< 1 Wafalme 6 >
1 Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
En la quatre cent quatre-vingtième année après la sortie des enfants d’Israël du pays d’Égypte, la quatrième année du règne de Salomon sur Israël, au mois de ziv, qui est le second mois, il bâtit la maison de Yahweh.
2 Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
La maison que le roi Salomon bâtit à Yahweh avait soixante coudées de longueur, vingt de largeur et trente coudées de hauteur.
3 Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
Le portique devant le temple de la maison avait vingt coudées de longueur dans le sens de la largeur de la maison, et dix coudées de largeur sur le devant de la maison.
4 Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
Le roi fit à la maison des fenêtres à grilles fixes.
5 Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
Il bâtit, contre la muraille de la maison, des étages autour des murs de la maison, autour du Lieu saint et du Lieu très saint, et il fit des chambres latérales tout autour.
6 Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
L’étage inférieur avait cinq coudées de largeur, celui du milieu six coudées de largeur, et me troisième sept coudées de largeur; car on avait fait en retrait les murs de la maison tout autour, en dehors, afin que les poutres n’entrassent pas dans les murs de la maison.
7 Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
Lorsqu’on bâtit la maison, on la bâtit de pierres toutes préparées dans la carrière; et ainsi ni marteau, ni hache, ni aucun instrument de fer ne furent entendus dans la maison, pendant qu’on la construisait.
8 Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
L’entrée de l’étage du milieu était du côté droit de la maison; on montait par des escaliers tournants à l’étage du milieu et de celui du milieu au troisième.
9 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
Salomon bâtit la maison et l’acheva; il couvrit la maison de poutres et de planches de cèdre.
10 Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
Il bâtit les étages adossés à toute la maison, en leur donnant cinq coudées de hauteur, et les liant à la maison par des bois de cèdre.
11 Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
Et la parole de Yahweh fut adressée à Salomon, en ces termes:
12 “Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
« Cette maison que tu bâtis..., si tu marches selon mes lois, si tu mets en pratique mes ordonnances, si tu observes tous mes commandements, réglant sur eux ta conduite, j’accomplirai à ton égard ma parole que j’ai dite à David, ton père;
13 Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
j’habiterai au milieu des enfants d’Israël, et je n’abandonnerai pas mon peuple d’Israël. »
14 Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
Et Salomon bâtit la maison et l’acheva.
15 Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
Il revêtit intérieurement les murs de la maison de planches de cèdre, depuis le sol de la maison jusqu’au plafond; il revêtit ainsi de lambris l’intérieur; et il recouvrit le sol de la maison de planches de cyprès.
16 Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
Il revêtit de planches de cèdre les vingt coudées à partir du fond de la maison, depuis le sol jusqu’au haut des murs, et il prit sur la maison de quoi lui faire un sanctuaire, le Saint des saints.
17 Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
La maison, c’est-à-dire le temple antérieur, était de quarante coudées.
18 Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
Le bois de cèdre à l’intérieur de la maison était sculpté en coloquintes et en fleurs épanouies; tout était cèdre; on ne voyait pas la pierre.
19 Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
Salomon disposa le sanctuaire à l’intérieur de la maison, au fond, pour y placer l’arche de l’alliance de Yahweh.
20 Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
L’intérieur du sanctuaire avait vingt coudées de longueur, vingt coudées de largeur et vingt coudées de hauteur. Salomon le revêtit d’or fin, et il revêtit l’autel de cèdre.
21 Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
Salomon revêtit d’or fin l’intérieur de la maison, et il ferma avec des chaînes d’or le devant du sanctuaire, qu’il couvrit d’or.
22 Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
C’est ainsi qu’il revêtit d’or toute la maison, la maison toute entière, et il revêtit d’or tout l’autel qui était devant le sanctuaire.
23 Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
Il fit dans le sanctuaire deux chérubins de bois d’olivier sauvage, ayant dix coudées de haut.
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
Une des ailes de chaque chérubin avait cinq coudées, et la deuxième aile du chérubin avait cinq coudées; il y avait dix coudées de l’extrémité d’une de ses ailes à l’extrémité de l’autre.
25 Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
Le second chérubin avait aussi dix coudées. Même mesure et même forme pour les deux chérubins.
26 Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
La hauteur d’un chérubin était de dix coudées; et de même pour le deuxième chérubin.
27 Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
Salomon plaça les chérubins au milieu de la maison intérieure, les ailes déployées; l’aile du premier touchait à l’un des murs, et l’aile du second chérubin touchait à l’autre mur, et leurs autres ailes se touchaient, aile contre aile, vers le milieu de la maison.
28 Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
Et Salomon revêtit d’or les chérubins.
29 Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
Il fit sculpter en relief, sur tous les murs de la maison, tout autour, à l’intérieur comme à l’extérieur, des chérubins, des palmiers et des fleurs épanouies.
30 Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
Il revêtit d’or le sol de la maison, à l’intérieur comme à l’extérieur.
31 Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
Il fit à la porte du sanctuaire des battants de bois d’olivier sauvage; l’encadrement avec les poteaux prenait le cinquième du mur.
32 Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
Sur les deux battants en bois d’olivier sauvage, il fit sculpter des chérubins, des palmiers et des fleurs épanouies, et il les revêtit d’or, étendant l’or sur les chérubins et sur les palmiers.
33 Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
De même il fit, pour la porte du temple, des poteaux de bois d’olivier sauvage, qui prenaient le quart du mur,
34 Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
et deux battants en bois de cyprès; le premier battant était formé de deux feuillets qui se repliaient; le deuxième battant était pareillement formé de deux feuillets qui se repliaient.
35 Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
Il y sculpta des chérubins, des palmiers et des fleurs épanouies, et il les revêtit d’or, adapté à la sculpture.
36 Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
Il bâtit le parvis intérieur de trois rangées de pierres de taille et d’une rangée de poutres de cèdre.
37 Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
La quatrième année, au mois de ziv, furent posés les fondements de la maison de Yahweh;
38 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.
et la onzième année, au mois de bul, qui est le huitième mois, la maison fut achevée dans toutes ses parties et telle qu’il convenait. Salomon la construisit dans l’espace de sept ans.