< 1 Wafalme 6 >
1 Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
Or Salomon bâtit la maison de l'Éternel, la quatre cent quatre-vingtième année après que les enfants d'Israël furent sortis du pays d'Égypte, la quatrième année de son règne sur Israël, au mois de Ziv, qui est le second mois.
2 Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
Et la maison que le roi Salomon bâtit à l'Éternel avait soixante coudées de long, vingt de large, et trente coudées de haut.
3 Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
Le portique devant le temple de la maison avait vingt coudées de long, selon la largeur de la maison, et dix coudées de large devant la maison.
4 Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
Il fit aussi à la maison des fenêtres à jalousies fixes.
5 Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
Et il bâtit, contre la muraille de la maison, à l'entour, un corps d'étages, entourant les murs de la maison, le temple et le sanctuaire; ainsi il fit des chambres latérales tout autour.
6 Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
La largeur de l'étage d'en bas était de cinq coudées; la largeur de celui du milieu de six coudées, et la largeur du troisième de sept coudées; car il avait fait en retraite le mur de la maison par dehors, tout autour, afin que la charpente n'entrât pas dans les murailles de la maison.
7 Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
Or, en bâtissant la maison, on la bâtit de pierres toutes préparées dans la carrière; de sorte que ni marteau, ni hache, ni aucun outil de fer ne furent entendus dans la maison quand on la bâtissait.
8 Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
L'entrée des chambres du milieu était au côté droit de la maison; et on montait par un escalier tournant à l'étage du milieu, et de celui du milieu au troisième.
9 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
Il bâtit donc la maison et l'acheva. Et il couvrit la maison de planches et de poutres de cèdre.
10 Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
Et il bâtit les étages contre toute la maison, chacun de cinq coudées de haut; et ils tenaient à la maison par des bois de cèdre.
11 Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
Alors la parole de l'Éternel fut adressée à Salomon, en ces termes:
12 “Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
Quant à cette maison que tu bâtis, si tu marches dans mes statuts, et si tu pratiques mes ordonnances, et si tu gardes tous mes commandements, pour y marcher, j'accomplirai à ton égard la parole que j'ai dite à David ton père;
13 Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
Et j'habiterai au milieu des enfants d'Israël, et n'abandonnerai point mon peuple d'Israël.
14 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
Ainsi Salomon bâtit la maison et l'acheva.
15 Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
Il lambrissa les murailles de la maison, par dedans, de planches de cèdre, depuis le sol de la maison jusqu'aux parois de la toiture; il couvrit de bois tout le dedans; et il revêtit le sol de la maison de planches de cyprès.
16 Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
Il lambrissa aussi de planches de cèdre vingt coudées à partir du fond de la maison, tant le sol que les murailles; il lambrissa ainsi intérieurement cet espace pour le sanctuaire, le lieu très-saint.
17 Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
Mais les quarante coudées sur le devant formaient la maison, savoir le temple.
18 Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
Et le cèdre, au-dedans de la maison, était sculpté en coloquintes et en fleurs épanouies; tout était de cèdre; la pierre ne se voyait pas.
19 Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
Quant au sanctuaire, il l'établit à l'intérieur de la maison vers le fond, pour y mettre l'arche de l'alliance de l'Éternel.
20 Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
Et le sanctuaire avait par-devant vingt coudées de long, vingt coudées de large et vingt coudées de haut; il le couvrit d'or fin; il en couvrit aussi l'autel, qui était en cèdre.
21 Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
Et Salomon couvrit d'or fin l'intérieur de la maison; et il fit passer le voile avec des chaînes d'or au-devant du sanctuaire, qu'il couvrit d'or.
22 Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
Ainsi il couvrit d'or la maison tout entière; il couvrit aussi d'or tout l'autel du sanctuaire.
23 Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
Et il fit dans le sanctuaire deux chérubins de bois d'olivier, de dix coudées de haut.
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
L'une des ailes d'un des chérubins avait cinq coudées, et l'autre aile du chérubin avait cinq coudées; depuis le bout d'une aile jusqu'au bout de l'autre aile, il y avait dix coudées.
25 Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
Le second chérubin était aussi de dix coudées. Les deux chérubins étaient d'une même mesure et taillés l'un comme l'autre.
26 Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
La hauteur d'un chérubin était de dix coudées, et l'autre chérubin était de même.
27 Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
Et il mit les chérubins au-dedans de la maison, vers le fond; et on étendit les ailes des chérubins, de sorte que l'aile de l'un touchait une muraille et l'aile de l'autre chérubin touchait l'autre muraille; et que leurs ailes se rencontraient au milieu de la maison, l'une des ailes touchant l'autre.
28 Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
Et il couvrit d'or les chérubins.
29 Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
Et sur toutes les murailles de la maison, tout autour, il fit sculpter en relief des chérubins, et des palmes, et des fleurs épanouies, tant au-dedans qu'au-dehors.
30 Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
Et il revêtit d'or le sol de la maison, tant au-dedans qu'au-dehors.
31 Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
Et il fit la porte du sanctuaire à deux battants, de bois d'olivier; l'encadrement avec les poteaux, occupait un cinquième de la paroi.
32 Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
Les deux battants étaient de bois d'olivier; et il y fit sculpter des chérubins, des palmes et des fleurs épanouies, et il les couvrit d'or, étendant l'or sur les chérubins et sur les palmes.
33 Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
Il fit aussi pour la porte du temple des poteaux de bois d'olivier, d'un quart de la paroi;
34 Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
Et deux battants de bois de cyprès; les deux pièces d'un des battants étaient brisées; et les deux pièces de l'autre battant étaient aussi brisées.
35 Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
Et il y sculpta des chérubins, des palmes et des fleurs épanouies, et il les couvrit d'or, exactement appliqué sur les sculptures.
36 Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
Il bâtit aussi le parvis intérieur de trois rangées de pierre de taille et d'une rangée de poutres de cèdre.
37 Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
La quatrième année, au mois de Ziv, les fondements de la maison de l'Éternel furent posés;
38 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.
Et la onzième année, au mois de Bul, qui est le huitième mois, la maison fut achevée, avec toutes ses appartenances et tous ses meubles. On mit sept ans à la bâtir.