< 1 Wafalme 6 >
1 Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
Or il arriva qu'en l'année quatre cent quatre-vingt, après que les enfants d'Israël furent sortis du pays d'Egypte, la quatrième année du règne de Salomon sur Israël, au mois de Zif, qui est le second mois, il bâtit une maison à l'Eternel.
2 Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
Et la maison que le Roi Salomon bâtit à l'Eternel avait soixante coudées de long, et vingt de large, et trente coudées de haut.
3 Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
Le porche qui était devant le Temple de la maison, avait vingt coudées de long, qui répondait à la largeur de la maison, et il avait dix coudées de large sur le devant de la maison.
4 Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
Il fit aussi des fenêtres à la maison, larges par dedans, [et] rétrécies par dehors.
5 Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
Et joignant la muraille de la maison il bâtit des appentis de chambres l'une sur l'autre tout alentour, [appuyés] sur les murailles de la maison, tout autour du Temple, et de l'Oracle, ainsi il fit des chambres tout à l'entour.
6 Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
La largeur de l'appentis d'en bas était de cinq coudées, et la largeur de celui du milieu était de six coudées, et la largeur du troisième était de sept coudées; car il avait fait des rétrécissements en la maison par dehors, afin que [la charpenterie des appentis] n'entrât pas dans les murailles de la maison.
7 Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
Or en bâtissant la maison on la bâtit de pierres amenées toutes telles qu'elles devaient être, de sorte qu'en bâtissant la maison on n'entendit ni marteau, ni hache, ni aucun outil de fer.
8 Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
L'entrée des chambres du milieu [était] au côté droit de la maison, et on montait par une vis aux [chambres] du milieu; et de celles du milieu à celles du troisième [étage].
9 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
Il bâtit donc la maison, et l'acheva, et il couvrit la maison de lambris en voûte, et de poutres de cèdre.
10 Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
Et il bâtit les appentis joignant toute la maison, chacun de cinq coudées de haut, et ils tenaient à la maison par le moyen des bois de cèdre.
11 Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
Alors la parole de l'Eternel fut adressée à Salomon, en disant:
12 “Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
Quant à cette maison que tu bâtis, si tu marches dans mes statuts, et si tu fais mes ordonnances, et que tu gardes tous mes commandements, en y marchant, je ratifierai en ta faveur la parole que j'ai dite à David ton père.
13 Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
Et j'habiterai au milieu des enfants d'Israël, et je n'abandonnerai point mon peuple d'Israël.
14 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
Ainsi Salomon bâtit la maison, et l'acheva.
15 Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
Il lambrissa d'ais de cèdre, les murailles de la maison par dedans, depuis le sol de la maison jusqu'à la voûte lambrissée; il [les] couvrit de bois par dedans, et il couvrit le sol de la maison d'ais de sapin.
16 Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
Il lambrissa aussi l'espace de vingt coudées d'ais de cèdre au fond de la maison, depuis le sol jusqu'au haut des murailles, et il lambrissa [cet espace] au dedans pour être l'Oracle, [c'est-à-dire], le lieu Très-saint.
17 Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
Mais la maison, [savoir] le Temple de devant, était de quarante coudées.
18 Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
Et les ais de cèdre qui étaient pour le dedans de la maison, étaient entaillés de boutons de fleurs épanouies, relevées en bosse; tout le dedans était de cèdre, on n'y voyait pas une pierre.
19 Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
Il disposa aussi l'Oracle au dedans de la maison vers le fond, pour y mettre l'Arche de l'alliance de l'Eternel.
20 Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
Et l'Oracle avait par devant vingt coudées de long, et vingt coudées de large, et vingt coudées de haut, et on le couvrit de fin or; on en couvrit aussi l'autel, [fait d'ais] de cèdre.
21 Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
Salomon donc couvrit de fin or la maison, depuis l'entredeux jusqu'au fond; et fit passer un voile avec des chaînes d'or au devant de l'Oracle, lequel il couvrit d'or.
22 Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
Ainsi il couvrit d'or toute la maison entièrement. Il couvrit aussi d'or tout l'autel qui était devant l'Oracle.
23 Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
Et il fit dans l'Oracle deux Chérubins de bois d'olivier, qui avaient chacun dix coudées de haut.
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
L'une des ailes de l'un des Chérubins avait cinq coudées, et l'autre aile du [même] Chérubin avait aussi cinq coudées; depuis le bout d'une aile jusqu'au bout de l'autre aile il y avait dix coudées.
25 Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
L'autre Chérubin était aussi de dix coudées; [car] les deux Chérubins étaient d'une même mesure, et taillés l'un comme l'autre.
26 Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
La hauteur d'un Chérubin était de dix coudées, de même que celle de l'autre Chérubin.
27 Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
Et il mit les Chérubins au dedans de la maison vers le fond, et on étendit les ailes des Chérubins, en sorte que l'aile de l'un touchait à une muraille, et l'aile de l'autre Chérubin touchait à l'autre muraille; et leurs [autres] ailes se venaient [joindre] au milieu de la maison, [et] l'une des ailes touchait l'autre.
28 Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
Et il couvrit d'or les Chérubins.
29 Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
Et il entailla toutes les murailles de la maison tout autour de sculptures bien profondes de Chérubins, et de palmes, et de boutons de fleurs épanouies, tant en [la partie] du dedans, qu'en [celle] du dehors.
30 Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
Il couvrit aussi d'or le sol de la maison, tant en [la partie] qui tirait vers le fond, qu'en celle du dehors.
31 Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
Et à l'entrée de l'Oracle il fit une porte à deux battants de bois d'olivier, dont les linteaux [et] les poteaux étaient de cinq membreures.
32 Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
[Il fit] donc une porte à deux battants de bois d'olivier, et entailla sur elle des moulures de Chérubins, de palmes, et de boutons de fleurs épanouies, et les couvrit d'or, étendant l'or sur les Chérubins et sur les palmes.
33 Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
Il fit aussi à l'entrée du Temple des poteaux de bois d'olivier, de quatre membreures;
34 Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
Et une porte à deux battants de bois de sapin; les deux pièces d'un des battants étaient brisées; et les deux pièces de l'autre battant étaient aussi brisées.
35 Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
Et il y entailla des Chérubins, des palmes, et des boutons de fleurs épanouies, et les couvrit d'or, proprement posé sur les entailleures.
36 Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
Il bâtit aussi le parvis de dedans de trois rangées de pierres de taille, et d'une rangée de poutres de cèdre.
37 Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
La quatrième année, au mois de Zif, les fondements de la maison de l'Eternel furent posés.
38 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.
Et la onzième année, au mois de Bul, qui est le huitième mois, la maison fut achevée avec toutes ses appartenances et ses ordonnances; ainsi il mit sept ans à la bâtir.