajili ya milango ya chumba cha ndani sana, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na pia kwa ajili ya milango ya ukumbi mkuu wa Hekalu.
и преддверие, и гвоздие, и фиалы и блюда и кадилницы златы спаяны: и вереи врат дому внутренняго Святаго Святых, и двери храма златыя.
51 Hivyo Mfalme Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Bwana.
И совершися дело, еже сотвори Соломон во храме Господни: и внесе Соломон святая Давида отца своего и вся святая Соломонова, сребро и злато, и сосуды даде в сокровище храма Господня.

< 1 Wafalme 7 >