< 1 Wafalme 6 >
1 Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
En el año cuatrocientos ochenta después de que los hijos de Israel salieron de la tierra de Egipto, en el cuarto año del reinado de Salomón sobre Israel, en el mes de Ziv, que es el segundo mes, comenzó a edificar la casa de Yahvé.
2 Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
La casa que el rey Salomón construyó para Yahvé tenía una longitud de sesenta codos, y su anchura veinte, y su altura treinta codos.
3 Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
El pórtico frente al templo de la casa tenía una longitud de veinte codos, que se extendía a lo ancho de la casa. Su anchura era de diez codos frente a la casa.
4 Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
Hizo ventanas de celosía fija para la casa.
5 Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
Contra la pared de la casa, construyó pisos alrededor, contra las paredes de la casa alrededor, tanto del templo como del santuario interior; e hizo habitaciones laterales alrededor.
6 Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
El piso más bajo tenía cinco codos de ancho, el del medio seis codos de ancho y el tercero siete codos de ancho, pues por fuera hizo desviaciones en la pared de la casa en todo su perímetro, para que las vigas no se introdujeran en las paredes de la casa.
7 Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
La casa, cuando se estaba construyendo, era de piedra preparada en la cantera; y no se oyó en la casa ningún martillo ni hacha ni ninguna herramienta de hierro mientras se estaba construyendo.
8 Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
La puerta de las habitaciones del medio estaba en el lado derecho de la casa. Se subía por una escalera de caracol al piso del medio, y del medio se subía al tercero.
9 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
Así que construyó la casa y la terminó; y la cubrió con vigas y tablas de cedro.
10 Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
Construyó los pisos a lo largo de la casa, cada uno de cinco codos de altura, y los apoyó en la casa con maderas de cedro.
11 Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
La palabra de Yahvé vino a Salomón, diciendo:
12 “Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
“En cuanto a esta casa que estás construyendo, si andas en mis estatutos, y ejecutas mis ordenanzas, y guardas todos mis mandamientos para andar en ellos, entonces confirmaré contigo mi palabra, que hablé a David tu padre.
13 Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
Habitaré en medio de los hijos de Israel y no abandonaré a mi pueblo Israel”.
14 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
Salomón construyó la casa y la terminó.
15 Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
Construyó las paredes de la casa por dentro con tablas de cedro; desde el piso de la casa hasta las paredes del techo, las cubrió por dentro con madera. Cubrió el piso de la casa con tablas de ciprés.
16 Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
Construyó veinte codos de la parte trasera de la casa con tablas de cedro desde el suelo hasta el techo. Construyó esto por dentro, para un santuario interior, para el lugar santísimo.
17 Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
La parte delantera del santuario tenía cuarenta codos de largo.
18 Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
En el interior de la casa había cedro tallado con capullos y flores abiertas. Todo era de cedro. No se veía ninguna piedra.
19 Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
Preparó un santuario interior en medio de la casa de adentro, para colocar allí el arca de la alianza de Yahvé.
20 Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
El santuario interior tenía veinte metros de largo, veinte metros de ancho y veinte metros de alto. La recubrió de oro puro. Cubrió el altar con cedro.
21 Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
Salomón recubrió de oro puro la casa por dentro. Trazó cadenas de oro delante del santuario interior y lo recubrió de oro.
22 Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
Recubrió de oro toda la casa, hasta que estuvo terminada. También recubrió de oro todo el altar que pertenecía al santuario interior.
23 Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
En el santuario interior hizo dos querubines de madera de olivo, de diez codos de altura cada uno.
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
La longitud de un ala del querubín era de cinco codos, y la del otro, de cinco codos. Desde la punta de un ala hasta la punta de la otra había diez codos.
25 Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
El otro querubín medía diez codos. Ambos querubines tenían una misma medida y una misma forma.
26 Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
Un querubín tenía diez codos de altura, y el otro querubín también.
27 Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
Puso los querubines dentro de la casa interior. Las alas de los querubines estaban extendidas, de tal manera que el ala de uno tocaba una pared y el ala del otro querubín tocaba la otra pared; y sus alas se tocaban entre sí en medio de la casa.
28 Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
Recubrió los querubines con oro.
29 Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
Talló todas las paredes de la casa alrededor con figuras talladas de querubines, palmeras y flores abiertas, por dentro y por fuera.
30 Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
Recubrió de oro el suelo de la casa, por dentro y por fuera.
31 Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
Para la entrada del santuario interior, hizo puertas de madera de olivo. El dintel y los postes de la puerta eran la quinta parte de la pared.
32 Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
Hizo, pues, dos puertas de madera de olivo, y talló en ellas tallas de querubines, palmeras y flores abiertas, y las recubrió de oro. Extendió el oro sobre los querubines y las palmeras.
33 Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
También hizo los postes de la entrada del templo de madera de olivo, de una cuarta parte de la pared,
34 Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
y dos puertas de madera de ciprés. Las dos hojas de una puerta eran plegables, y las dos hojas de la otra puerta eran plegables.
35 Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
Esculpió querubines, palmeras y flores abiertas, y los recubrió con oro ajustado a la obra grabada.
36 Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
Construyó el atrio interior con tres hileras de piedra tallada y una hilera de vigas de cedro.
37 Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
Los cimientos de la Casa de Yahvé fueron puestos en el cuarto año, en el mes de Ziv.
38 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.
En el undécimo año, en el mes de Bul, que es el octavo mes, la casa fue terminada en todas sus partes y según todas sus especificaciones. Así pasó siete años construyéndola.